Articles by "HABARI MAHAKAMANI"
Showing posts with label HABARI MAHAKAMANI. Show all posts
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachilia huru mfanyabiashara maarufu Jennifer Jovin, anayefahamika zaidi kwa jina la Niffer (26), pamoja na mwenzake Mika Chavala (32), baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kuondoa mashtaka dhidi yao.

Uamuzi huo umetolewa leo, Jumatano Desemba 3, 2025, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Aaron Lyamuya, mara baada ya DPP kuwasilisha hati ya Nolle Prosequi—taarifa rasmi ya kutokuwa na nia ya kuendelea na mashitaka—kwa mujibu wa kifungu cha 92(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai, marejeo ya mwaka 2023.

Hakimu Lyamuya alisema kuwa baada ya hati hiyo kuwasilishwa, mahakama haina mamlaka ya kuendelea kusikiliza shauri hilo, hivyo ililazimika kuwaachia huru washtakiwa hao mara moja.

Hati ya Nolle Prosequi hutoa mamlaka kwa DPP kusitisha mashitaka wakati wowote kabla ya hukumu kutolewa, bila kuhitaji kutoa sababu mahakamani.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju akisisitiza jambo.
---

●Atoa ahadi hiyo alipotembelea Gereza la Isanga Dodoma

●Apongeza uboreshaji huduma za magereza nchini


Na Mary Gwera, Mahakama-Dodoma.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju ameahidi kushughulikia changamoto za kimahakama zinazowakabili mahabusu na yùiwaliopo gerezani lengo likiwa ni kurahisisha upatikanaji wa haki kwa wakati.

Mhe. Masaju amebainisha hayo leo tarehe 10 Julai, 2025 wakati akizungumza na Mahabusu na Wafungwa alipotembelea Gereza Kuu la Isanga mkoani Dodoma kwa lengo la kusikiliza changamoto mbalimbali zinazowakabili wafungwa na mahabusu waliopo kwenye gereza hilo.

“Kwetu sisi hizi taarifa ambazo tumezipata hapa, malalamiko haya yatatusaidia kutambua tatizo liko wapi, hivyo yatatusaidia kubuni mikakati ya namna ya kushughulikia changamoto hizi ipasavyo na kwa ufanisi,” amesema Mhe. Masaju.

Jaji Mkuu amesema kuwa, moja ya malengo ya kutembelea Gereza hilo ni pamoja na kutekeleza maelekezo yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati alipomuapisha Mhe. Masaju kushika nafasi hiyo ambapo alimuelekeza kufanyia kazi maoni na mapendekezo ya Tume ya Haki Jinai ikiwa ni pamoja na kuangalia eneo la Magereza.

“Pamoja na kwamba ninapenda kutembelea Magereza mara kwa mara, lakini hii ziara imekuja nikiwa na sababu mahsusi, nilipoapishwa siku ile moja ya maelekezo ambayo Rais aliniambia ni kwamba niyafanyie kazi mapendekezo ya Tume ya Haki Jinai,” ameeleza Mhe. Masaju.

Ameongeza kuwa, pamoja na kwamba taarifa za Tume hiyo zipo ofisini ni muhimu kuzungumza na wahusika kwakuwa wanatoa picha halisi ya wapi pa kuanzia na kujua ni mikakati gani ya kuweka katika kushughulikia mapendekezo yaliyoainishwa na Tume ya Haki Jinai.

Akizungumzia kuhusu baadhi ya hoja, malalamiko na changamoto zilizotolewa na Mahabusu, wafungwa, Mhe. Masaju amewaahidi kuwa, yatafanyiwa kazi na matokeo yake watayaona. Amewataka pia, Mahabusu na wafungwa hao waendelee kuwa raia wema.

Baadhi ya changamoto zilizowasilishwa na mahabusu na wafungwa kupitia taarifa zao walizowasilisha mbele ya Jaji Mkuu na ujumbe alioambatana nao ni pamoja na ucheleweshaji wa vitabu vya rufani, kukosa nakala za nia, unyanyasaji katika vituo vya Polisi ikiwemo vipigo, mashahidi kutofika mahakamani kwa wakati na kadhalika.

