Katika kipindi cha muongo mmoja uliopita, Tanzania imeshuhudia ongezeko kubwa la magonjwa sugu yasiyoambukiza kama Kansa, Kisukari, Presha, Tezi dume, Mvurugiko wa hedhi na homoni kwa wanawake, Baridi yabisi na Henia. Pamoja na maendeleo ya tiba za kisasa, hali ya afya ya wananchi inaonekana kuzidi kuwa tete, huku wengi wakielekea kurejea katika tiba za asili kama mbadala wa matibabu ya kisasa yasiyotoa nafuu ya kudumu.
Takwimu hazidanganyi:
Kwa mujibu wa ripoti ya Wizara ya Afya ya mwaka 2010, asilimia 6.5 ya Watanzania walikuwa wanaishi na Kisukari, huku Kansa ikihusishwa na asilimia 2.3 ya vifo vya kila mwaka. Hata hivyo, kufikia mwaka 2023, idadi hiyo imeongezeka kwa kiasi kikubwa ambapo Kisukari kinawakumba asilimia 11.2 ya Watanzania, ongezeko la asilimia 72.3, na Kansa kuchangia asilimia 5.1 ya vifo, ongezeko la zaidi ya mara mbili.
Ripoti ya Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (2023) inaonyesha kuwa wagonjwa wanaopokea matibabu ya Kansa wameongezeka kutoka 24,000 mwaka 2010 hadi zaidi ya 61,000 mwaka 2023.
Hali hii inaibua hoja nzito juu ya uwezo wa mfumo wa sasa wa afya kukabiliana na changamoto hizi. Ndiyo maana wataalamu wengi wa afya na wananchi wameanza kuangazia upya tiba asilia kama suluhisho la muda mrefu.
Tiba Asilia siyo Ushirikina
Hii inadhihirisha kuwa tiba asilia si mbadala duni, bali ni njia ya kurudisha mwili katika hali yake ya asili ya kuweza kujitibu.
Mifano Hai ya Walionufaika na Tiba Asilia
Asajile Mwambona, mkazi wa Mwanjelwa Mbeya, alikuwa akisumbuliwa na Kisukari kwa miaka tisa bila mafanikio licha ya kutumia dawa za hospitali. Alipoamua kujaribu matumizi ya dawa za asili kutoka Kyela, alitumia mchanganyiko wa majani ya Mlonge na mizizi ya Mlenda pori kwa miezi sita. Sasa anaendelea na maisha bila dawa za hospitali.
Mifano ya Miti Dawa na Matumizi Yake kwa Magonjwa Mbalimbali
1. Kansa
Mlonge (majani): Saga, chemsha, kunywa vikombe viwili kila siku.
Ubuyu (unga): Kijiko kimoja asubuhi na jioni kwenye maji vuguvugu.
2. Kisukari
Mwarobaini (mizizi): Chemsha, kunywa vikombe vitatu kwa siku.
Majani ya mpapai: Tengeneza juisi, kunywa asubuhi kabla ya kula.
3. Presha
Mdalasini na asali: Lamba kijiko kila asubuhi.
Tangawizi: Chemsha vipande, kunywa kikombe kila asubuhi na jioni.
4. Tezi Dume
Mbegu za maboga: Kijiko kimoja kila siku.
Mizizi ya mpera: Chemsha, kunywa kikombe baada ya chakula.
5. Mvurugiko wa Hedhi/Homoni
Mchaichai + majani ya kitunguu saumu: Chemsha pamoja, kunywa mara mbili kwa siku.
Tangawizi + mdalasini: Saga pamoja, tumia kama chai.
6. Baridi Yabisi (Arthritis)
Mizizi ya mlenda pori: Chemsha, unywe mara tatu kwa siku.
Mlonge (unga wa majani): Tumia kijiko kimoja kwenye uji au maji moto mara mbili kwa siku.
7. Henia
Mizizi ya mchungwa mwitu: Chemsha, unywe kikombe kila siku.
Mzambarau pori (magome): Saga, changanya na asali, lamba mara mbili kwa siku.
Mchango wa Serikali Kupitia Baraza la Tiba Asilia
Serikali kupitia Baraza la Tiba Asilia na Tiba Mbadala (BTATTM) inasajili waganga, kuthibitisha dawa na kufuatilia matumizi salama.
Prof. Japhet Otieno, mwenyekiti wa sasa, anabainisha kuwa baraza tayari limesajili zaidi ya dawa 200, na linaendelea na tafiti kwa lengo la kutambulika kimataifa.
Wauzaji wa Dawa za Asili: Kati ya Faida na Changamoto
1. Wachimbaji/Wakusanyaji
2. Wauzaji Masokoni/Maonesho
Onyo kwa Wauzaji: Dawa Si Biashara Tu
Serikali imeweka sheria kali dhidi ya wauzaji wa dawa zisizothibitishwa au tiba zisizo halali.
.jpeg)

Ili uwe mwanaharakati katika jambo fulani, ni lazima usajiliwe katika nchi husika. Kama umefungua shirika la kiraia kitaifa au kimataifa, ni lazima ufanye kazi iliyosajiliwa na si vinginevyo, kama unakuja kumuona rafiki yako, karibu na uende, kwanini unaita waandishi wa habari (Media Press)? Kwanini uzungumzie masuala ya kisiasa katika nchi ambayo wewe sio raia wa nchi hiyo? Tena kwa uchochezi? Lengo ni nini?
Katika sheria ya vyama vya siasa Tanzania ya mwaka 2019 kifungu cha 6C (4) kinakataza mtu ambae sio raia wa Tanzania kushiriki katika chama cha siasa au harakati za kisiasa. Aidha ili uweze kushiriki kazi za uwakili katika nchi yoyote (Participation of advocatism outside territory/Transnational advocacy), unapaswa kuomba kibali kutoka katika nchi husika ili kushiriki kazi za uwakili. Sheria ya uwakili kifungu cha 39-48 kinaeleza wazi uhalali wa kuwa wakili katika mashauri mahakamani. Martha Wangari Karua sio wakili wa kesi husika na hana kibali, Mama Karua sio mtanzania ni raia wa taifa jingine, hana uhalali wa kisheria kuja Tanzania na kushiriki au kuzungumzia masuala ya kisiasa.
Martha Wangari Karua aliwahi kugombea urais wa Kenya 2013 kupitia chama cha National Rainbow Coalition-Kenya (Narc-Kenya) na mgombea mwenza wa Raila Odinga mwaka 2022. Ni mwanasiasa nchini kenya, hakupaswa kuja Tanzania na kuanza shughuli za kisiasa, hakuna mkataba wa kimataifa au wa Afrika ya Mashariki unaoruhusu kuvuka mipaka ya nchi na kufanya siasa pasipo uhalali bila kuwa raia halali.
Mh. Rais Samia Suluhu Hassan kwakuwa ni mwenye busara, mwanadiplomasia nguli kwa kuzingatia umoja wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki amefanya huruma kumrudisha nchini kwao, alitakiwa Martha Wangari Karua akamatwe na kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kulipa fine, kufungwa jela au vyote kwa pamoja.
Akajaribu alichokifanya Tanzania huko nchini China, Vietnam na kwingine!!
Na:Mwanasheria Ally Babu (LL. B, LL.M-International Criminal Justice) – 0767126969



.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
