Articles by "MAKALA"
Showing posts with label MAKALA. Show all posts
Na “Mzee wa Atikali” ✍️✍️✍️
Simu: 0754 744 557
Ijumaa, Novemba 7, 2025
Utangulizi

Katika taarifa iliyochapishwa na Nyasa Daily, Mwanasheria Mkuu wa Malawi, Mhe. Thabo Nyirenda, ametunukiwa tuzo ya “Mwanasheria Mkuu Bora Barani Afrika” kwa mchango wake katika kuimarisha utawala wa sheria, uadilifu, na ushujaa katika kusimamia haki.

Hata hivyo, kwa kuzingatia historia ndefu ya bara letu, kuna majina mengine yaliyowahi kung’aa kwa ubora na uadilifu katika taaluma ya sheria. Miongoni mwao ni marehemu Bashiru Swanzy wa Ghana, Charles Njonjo wa Kenya, na kwa heshima kubwa, Mhe. Jaji Joseph Sinde Warioba wa Tanzania.

Makala hii inamchambua Mhe. Warioba kama kielelezo cha ubobevu, uadilifu, ujasiri, na uzalendo wa kweli katika kutetea misingi ya kisheria na maadili ya kitaifa.
Mwanasheria wa Uadilifu na Ujasiri

Mhe. Warioba, ambaye aliwahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia mwaka 1976 hadi 1985, ni miongoni mwa viongozi waliotambulika kwa uthabiti wa maadili, bidii ya kazi, na ushujaa wa kusimamia ukweli bila woga.
Ni mwanasheria mwenye weledi wa hali ya juu ambaye amewahi kuhudumu hadi ngazi ya kimataifa kama Jaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Umoja wa Mataifa. Heshima kubwa anayopata kitaifa na kimataifa ni matokeo ya maisha yake yaliyosimama imara katika misingi ya haki, ukweli, na uwajibikaji.

Uthabiti Mbele ya Nguvu ya Kiongozi

Wakati wa utawala wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, viongozi wengi walikuwa na heshima kuu na wakati mwingine woga kwa Rais huyo mwenye hekima na uthabiti wa kimaamuzi. Hata hivyo, Mhe. Warioba alisimama tofauti. Alimheshimu Rais Nyerere kwa dhati, lakini hakuwahi kuogopa kumwambia ukweli pale alipoona sheria inavunjwa.

Mfano wa wazi ni kisa cha “Msala wa Majaji”, ambapo Mhe. Warioba alikataa shinikizo la Rais Nyerere kutumia dissenting opinion kumwondoa jaji ambaye kamati ya uchunguzi ilikuwa imemwachia huru. Kwa uthabiti na ujasiri, alisisitiza kuwa kufanya hivyo kungekuwa kinyume na Katiba ya mwaka 1977.

Uthubutu huo wa kisheria unamtofautisha na wanasheria wengi wa bara hili. Ni nadra kupata Mwanasheria Mkuu mwenye ujasiri wa kumweleza Rais wake asivunje Katiba.
Uadilifu Katika Uteuzi

Kisa kingine ni lile la Mhe. Chediel Mgonja, aliyeteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga mwaka 1983 baada ya kuvuliwa ubunge na Mahakama ya Rufaa kwa kosa la rushwa. Mhe. Warioba alipoona tangazo hilo, alikwenda moja kwa moja Ikulu kumwonya Rais Nyerere kuwa uteuzi huo ni kinyume cha Katiba.

Awali, Rais Nyerere alikasirika, lakini baadaye alitafakari na kukubali hoja za kisheria za Mhe. Warioba, akatengua uteuzi huo na hata kumuomba radhi hadharani mbele ya Waziri Mkuu Edward Sokoine.

Kitendo hicho si tu kilionesha uadilifu wa Mhe. Warioba, bali pia kilidhihirisha namna alivyopata heshima ya kweli kutokana na ujasiri na ukweli wake.
Upinzani Dhidi ya Sheria Kandamizi

Mwaka 1984, wakati Baraza la Mawaziri likijadili Muswada wa Sheria ya Uhujumu Uchumi, Mhe. Warioba alikosoa kwa uwazi vifungu vilivyokuwa vinavunja haki za binadamu, akisisitiza kwamba sheria hiyo ilikuwa na mapungufu makubwa.