Aidha, Jaji Mkuu amempongeza Kamishna Jenerali wa Magereza Tanzania, Jeremiah Yoram Katungu kwa kuendelea kuboresha huduma za magereza nchini.

“Nalipongeza Jeshi la Magereza kwa hatua kubwa za uboreshaji wa huduma kwa kuwa hali haikuwa hivi siku za nyuma, mimi nimekuwa nikitembelea magereza mara kwa mara, nimetembelea sehemu wanapolala wafungwa wenye adhabu za kunyongwa pameboreshwa sana tofauti na ilivyokuwa awali, vilevile nawapongeza kwa kutumia nishati safi kupikia,” amesema Mhe. Masaju.

Kwa upande wake, Kamishna Jenerali wa Magereza Tanzania, Jeremiah Yoram Katungu akitoa taarifa ya hali ya magereza mbele ya Jaji Mkuu amesema, kwa sasa kumekuwa na upungufu wa wahalifu huku akiishukuru Mahakama ya Tanzania kwa ushirikiano inaotoa pamoja na wadau wengine wa haki jinai.

"Jeshi la Magereza lina jumla ya Magereza 129 nchini, na Magereza haya yana uwezo wa kuhifadhi wahalifu 29,902, kwa tarehe 10 Julai, 2025 tumekuwa na wahalifu pungufu ya nafasi zilizopo, tunahifadhi wahalifu takribani 27,000 kwa siku na nafasi zilizopo ni 29,902 tafsiri yake ni kwamba tumekuwa na upungufu wa wahalifu kulingana na nafasi zilizopo," amesema Kamishna Jenerali Katungu.

Kadhalika, Kamishna huyo, amemshukuru Rais Samia kwa kuunda Tume ya Haki Jinai kwakuwa wamefanyika kazi mapendekezo yaliyotolewa na Tume hiyo kuhusu Magereza na manufaa yake yameanza kuonekana kwakuwa kumekuwa na upungufu wa wahalifu.

Ameongeza kwa kuushukuru Mhimili wa Mahakama kwa kuendelea kushirikiana na Jeshi hilo hususani katika usikilizwaji wa mashauri ya mahabusu na wafungwa hususani katika matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano sambasamba na kaguzi za mara kwa mara zinazofanywa na Majaji.

Mhe. Masaju amepata fursa ya kukagua maeneo kadhaa katika gereza hilo ikiwa ni pamoja na vyumba wanapolala wafungwa wa kunyongwa, jikoni na sehemu nyingine kadhaa.

Gereza la Isanga limekuwa ni Gereza la kwanza kutembelewa tangu Jaji Mkuu, Mhe. Masaju alipoteuliwa kushika nafasi hiyo. Jaji Mkuu ameambatana na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo, Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Bw. Sylvester Mwakitalu, Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Kiaki Nkya, Naibu Msajili Mwandamizi wa Mahakama ya Rufani (T), Mhe. Emmanuel Mrangu, Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Chiganga Tengwa, Mwakilishi wa Uhamiaji, Watumishi wengine wa Mahakama na wadau.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju (mwenye tai nyekundu) akifanya ukaguzi wa Gereza la Isanga leo tarehe 10 Julai, 2025 alipotembelea gereza hilo. Kushoto kwake ni Kamishna Jenerali wa Magereza Tanzania, Jeremiah Yoram Katungu.


Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju (mwenye tai nyekundu) akiwa katika eneo la Gereza la Isanga Dodoma alipofanya ziara katika gereza hilo leo tarehe 10 Julai, 2025.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju (wa pili kulia) akiwa ndani ya kasha maalum la kisasa lililotolewa na Mahakama linalotumika katika gereza hilo kuendeshea mashauri kwa njia ya mtandao bila washtakiwa kufikishwa mahakamani. Kulia kwa Jaji Mkuu ni Kamishna Jenerali wa Magereza Tanzania, Jeremiah Yoram Katungu na anayefuata ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani na kulia kwa Mhe. Dkt. Siyani ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo.

FdhtJaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju akikagua gwaride maalum aliloandaliwa na Jeshi la Magereza alipotembelea Gereza la Isanga mkoani Dodoma leo tarehe 10 Julai, 2025.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Gereza la Isanga Dodoma kwa lengo la kufanya ukaguzi.
Sehemu ya Maofisa kutoka Mahakama ya Tanzania wakifuatilia kwa makini kilichokuwa kikijiri wakati wa ziara ya Jaji Mkuu katika Gereza la Isanga mkoani Dodoma.Wa kwanza kushoto ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo, wa pili kushoto ni Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Kiaki Nkya, katikati ni Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Chiganga Tengwa, wa pili kulia ni Naibu Msajili Mwandamizi wa Mahakama ya Rufani (T), Mhe. Emmanuel Mrangu na wa kwanza kulia ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ambaye pia ni Msaidizi Binafsi wa Jaji Mkuu, Mhe. Venance Mlingi.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju (wa pili kulia) akipokea taarifa kutoka kwa Mkuu wa Gereza la Isanga leo tarehe 10 Julai, 2025 alipotembelea gereza hilo.


Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju (katikati) akiwa katika picha za pamoja na Maofisa wa Mahakama na Magereza na wadau wengine wa Haki Jinai. Wa pili kushoto ni Kamishna Jenerali wa Magereza Tanzania, Jeremiah Yoram Katungu, wa pili kulia ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, wa kwanza kulia ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo na wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Bw. Sylvester Mwakitalu.


Kamishna Jenerali wa Magereza Tanzania, Jeremiah Yoram Katungu (kushoto) akikabidhi zawadi ya begi kwa Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju baada ya kukamilisha ziara ya ukaguzi aliyofanya katika Gereza la Isanga lililopo jijini Dodoma.

Kamishna Jenerali wa Magereza Tanzania, Jeremiah Yoram Katungu (kushoto) akimkabidhi zawadi Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani (kulia). Anayeshuhudia katikati ni Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju na wa kwanza kulia ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo (kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Kamishna Jenerali wa Magereza Tanzania, Jeremiah Yoram Katungu. (Picha na MARY GWERA na ARAPHA RUSHEKE, Mahakama - Dodoma)
Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju-juu na chini-akizungumza kwenye sherehe ya kuwapokea na kuwakubali Mawakili wa Kujitegemea wapya 449 leo tarehe 3 Julai, 2025 jijini Dodoma.

Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Kiaki Nkya akitoa utambulisho wa wageni mbalimbali.

Na Faustine Kapama na Arapha Rusheke, Dodoma.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju amewahimiza Mawakili wapya kuzingatia maadili, uadilifu na weledi na kuishi viapo vyao wanapotekeleza majukumu yao katika muktadha mzima wa utoaji haki kwa Wananchi.

Mhe. Masaju, ambaye ni Jaji Mkuu wa tisa wa Tanzania na Jaji Mkuu wa saba Mtanzania, ametoa wito huo leo tarehe 3 Julai, 2025 baada ya kuwapokea na kuwakubali waombaji 449 kuwa Mawakili wa Kujitegemea.

Hili ni tukio lake la kwanza tangu alipoapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu tarehe 15 Juni, 2025, kuwa Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania.

Katika hotuba yake kwenye sherehe hiyo ya uapisho iliyofanyika katika ukumbi wa Jiji Mtumba Jijini Dodoma, Jaji Mkuu Masaju amewakumbusha Mawakili kuwa taaluma ya sheria ni wito wa kuhudumia wananchi kwa haki na sio njia ya kujinufaisha binafsi.

“Mnaingia kwenye taaluma nyeti inayogusa maisha ya watu. Haki ya mwananchi inaweza kupatikana au kupotea kupitia maneno yenu. Kuweni waadilifu, wenye maadili, na waaminifu kwa wito wenu,” amesema Mhe. Masaju kwa msisitizo.

Ameongeza kuwa Mawakili wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kutetea haki za wanyonge, kulinda Katiba na kushiriki kikamilifu katika mageuzi ya kimahakama yanayoendelea nchini.

Hafla hiyo imehudhuriwa na Viongozi wa Mahakama, wakiwemo Majaji wa Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu ya Tanzania. Alikuwepo pia Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Wakili Mkuu wa Serikali.