Alipokosa kusikilizwa, alitishia kujiuzulu, akiamini kwamba utekelezaji wa sheria isiyo na haki ni kinyume na misingi ya utawala bora. Baadaye, kwa ujasiri uleule, aligoma kutekeleza agizo la Rais na Waziri Mkuu la kutoa dhamana kwa mtuhumiwa, akisisitiza kuwa sheria hairuhusu. Hatimaye, hoja zake zilizingatiwa, na Bunge likafanya marekebisho ya haraka Juni 1984 — ikiweka rekodi kama mojawapo ya sheria zilizorekebishwa ndani ya muda mfupi zaidi.

Hitimisho

Mhe. Jaji Joseph Sinde Warioba ni mfano halisi wa Mwanasheria Mkuu anayekidhi vigezo vyote vya ubora: ubobevu wa taaluma, uadilifu wa hali ya juu, bidii, ujasiri, na uthabiti katika kutetea sheria.

Kwa weledi wake, ujasiri wake mbele ya mamlaka, na uaminifu wake usiotetereka, Mhe. Warioba amejijengea heshima isiyofutika katika historia ya Afrika.

Katika enzi za sasa ambapo baadhi ya viongozi wanayumbishwa na maslahi binafsi, historia ya Mhe. Warioba inabaki kuwa somo kwa vizazi vijavyo kuhusu maana halisi ya utumishi wa umma, uadilifu, na utii wa Katiba.

With permission from:
“Mzee wa Atikali” ✍️✍️✍️
Simu: 0754 744 557
Ijumaa, Novemba 7, 2025

“God bless you with great health, Mhe. Warioba — you remain an enduring inspiration.” 🌿
Na Mwandishi wa Makala za Moto

Katika kipindi cha muongo mmoja uliopita, Tanzania imeshuhudia ongezeko kubwa la magonjwa sugu yasiyoambukiza kama Kansa, Kisukari, Presha, Tezi dume, Mvurugiko wa hedhi na homoni kwa wanawake, Baridi yabisi na Henia. Pamoja na maendeleo ya tiba za kisasa, hali ya afya ya wananchi inaonekana kuzidi kuwa tete, huku wengi wakielekea kurejea katika tiba za asili kama mbadala wa matibabu ya kisasa yasiyotoa nafuu ya kudumu.

Takwimu hazidanganyi:

Kwa mujibu wa ripoti ya Wizara ya Afya ya mwaka 2010, asilimia 6.5 ya Watanzania walikuwa wanaishi na Kisukari, huku Kansa ikihusishwa na asilimia 2.3 ya vifo vya kila mwaka. Hata hivyo, kufikia mwaka 2023, idadi hiyo imeongezeka kwa kiasi kikubwa ambapo Kisukari kinawakumba asilimia 11.2 ya Watanzania, ongezeko la asilimia 72.3, na Kansa kuchangia asilimia 5.1 ya vifo, ongezeko la zaidi ya mara mbili.

Ripoti ya Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (2023) inaonyesha kuwa wagonjwa wanaopokea matibabu ya Kansa wameongezeka kutoka 24,000 mwaka 2010 hadi zaidi ya 61,000 mwaka 2023.

Hali hii inaibua hoja nzito juu ya uwezo wa mfumo wa sasa wa afya kukabiliana na changamoto hizi. Ndiyo maana wataalamu wengi wa afya na wananchi wameanza kuangazia upya tiba asilia kama suluhisho la muda mrefu.

Tiba Asilia siyo Ushirikina

Mmoja wa wataalamu maarufu duniani katika tiba asilia, Dk. Sebi (Alfredo Darrington Bowman), alipata kusema:
"Mwili wa binadamu hauugui kwa sababu ya kukosa kemikali; unaugua kwa sababu ya ukosefu wa uwiano wa asili. Tiba asilia huleta huo uwiano."

Naye Profesa Patrick Ogwang wa Uganda, mtafiti wa tiba asilia na mvumbuzi wa dawa ya COVID-19 ya Covidex alisema:
"Ukiupa mwili kile unachokihitaji kutoka kwa mimea, huhitaji kuutibu tena kwa dawa za viwandani."

Hii inadhihirisha kuwa tiba asilia si mbadala duni, bali ni njia ya kurudisha mwili katika hali yake ya asili ya kuweza kujitibu.