Wengine ni Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini, mwakilishi wa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), familia za Mawakili wapya na Wadau mbalimbali wa sekta ya sheria.

Uapisho huo unaashiria mwanzo mpya kwa Mawakili hao katika kujenga jamii yenye haki, usawa na utawala bora wa sheria.
Sehemu ya Mawakili wapya-juu na chini-wakifuatilia kilichokuwa kinajiri wakati wa sherehe hiyo.
Sehemu ya Mawakili wapya-juu na chini-wakifuatilia kilichokuwa kinajiri wakati wa sherehe hiyo.

Viongozi mbalimbali, wakiwemo Majaji Wastaafu wakiwa kwenye sherehe hiyo. Picha chini ni wageni mbalimbali wakifuatilia kilichokuwa kinajiri.

Meza Kuu inayoongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju.
Majaji wa Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu ya Tanzania-juu na chini-wakiwa kwenye sherehe hizo.
Viongozi Waandamizi wa Mahakama ya Tanzania wakifuatilia kilichokuwa kinajiri wakati wa sherehe hiyo. Kushoto ni Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Chiganga Tengwa na kulia ni Naibu Msajili Mwandamizi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Sundi Fimbo.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemruhusu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, kujitetea mwenyewe katika kesi ya uhaini inayomkabili, baada ya yeye kuwasilisha ombi hilo mahakamani.

Ruhusa hiyo imetolewa leo Juni 16, 2025 na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Franco Kiswaga baada ya Lissu kueleza kuwa haki yake ya kuonana na mawakili wake kwa faragha akiwa mahabusu imekuwa ikikiukwa kwa siku 68 tangu apelekwe gerezani.

Katika maelezo yake, Lissu amesema licha ya kuwa na jopo la zaidi ya mawakili 30 aliowachagua mwenyewe kwa kuamini uwezo wao wa kisheria, hajawahi kupewa fursa ya kuonana nao ana kwa ana ili kujadili utetezi wake. 

Anadai mazungumzo yao yote yamekuwa yakifanyika kwa kutumia simu kupitia kioo kilichowekwa gerezani, pasipo uwezekano wa kubadilishana nyaraka au kuandika chochote, jambo analodai linakiuka haki zake za msingi.

"Hakuna sehemu ya kukaa, hakuna meza, hakuna kiti. Tunazungumza tukiwa tumesimama na kwa njia ya simu, mbele ya maaskari na wengine. Hii sio faragha," anadai Lissu.

Lissu anabainisha kuwa zaidi ya mara moja, Mkuu wa Gereza anakataa kumruhusu kuonana na mawakili wake kwa faragha, licha ya kuwa ni haki yake ya kikatiba na kwa mujibu wa Kanuni za Usimamizi wa Magereza pamoja na 'Mandela Rules' (Kanuni za Kimataifa za Haki za Wafungwa).

Aidha, anadai kuwa mawakili wake walijitahidi sana kutafuta haki hiyo bila mafanikio, hadi kufikia hatua ya yeye kuamua kujitetea mwenyewe ili wasije kulaumiwa baadaye endapo kutatokea dosari yoyote katika kesi hiyo.

"Hii ni kesi yangu, na kwa kuwa adhabu ya uhaini ni kifo kwa kunyongwa, sitaki mawakili wangu waje kulaumiwa. Kuanzia leo, nitajitetea mwenyewe," alidai

Lissu pia alilalamikia kukiukwa kwa haki yake ya kuabudu akiwa gerezani, akidai kunyimwa ruhusa ya kushiriki ibada za Kikristo tangu alipohamishiwa Gereza la Ukonga, hata katika sikukuu muhimu kama Ijumaa Kuu na Pasaka. Alidai hali hiyo inakiuka haki za binadamu na kanuni za magereza, zinazotambua haki ya mfungwa kuabudu.

Mbali na hilo, Lissu alifichua kuwa amekuwa akishikiliwa katika sehemu ya gereza inayohifadhi wafungwa waliokwishahukumiwa kunyongwa, licha ya kwamba yeye bado hajahukumiwa. Anadai anafuatiliwa na askari wawili kila anapotoka kwenda kuonana na mawakili au wageni, kama ilivyo kwa wafungwa waliokwishahukumiwa adhabu ya kifo.

"Naishi kwenye eneo la kusubiri kunyongwa, ninatembea katikati ya mifereji ya maji machafu. Hii ni hatari kwa afya yangu na usalama wangu," alidai.

Akijibu hoja hizo, Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga, alidai Mahakama ilishatoa uamuzi kuhusu ombi la Lissu la kujitetea mwenyewe, na kwamba upande wa Jamhuri haukuwa na pingamizi. Aliongeza kuwa baadhi ya malalamiko yaliyotolewa yanahusu uongozi wa gereza na hayapaswi kujadiliwa mahakamani pasipo kufuata taratibu rasmi za kisheria, kama vile kuwasilisha maombi maalum ya mandamus.

Katika hatua nyingine ya kesi hiyo, Katuga alidai kuwa jalada la kesi bado lipo ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) kwa ajili ya kulipitia na kutoa maelekezo ya kama kesi hiyo itahamishiwa Mahakama Kuu au la.

Kesi hiyo imepangwa kutajwa tena Julai Mosi 2025.
Na Happiness Katabazi.

RAIS Samia Suluhu Hassan Leo amemteua Jaji wa Mahakama ya Rufani George Mcheche Masaju Kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania.

Kwa Mujibu wa taarifa kwa umma iliyosainiwa na Katibu Mkuu Kiongozi Leo Juni 13 imesema ...

Hongera sana mtani na rafiki yangu Masaju kuteuliwa kuwa Jaji Mkuu .

Januari 10 mwaka 2025 , Rais Samia alimteua Jaji Masaju kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.

Aprili 21 mwaka 2023 , Rais Samia aliteua Jaji Masaju kuwa Mshauri wake wa masuala ya Sheria ( Advisor to the President - Legal Affairs) Na wakati akimteua kushika nafasi hiyo Jaji Masaju alikuwa ni Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma.

Novemba 5 mwaka 2015 , Masaju aliteuliwa mara ya pili kushika wadhifa wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Rais wa awamu ya Tano Marehemu Dr. John Magufuli ndiye akimteua Masaju kuwa AG .

Mara ya kwanza ilikuwa ni serikali ya awamu ya nne Januari 2 Mwaka 2015, Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambaye amestaafu wadhifa wa Cheo cha Rais , alimteua Masaju Kuwa Mwanasheria Mkuu wa serikali ikiwa ni siku chake aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema ambaye kwasasa ni marehemu kujihudhuru wadhifa huo.

February mosi mwaka 2018 Rais Magufuli alimteua Masaju kuwa Jaji wa Mahakama Kuu nchini.

Masaju ni miongoni mwa Wanasheria wa serikali wazalendo na wanaowaaminiwa kiutendaji na ndiyo maana zilipokuwa zikifunguliwa Kesi ambazo zilikuwa zikivuta hisia za watu Wengi Masaju alikuwa akivaa suti na gauni lake la uwakili na kutinga Mahakama ya Rufaa, Mahakama Kuu na kuiendesha Kesi hiyo yeye Mwenyewe akisaidiwana na vijana wake.

Na nilipokuwa Mwandishi wa Habari za mahakamani,nilipokuwa nikimuona Masaju Kubeba gauni jeusi na begi lilokuwa na Nyaraka za kuendeshea Kesi basi nilikuwa Nasema Kimolo moyo Kuwa upande wa wa pili Katika Kesi hiyo ujiandae kikamilifu .

Ushahidi mchache wa haya ninayoyasema kuhusu Masaju ambayo nilikushuhudia kwa macho yangu mwanzo hadi Mwisho ni Rufaa ya Kesi maarufu ya mgombea Binafsi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya Mchungaji Christopher Mtikila Katika Mahakama ya Rufaa nchini Masaju alikuwa kiongozi wa Mawakili wa serikali kuendesha Kesi hiyo ya kihistoria ambayo ikisikilzwa na jopo la Majaji Saba waliokuwa wakiongozwa na Jaji Mkuu wa wakati huo , Agustino Ramadhani, Masaju alifanikiwa Kujenga hoja na hatimaye jopo lilikubaliana naye na kutengua hukumu ya Mahakama Kuu ambayo iliruhurusu Mgombea Binafsi.