Mifano Hai ya Walionufaika na Tiba Asilia

Asajile Mwambona, mkazi wa Mwanjelwa Mbeya, alikuwa akisumbuliwa na Kisukari kwa miaka tisa bila mafanikio licha ya kutumia dawa za hospitali. Alipoamua kujaribu matumizi ya dawa za asili kutoka Kyela, alitumia mchanganyiko wa majani ya Mlonge na mizizi ya Mlenda pori kwa miezi sita. Sasa anaendelea na maisha bila dawa za hospitali.

James Mabula wa Mlowo Mbozi alikuwa akisumbuliwa na presha ya kupanda kwa zaidi ya miaka mitano. Mizizi ya porini aliyoinunua kutoka kwa mtaalamu Joseph Mwalwande ilimsaidia.
"Sikuijua ni mizizi ya aina gani, lakini baada ya wiki mbili, presha ilianza kushuka," anasema.

Mifano ya Miti Dawa na Matumizi Yake kwa Magonjwa Mbalimbali

1. Kansa

Mlonge (majani): Saga, chemsha, kunywa vikombe viwili kila siku.

Ubuyu (unga): Kijiko kimoja asubuhi na jioni kwenye maji vuguvugu.

2. Kisukari

Mwarobaini (mizizi): Chemsha, kunywa vikombe vitatu kwa siku.

Majani ya mpapai: Tengeneza juisi, kunywa asubuhi kabla ya kula.

3. Presha

Mdalasini na asali: Lamba kijiko kila asubuhi.

Tangawizi: Chemsha vipande, kunywa kikombe kila asubuhi na jioni.

4. Tezi Dume

Mbegu za maboga: Kijiko kimoja kila siku.

Mizizi ya mpera: Chemsha, kunywa kikombe baada ya chakula.

5. Mvurugiko wa Hedhi/Homoni

Mchaichai + majani ya kitunguu saumu: Chemsha pamoja, kunywa mara mbili kwa siku.

Tangawizi + mdalasini: Saga pamoja, tumia kama chai.

6. Baridi Yabisi (Arthritis)

Mizizi ya mlenda pori: Chemsha, unywe mara tatu kwa siku.

Mlonge (unga wa majani): Tumia kijiko kimoja kwenye uji au maji moto mara mbili kwa siku.

7. Henia

Mizizi ya mchungwa mwitu: Chemsha, unywe kikombe kila siku.

Mzambarau pori (magome): Saga, changanya na asali, lamba mara mbili kwa siku.

Mchango wa Serikali Kupitia Baraza la Tiba Asilia

Serikali kupitia Baraza la Tiba Asilia na Tiba Mbadala (BTATTM) inasajili waganga, kuthibitisha dawa na kufuatilia matumizi salama.

Prof. Hamis Malebo aliwahi kusema:
"Tunachofanya sisi siyo kuzuia tiba asilia, bali kuhakikisha zinatumika kwa usahihi na usalama kwa watumiaji."

Prof. Japhet Otieno, mwenyekiti wa sasa, anabainisha kuwa baraza tayari limesajili zaidi ya dawa 200, na linaendelea na tafiti kwa lengo la kutambulika kimataifa.

Wauzaji wa Dawa za Asili: Kati ya Faida na Changamoto

1. Wachimbaji/Wakusanyaji


Mfano ni Mbaraka Matete wa Morogoro:
"Naenda hadi misitu ya Uluguru kutafuta mizizi. Naandaa dawa na kuwauzia wauzaji kutoka mikoa mbalimbali."

2. Wauzaji Masokoni/Maonesho


Mfano ni Mama Riziki wa Kariakoo na Yohana Kisamo wa Maonesho ya Nanenane Morogoro.

Onyo kwa Wauzaji: Dawa Si Biashara Tu

Dk. Zakaria Mshana wa Ifakara anaonya:
"Kuuza dawa bila uelewa ni sawa na kumpa mtu sumu akidhani ni tiba."

Serikali imeweka sheria kali dhidi ya wauzaji wa dawa zisizothibitishwa au tiba zisizo halali.

Ni nadra sana kwa mwanasiasa wa kiafrika kuamua kutogombea uchaguzi uliopo mbele yake, wanasiasa wetu wengi wanapenda sana kuongoza or madaraka na hawatoki mpaka walazimishwe.

Uamzi wa Kassim Majaliwa, ambaye sasa bado ni Waziri Mkuu wa Tanzania umewashangaza wengi sana ndani na nje ya nchi.