Ushahidi wa pili, ni Mwaka 2014, katika kesi ya Kikatiba Na.24/2013 , Masaju aliwakilisha upande wa Mwanasheria Mkuu Katika Kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa na Kituo ca Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) pamoja na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS)dhidi ya Waziri Mkuu iliyokuwa ukiomba Mahakama Kuu itoe Tafsiri ya Ibara ya 100 Kuwa wabunge wana Uhuru bila mipaka kwani Pinda alitoa Kauli Bunge akitaka Polisi iwapige wanaovunja Sheria za nchi.

Juni 6 Mwaka 2014 , Jopo la Majaji wa Tatu wa Mahakama Kuu Dar es Salaam, Fakji Jundu, Dk.Fauz Twaibu na Augustine Mwarija walitoa uamuzi wa Kuitupa Kesi hiyo kwa sababu Imeona walalamikaji walikuwa hawana Haki ya kisheria ya kushitaki Pinda.

Jopo hilo lilitoa uamuzi huo ambapo jaji Jaji Jundu alisema anakubaliana na pingamizi la awali lilowasilishwa na wakili wa mdaiwa (Pinda), Ambaye ni Naibu Mwanasheri Mkuu wa Serikali, George Masaju, ambalo lilikuwa likiomba Mahakama itoe amri ya kuifuta Kesi hiyo kwasababu walalamikaji hawana Haki a kisheria ya kuwashitaki wadaiwa na kwamba Waliokuwa na Haki ya kushitaki Pinda ni wananchi na siyo Taasisi hizo za walalamikaji.

LHRC na TLS walimshtakiwa Waziri Mkuu Pinda pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kauli aliyoitoa bungeni Juni 20 mwaka 2013.Ilidaiwa Katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo Waziri Pinda akijibu alisema, ‘ukifanya fujo…unaambiwa usifanye hiki ukaamua kukaidi, utapigwa tu, muwapige tu sababu tumechoka’.

Jaji Jundu alisema, Masaju Aliwasilisha pingamizi la awali akiomba kesi hiyo itupwe kwa sababu mahakama hiyo haina uwezo wa kuisikiliza, waliofungua hawakustahili kuifungua na iko kwa ajili ya kupoteza MUDa wa Mahakama.

Katika uamuzi huo, majaji walikubaliana na hoja tatu za pingamizi kuwa walalamikaji katika kesi hiyo hawakuwa na haki ya kufungua kesi hiyo na kwamba walikosea taratibu za ufunguaji wa kesi kama hizo kwa kuwa walikiuka amri na kanuni zinazoongoza Mashauri ya Madai (CPC).

Katika hoja ya kwanza kuwa Pinda kama mbunge analindwa na Katiba, jopo hilo lilisema kuwa ni kweli wabunge wanalindwa na Katiba Ibara ya 100 (1) kuhusu haki na upendeleo (Previledge), yaani haki na uhuru wa mjadala na maoni. Hata hivyo, lilikataa hoja za utetezi kuwa wabunge wana kinga isiyo na mipaka ya kutokushtakiwa kwa kauli au jambo lolote walilolitamka bungeni.

“Ibara ya 100(1) ya Katiba haiwezi kujadiliwa mahali popote ikiwemo mahakamani, ibara hiyo inasema kwamba, kutakuwa na uhuru wa mawazo, majadiliano na utaratibu katika Bunge na uhuru huo hautavunjwa wala kuhojiwa na chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano au katika mahakama au mahali penginepo nje ya Bunge.

“Ibara ya 100(2) inaweza kujadiliwa mahakamani, inasema kwamba bila kuathiri katiba hii au masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika, Mbunge yoyote hatashtakiwa au kufunguliwa shauri la madai mahakamani kutokana na jambo lolote alilolisema au kulifanya ndani ya Bunge au alilolileta bungeni kwa njia ya maombi, muswada, hoja au vinginevyo.

“Mwananchi mmoja mmoja aliyeathirika na jambo lililozungumzwa na mbunge bungeni anaweza kushtaki lakini si taasisi kama ilivyo katika kesi hii,”alisema.