Hatujazoea kusikia busara kama hii ya kuchukua uamzi wa kutogombea tena nafasi ya ubunge ambayo inaaminika na wengi kuwa ni nafasi ya utajiri au ya kujitajirisha, na ndiyo maana inafuatwa na watu wengi hata wenye taaluma yao ya ualimu, uinjinia na uprofesa wa hiki na kile, sambamba na matumizi makubwa ya fedha za kununua kura.

Kwa nchi za wenzetu ambako uongozi wa kisiasa wanauchukulia kama ni utumishi wa umma, suala la uongozi kwao si la kufa na kupona. Watu wengi huko wanaingia kwenye nafasi za kisiasa mara nyingi kwa kufuatwa na wananchi, na wakishakubali watakuja kutekeleza majukumu waliyopewa na wananchi basi, na wakishamaliza tu muda wao hawahangaiki kujiandaa na uchaguzi ujao, wanaacha na kwenda kufanya mambo yao binafsi.

Majaliwa ni nani na yukoje? Sina historia yake ya tangu kuzaliwa na malezi yake ya familia, shule, jamii alimolelewa, zaidi tu nafahamu kuwa yeye ni Mwalimu na ameingia kwenye siasa wakati wa utawala wa Rais Jakaya Kikwete na kuteuliwa kuwa Waziri wa Tamisemi akitokea ualimu, kisha Waziri Mkuu wakati wa Rais John Magufuli kwa vipindi vyote vya awamu ya tano (2015 - 2025).

Kwenye uongozi wake, Majaliwa ameonyesha mambo mengi ya kiuongozi ambayo yamepelekea watanzania wengi kuwa na imano na matumaini naye, kwamba ikitokea akagombea nafasi ya u_rais basi anafaa kuwa Rais wa Tanzania.

Anazo sifa nyingi lakini nitaje chache,

Kwanza, Kassim Majaliwa ni mtu makini na mtulivu na anayependa kuongoza kisayansi na si kisiasa zetu za "michakato, au umbea, majungu, uongo na fitina pamoja na kuviziana".

Pili, Majaliwa ni mvumilivu sana na ni muungwana asiye na papara. Yapo mambo ambayo hata watanzania wameona akifanyiwa lakini kwake hayakuwa kitu, alionesha haiba mpaka hata sasa.

Na kuna wakati aliweza kukemewa na hata kupewa maagizo na watu alioshiriki kuwateua mwenyewe kwenye nafasi walizonazo na akakaa kimya au kufuata hayo maagizo bila ya chuki.

Ni Kassim Majaliwa ambaye, wakati mwingine alikuwa akifanya kazi ambazo zingeweza kufanywa na wasaidizi wake (mawaziri) lakini alifanya yeye bila kujali udogo wa shughuli yenyewe.

Sitaki kusema mengi, lakini lipo jambo la kujifunza kwa Majaliwa nalo ni kwamba, hakuna kitu kizuri kama kuyaacha madaraka wakati bado yanakuhitaji, na vile vile kuyaachia madaraka ikiwa wananchi bado wanakupenda.

Mungu aendelee kumtunza Kassm Majaliwa wa watanzania, hakika bado tunamhitaji sana ktk taifa letu, kama sio leo basi

Kwiyeya Singu. 0784977072

Na Mwandishi Wetu.

Alizaliwa mwaka 1960 katika kijiji kidogo cha Namoto, wilayani Ruangwa, mkoani Lindi. Leo hii, jina la Kassim Majaliwa Majaliwa linaandikwa kwa heshima kubwa katika historia ya Tanzania. Safari yake ni ya kuvutia kutoka maisha ya kawaida kabisa hadi kuwa mmoja wa viongozi wa juu kabisa wa taifa.
‎Kiu yake kubwa ilikuwa ni kufundisha, hivyo hakuchelewa alisomea ualimu katika Chuo cha Ualimu Mtwara na baadaye Chuo cha Ualimu Kitangali kilichopo Mtwara.
‎Alianza kuwa mwalimu, akilea vijana kwa bidii na maadili, Akawa mkufunzi katika Chuo cha Ualimu mtwara huku akijijengea misingi imara kwa huduma ya jamii,
‎Hakika alijitengeneza kama kiongozi mwenye maarifa, nidhamu, na mwelekeo wa maendeleo kwa taifa.
Kiu yake ya kujifunza iliendelea hadi alipopata shahada kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (Open University of Tanzania).
‎Majaliwa aliyeanzia ualimu, ukufunzi wa chuo cha ualimu, ukatibu wa chama cha walimu, Ukuu wa wilaya ya Rufiji, Unaibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu tawala za mikoa na Serikali za motaa TAMISEMI yana hatimaye Waziri Mkuu wa –
‎ leo ameandika historia isiyo futika katika taifa letu.
‎CHAMA CHA WALIMU MKOA WA SINGIDA CWT wanamkumbuka zaidi hasa kipindi ambacho alianzisha, kusimamia na kukamilisha ujenzi wa jengo la ghorofa la ofisi za chama cha walimu mkoani Singida alipokuwa akihudumu kama Katibu wa CWT mkoani Singida.
‎Majaliwa amechagua historia imjadili katika maisha yake yote.
Rais mstaafu Jakaya Kikwete aliiona nyota ya Majaliwa kutokea Singida, akamteua kuwa Mkuu wa Wilaya ya Urambo alipowekwa kiti moto na wabunge wawili wababe wa wilaya hiyo – marehemu Samuel Sitta na Juma Kapuya waliokuwa wabunge wa Jimbo la Urambo na Kaliua.
‎Hamad, Majaliwa akahamishiwa wilaya ya Rufiji alipohudumu hadi mwaka 2010 ndipo alipoamua kujitosa jimboni Ruangwa kugombea ubunge wa jimbo hilo.
‎Hakika nyota njema iliyoanzia ualimu haikazimika baada ya uchaguzi huo ambapo siku anawaaga watumishi wa wilaya ya Rufiji alikohudumu kama mkuu wa wilaya baada ya kushinda ubunge.
‎Katikati ya maandalizi ya kuelekea jimboni, analisikia jina lake akiwa miongoni mwa manaibu mawaziri wa serikali ya Jakaya Mrisho Kikwete.
‎Mwaka 2010, alichaguliwa kuwa Mbunge wa Ruangwa, kutokana ile kasi yake ya utendaji, jicho la hayati John Pombe Joseph Magufuli lilimuona Novemba 2015 na kumteua kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania.
‎Mtu mwema aliyewahi kutokea katika ardhi ya nchi yetu.
Leo hii tunamzungumzia Kasim Majaliwa
‎Kiongozi imara ambaye ameziishi Enzi na kuziheshimu nyakati zake
‎Kwa ridhaa yake mwenyewe Ameamua kuuwaga Waziri Mkuu baada ya kutangaza kutogombea ubunge wa Ruangwa.
‎Vyovyote iwavyo, vyovyote itakavyotafsiriwa, na vyovyote itakavyoonekana – lakini ukweli usemwe, Majaliwa ameandika historia yake. Sio rahisi kwa kiongozi wa ngazi yake kuamua kung’atuka na kuachia madaraka makubwa kama Uwaziri Mkuu.
‎Watangulizi wake kadhaa iliwabidi wastaafu siasa baada ya kushindwa kupata uteuzi wa nafasi ya juu baada ya kuhudumu kama Waziri Mkuu. Naam, tulimuona hayati Msuya akishindwa urais na hayati Mkapa ndipo akastaafu rasmi siasa mwaka 1995. Ilimchukua hadi kushindwa urais na Jakaya Kikwete mwaka 2005 ndipo akaamua kuistaafu rasmi siasa na kuitwa Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye. Sio hao tu, hata Mizengo Pinda ilimbidi ashindwe kwanza kura za maoni za urais mwaka 2015 na kuteuliwa Magufuli ndipo akatangaza kustaafu siasa.
‎Tofauti kabisa na Majaliwa Kassim Majaliwa aliyetangaza kutogombea tena ubunge wa Ruangwa. Ifahamike kuwa kutokugombea ubunge ni sawa na kusema ameamua kustaafu Uwaziri Mkuu, kwa sababu hauwezi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kama hautokani na ubunge wa kuchaguliwa jimboni. Hii ndiyo kusema kuwa Majaliwa amestaafu rasmi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania.