Alisema kutokana na sababu hizo, mahakama inatupilia mbali kesi hiyo kwa sababu waliofungua kesi, LHRC na TLS hawakustahili kisheria kufungua kesi hiyo kwa sababu hawakuathirika.

Kesi ya Tatu ni Kesi iliyovuta hisia za watu Wengi ni Kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa Mwaka 2014 na Mwandishi wa Habari Saed Kubenea dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.

Kubenea alikuwa anaomba Mahakama hiyo itoe amri ya muda ya Kuzuia Bunge Maalum la Katiba lisiendelee na kazi kwasababu linavunja Sheria.

Hata hivyo Masaju aliwasilisha mapingamizi mawili ambayo yaliomba Mahakama hiyo itupilie Mbali Maombi ya Kubenea Kwani hayana Msingi na Mahakama hiyo ilitupilia mbali Maombi ya Kubenea na Bunge linaendelea na kazi zake.

Mifano ni mingi ya Kuonyesha Masaju Kabla ya kuteuliwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Januari 2 na Novemba 5 Mwaka 2015 , kuna kazi nzuri ya kuiwakilisha upande wa serikali Katika Kesi mbalimbali mahakamani aliifanya hivyo anastahili.

Ni neema ya Mungu na na rekodi yake ya Utendaji Kazi ndiyo imesabisha Marais wa wawili ya marehemu Dk.John Magufuli na rais wa Sasa Samia Suluhu Hassan wakuteue kushika nyadhifa hizo ikiwemo hii ya Jaji Mkuu ambayo umeteuliwa Leo Juni 13 mwaka huo ili amsaidie kuchapa kazi.

Wosia wangu wa Masaju endelea na msimamo wako ule ule wa kusimamia haki na Kusema ukweli bila woga.

Masaju ambaye kabla ya kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa serikali na aliwahi kuwa mshauri wa Rais Kikwete katika masuala ya sheria ni mtu asiye penda kuburuzwa na mambumbumbu wa Sheria, ni mtu anayejali utu,heshima na Kupenda watu watii Sheria za nchi na ni mzalendo kwa taifa lake.

Hongera Mtani wangu Masaju, Mungu akuongoze katika nafasi hii ya Jaji Mkuu wa Tanzania.

0716 774494
6/13/2025

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu
jijini Dar es Salaam imemuhukumu kifungo cha miaka miwili jela au fauni ya Sh.1,000,000 Ofisa Habari na Mawasiliano wa Timu ya Mpira wa Miguu ya ‘KENGOLD Sports Club’ Joseph Mkoko kwa kosa la kuomba na kupokea rushwa ya Sh.1,500,000.

Makosa hayo ni kinyume na kifungu cha 15(1)(a) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura ya 329 Marejeo ya mwaka 2024.

Awali ilidaiwa kuwa Ofisa huyo alipokea rushwa kutoka kwa mchezaji mmoja wa zamani wa timu ya mpira wa miguu ya Vital’o ya Burundi, ili amsaidie kusajiliwa na ‘KENGOLD Sports Club’ na kupata upendeleo wa kupangwa kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo.

Mshtakiwa alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa mara ya kwanza mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Dk. Beda Nyaki Mei 30, 2025 na kufunguliwa Shauri la Jinai namba 13138/2025 huku upande wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) ikisimamiwa na Mwendesha Mashtaka Imani Nitume.

Aliposomewa mashtaka yake, mshtakiwa alikubali na kesi iliahirishwa hadi leo Juni 11, 2025 kwa ajili ya kusoma maelezo ya awali ya kosa.

Leo, mshtakiwa alikumbushwa makosa yake na kuendelea kukubali na aliposomewa maelezo ya awali ya kosa pia alikubali, hivyo mahakama imemtia hatiani.
Wakili Peter Njau akiongea na vyombo vya habari.

Na Vero Ignatus, Arusha.

Mahakama kuu kanda ya Arusha imesimamisha utekelezaji wa Amri iliyokuwa imetolewa na serikali kupitia tangazo LA serikali namba 673 ya mwaka 2024 la kufuta vijiji na kata na vitongoji katika wilaya ya Ngorongoro.