Amestaafu akiwa bado ana nguvu, ana nishati na uwezo wa kuendelea kuwa mtumishi mwandamizi wa serikali. Waziri Mkuu mwenye historia ya utumishi uliojaa uadilifu na kujitolea. Ni kiongozi wa kipekee anayestaafu mapema kuliko waliomtangulia, lakini akiacha alama ya kudumu. Kassim Majaliwa ni kielelezo cha uongozi wa kweli – unaotanguliza maadili, unyenyekevu, na maslahi ya taifa kuliko jina binafsi.
‎Tanzania itamkumbuka daima kama mtumishi mwadilifu, ambaye alitumikia taifa kwa moyo wote – kwa utulivu, busara, na heshima ya juu. Hongera sana Majaliwa, tumeuona na kuuonja utamu wa utumishi wako kama Waziri Mkuu wa nchi hii.
Hakika wewe ni shujaa unayestahili kukumbukwa, ni mwamba unayehitaji kuegemewa.
‎Unaanza maisha mapya ya ustaafu ukiwa na nguvu na maarifa mapana kiasi cha kuwa mshauri bora kwa wa watakaoendelea madarakani.
‎Itoshe kusema umafanya kila ulichotakiwa kufanya katika nchi, Taifa limafaidika katika kila idara ulipokwepo
‎Sasa ni muda wa wajukuu kufurahia wema wa Babu Kasim Majaliwa
‎Kila la heri, Fahari ya Kusini.
‎Kila la heri, Mpiganaji.
Na Happiness Katabazi.

RAIS Samia Suluhu Hassan Leo amemteua Jaji wa Mahakama ya Rufani George Mcheche Masaju Kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania.

Kwa Mujibu wa taarifa kwa umma iliyosainiwa na Katibu Mkuu Kiongozi Leo Juni 13 imesema ...

Hongera sana mtani na rafiki yangu Masaju kuteuliwa kuwa Jaji Mkuu .

Januari 10 mwaka 2025 , Rais Samia alimteua Jaji Masaju kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.

Aprili 21 mwaka 2023 , Rais Samia aliteua Jaji Masaju kuwa Mshauri wake wa masuala ya Sheria ( Advisor to the President - Legal Affairs) Na wakati akimteua kushika nafasi hiyo Jaji Masaju alikuwa ni Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma.

Novemba 5 mwaka 2015 , Masaju aliteuliwa mara ya pili kushika wadhifa wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Rais wa awamu ya Tano Marehemu Dr. John Magufuli ndiye akimteua Masaju kuwa AG .

Mara ya kwanza ilikuwa ni serikali ya awamu ya nne Januari 2 Mwaka 2015, Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambaye amestaafu wadhifa wa Cheo cha Rais , alimteua Masaju Kuwa Mwanasheria Mkuu wa serikali ikiwa ni siku chake aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema ambaye kwasasa ni marehemu kujihudhuru wadhifa huo.

February mosi mwaka 2018 Rais Magufuli alimteua Masaju kuwa Jaji wa Mahakama Kuu nchini.

Masaju ni miongoni mwa Wanasheria wa serikali wazalendo na wanaowaaminiwa kiutendaji na ndiyo maana zilipokuwa zikifunguliwa Kesi ambazo zilikuwa zikivuta hisia za watu Wengi Masaju alikuwa akivaa suti na gauni lake la uwakili na kutinga Mahakama ya Rufaa, Mahakama Kuu na kuiendesha Kesi hiyo yeye Mwenyewe akisaidiwana na vijana wake.

Na nilipokuwa Mwandishi wa Habari za mahakamani,nilipokuwa nikimuona Masaju Kubeba gauni jeusi na begi lilokuwa na Nyaraka za kuendeshea Kesi basi nilikuwa Nasema Kimolo moyo Kuwa upande wa wa pili Katika Kesi hiyo ujiandae kikamilifu .

Ushahidi mchache wa haya ninayoyasema kuhusu Masaju ambayo nilikushuhudia kwa macho yangu mwanzo hadi Mwisho ni Rufaa ya Kesi maarufu ya mgombea Binafsi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya Mchungaji Christopher Mtikila Katika Mahakama ya Rufaa nchini Masaju alikuwa kiongozi wa Mawakili wa serikali kuendesha Kesi hiyo ya kihistoria ambayo ikisikilzwa na jopo la Majaji Saba waliokuwa wakiongozwa na Jaji Mkuu wa wakati huo , Agustino Ramadhani, Masaju alifanikiwa Kujenga hoja na hatimaye jopo lilikubaliana naye na kutengua hukumu ya Mahakama Kuu ambayo iliruhurusu Mgombea Binafsi.

Ushahidi wa pili, ni Mwaka 2014, katika kesi ya Kikatiba Na.24/2013 , Masaju aliwakilisha upande wa Mwanasheria Mkuu Katika Kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa na Kituo ca Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) pamoja na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS)dhidi ya Waziri Mkuu iliyokuwa ukiomba Mahakama Kuu itoe Tafsiri ya Ibara ya 100 Kuwa wabunge wana Uhuru bila mipaka kwani Pinda alitoa Kauli Bunge akitaka Polisi iwapige wanaovunja Sheria za nchi.

Juni 6 Mwaka 2014 , Jopo la Majaji wa Tatu wa Mahakama Kuu Dar es Salaam, Fakji Jundu, Dk.Fauz Twaibu na Augustine Mwarija walitoa uamuzi wa Kuitupa Kesi hiyo kwa sababu Imeona walalamikaji walikuwa hawana Haki ya kisheria ya kushitaki Pinda.

Jopo hilo lilitoa uamuzi huo ambapo jaji Jaji Jundu alisema anakubaliana na pingamizi la awali lilowasilishwa na wakili wa mdaiwa (Pinda), Ambaye ni Naibu Mwanasheri Mkuu wa Serikali, George Masaju, ambalo lilikuwa likiomba Mahakama itoe amri ya kuifuta Kesi hiyo kwasababu walalamikaji hawana Haki a kisheria ya kuwashitaki wadaiwa na kwamba Waliokuwa na Haki ya kushitaki Pinda ni wananchi na siyo Taasisi hizo za walalamikaji.

LHRC na TLS walimshtakiwa Waziri Mkuu Pinda pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kauli aliyoitoa bungeni Juni 20 mwaka 2013.Ilidaiwa Katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo Waziri Pinda akijibu alisema, ‘ukifanya fujo…unaambiwa usifanye hiki ukaamua kukaidi, utapigwa tu, muwapige tu sababu tumechoka’.

Jaji Jundu alisema, Masaju Aliwasilisha pingamizi la awali akiomba kesi hiyo itupwe kwa sababu mahakama hiyo haina uwezo wa kuisikiliza, waliofungua hawakustahili kuifungua na iko kwa ajili ya kupoteza MUDa wa Mahakama.

Katika uamuzi huo, majaji walikubaliana na hoja tatu za pingamizi kuwa walalamikaji katika kesi hiyo hawakuwa na haki ya kufungua kesi hiyo na kwamba walikosea taratibu za ufunguaji wa kesi kama hizo kwa kuwa walikiuka amri na kanuni zinazoongoza Mashauri ya Madai (CPC).

Katika hoja ya kwanza kuwa Pinda kama mbunge analindwa na Katiba, jopo hilo lilisema kuwa ni kweli wabunge wanalindwa na Katiba Ibara ya 100 (1) kuhusu haki na upendeleo (Previledge), yaani haki na uhuru wa mjadala na maoni. Hata hivyo, lilikataa hoja za utetezi kuwa wabunge wana kinga isiyo na mipaka ya kutokushtakiwa kwa kauli au jambo lolote walilolitamka bungeni.

“Ibara ya 100(1) ya Katiba haiwezi kujadiliwa mahali popote ikiwemo mahakamani, ibara hiyo inasema kwamba, kutakuwa na uhuru wa mawazo, majadiliano na utaratibu katika Bunge na uhuru huo hautavunjwa wala kuhojiwa na chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano au katika mahakama au mahali penginepo nje ya Bunge.

“Ibara ya 100(2) inaweza kujadiliwa mahakamani, inasema kwamba bila kuathiri katiba hii au masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika, Mbunge yoyote hatashtakiwa au kufunguliwa shauri la madai mahakamani kutokana na jambo lolote alilolisema au kulifanya ndani ya Bunge au alilolileta bungeni kwa njia ya maombi, muswada, hoja au vinginevyo.

“Mwananchi mmoja mmoja aliyeathirika na jambo lililozungumzwa na mbunge bungeni anaweza kushtaki lakini si taasisi kama ilivyo katika kesi hii,”alisema.

Alisema kutokana na sababu hizo, mahakama inatupilia mbali kesi hiyo kwa sababu waliofungua kesi, LHRC na TLS hawakustahili kisheria kufungua kesi hiyo kwa sababu hawakuathirika.

Kesi ya Tatu ni Kesi iliyovuta hisia za watu Wengi ni Kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa Mwaka 2014 na Mwandishi wa Habari Saed Kubenea dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.

Kubenea alikuwa anaomba Mahakama hiyo itoe amri ya muda ya Kuzuia Bunge Maalum la Katiba lisiendelee na kazi kwasababu linavunja Sheria.

Hata hivyo Masaju aliwasilisha mapingamizi mawili ambayo yaliomba Mahakama hiyo itupilie Mbali Maombi ya Kubenea Kwani hayana Msingi na Mahakama hiyo ilitupilia mbali Maombi ya Kubenea na Bunge linaendelea na kazi zake.

Mifano ni mingi ya Kuonyesha Masaju Kabla ya kuteuliwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Januari 2 na Novemba 5 Mwaka 2015 , kuna kazi nzuri ya kuiwakilisha upande wa serikali Katika Kesi mbalimbali mahakamani aliifanya hivyo anastahili.

Ni neema ya Mungu na na rekodi yake ya Utendaji Kazi ndiyo imesabisha Marais wa wawili ya marehemu Dk.John Magufuli na rais wa Sasa Samia Suluhu Hassan wakuteue kushika nyadhifa hizo ikiwemo hii ya Jaji Mkuu ambayo umeteuliwa Leo Juni 13 mwaka huo ili amsaidie kuchapa kazi.

Wosia wangu wa Masaju endelea na msimamo wako ule ule wa kusimamia haki na Kusema ukweli bila woga.

Masaju ambaye kabla ya kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa serikali na aliwahi kuwa mshauri wa Rais Kikwete katika masuala ya sheria ni mtu asiye penda kuburuzwa na mambumbumbu wa Sheria, ni mtu anayejali utu,heshima na Kupenda watu watii Sheria za nchi na ni mzalendo kwa taifa lake.

Hongera Mtani wangu Masaju, Mungu akuongoze katika nafasi hii ya Jaji Mkuu wa Tanzania.

0716 774494
6/13/2025

Ili uwe mwanaharakati katika jambo fulani, ni lazima usajiliwe katika nchi husika. Kama umefungua shirika la kiraia kitaifa au kimataifa, ni lazima ufanye kazi iliyosajiliwa na si vinginevyo, kama unakuja kumuona rafiki yako, karibu na uende, kwanini unaita waandishi wa habari (Media Press)? Kwanini uzungumzie masuala ya kisiasa katika nchi ambayo wewe sio raia wa nchi hiyo? Tena kwa uchochezi? Lengo ni nini?

Katika sheria ya vyama vya siasa Tanzania ya mwaka 2019 kifungu cha 6C (4) kinakataza mtu ambae sio raia wa Tanzania kushiriki katika chama cha siasa au harakati za kisiasa. Aidha ili uweze kushiriki kazi za uwakili katika nchi yoyote (Participation of advocatism outside territory/Transnational advocacy), unapaswa kuomba kibali kutoka katika nchi husika ili kushiriki kazi za uwakili. Sheria ya uwakili kifungu cha 39-48 kinaeleza wazi uhalali wa kuwa wakili katika mashauri mahakamani. Martha Wangari Karua sio wakili wa kesi husika na hana kibali, Mama Karua sio mtanzania ni raia wa taifa jingine, hana uhalali wa kisheria kuja Tanzania na kushiriki au kuzungumzia masuala ya kisiasa.

Martha Wangari Karua aliwahi kugombea urais wa Kenya 2013 kupitia chama cha National Rainbow Coalition-Kenya (Narc-Kenya) na mgombea mwenza wa Raila Odinga mwaka 2022. Ni mwanasiasa nchini kenya, hakupaswa kuja Tanzania na kuanza shughuli za kisiasa, hakuna mkataba wa kimataifa au wa Afrika ya Mashariki unaoruhusu kuvuka mipaka ya nchi na kufanya siasa pasipo uhalali bila kuwa raia halali.

Mh. Rais Samia Suluhu Hassan kwakuwa ni mwenye busara, mwanadiplomasia nguli kwa kuzingatia umoja wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki amefanya huruma kumrudisha nchini kwao, alitakiwa Martha Wangari Karua akamatwe na kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kulipa fine, kufungwa jela au vyote kwa pamoja.

Akajaribu alichokifanya Tanzania huko nchini China, Vietnam na kwingine!!

Na:Mwanasheria Ally Babu (LL. B, LL.M-International Criminal Justice) – 0767126969