Uamuzi huo umetolewa na Jaji Ayubu Mwenda Augusti 22,2024 ambapo alisikiliza maombi madogo ya zuio yaliyowasilishwa na ndugu Isaya Ole posi mwananchi wa ngorongoro kwa kupitia Wakili wake Peter Njau

Baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili, Jaji Mwenda aliridhia maombi hayo madogo na kukubali zuio la kusimamisha tamko hilo kupisha usikilizaji wa maombi ya msingi ,hadi amri ya Mahakama itakavyoelekeza na vinginevyo.

Kwa upande wake Wakili wa kujitegemea Peter Njau alisema awaki kwa wananchi wa ngorongoro kuliweza kitokea taharuki kutokana na tangazo lililokuwa umetolewa na serikali kupitia mamlaka ya mji mdogo wa ngorongoro la kuwataka wakazi wake kuhama, ila baada kusikikizwa kwa pande zote mbili Jaji aliweza outta Amri ya kuzuia

"Mteja wangu aliweza kuniomba kumuwakilisha katika shauri kuweza kuomba Mahakama itazame uhalali wa Amri ole ni kuweza kuleta shauri lile mahakamani na kulisajili maombi madogo na yalisikilizwa kwa pande zote mbili na aliweza kutoa Amri ya kuzuia" Alisema Wakili Peter Njau"
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Morogoro Mhe. Latifa Mansoor akifungua kikao kazi maalum kwa ajili ya kupokea maoni na mapendekezo ya kuanzishwa kwa Mfumo wa kuratibu Ajira, Maadili na Nidhamu wa Tume ya Utumishi wa Mahakama leo tarehe 6 Agosti, 2024 mjini Morogoro.
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Mahakama ambaye pia ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzaniua Prof. Elisante Ole Gabriel akizungumza wakati wa Kikao Kazi Maalum kwa ajili ya kupokea maoni na mapendekezo ya kuanzishwa kwa Mfumo wa kuratibu Ajira, Maadili na Nidhamu wa Tume leo tarehe 6 Agosti, 2024 mjini Morogoro.
Sehemu ya Viongozi wa Tume, Mahakama pamoja na Wadau wakiwa kwenye kikao kazi maalum kwa ajili ya kupokea maoni na mapendekezo ya kuanzishwa kwa Mfumo wa kuratibu Ajira, Maadili na Nidhamu wa Tume ya Utumishi wa Mahakama leo tarehe 6 Agosti, 2024 mjini Morogoro. Kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar Mmuya.
Sehemu ya Watumishi wa Tume, Mahakama pamoja na Wadau wakiwa kwenye kikao kazi hicho. Wa pili Kulia ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Kongwa Bi. Souz Ngate.
Sehemu ya Viongozi wa Mahakama na Wadau wakiwa kwenye kikao kazi hicho. Katikati ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimawatu wa Mahakama ya Tanzania Bi. Beatrice Patrick
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Morogoro Mhe. Latifa Mansoor (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Tume, Mahakama pamoja na wadau mara baada ya kufungua kikao kazi maalum kwa ajili ya kupokea maoni na mapendekezo ya kuanzishwa kwa Mfumo wa kuratibu Ajira, Maadili na Nidhamu wa Tume ya Utumishi wa Mahakama leo tarehe 6 Agosti, 2024 mjini Morogoro.

Na Lydia Churi na Evelyne Odemba- Morogoro.

Tume ya Utumishi wa Mahakama inakusudia kuanzisha mfumo wa kielekitroniki utakaoratibu masuala ya Ajira, Maadili na nidhamu kwa watumishi wa Mahakama.

Katika mchakato wa kuanzishwa kwa Mfumo huo, leo Agosti 6, 2024 Tume imekutana na wadau wake muhimu katika kikao kazi kilichoanza mjini Morogoro kwa lengo la kupokea maoni na mapendekezo kwa lengo la kuanzisha mfumo huo utakaorahisisha utendaji kazi na kuleta uwazi zaidi.

Akifungua rasmi kikao kazi hicho, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Morogoro Mhe. Latifa Mansoor alisema kuanzishwa kwa mfumo wa Kielekitroniki wa Ajira, Maadili na nidhamu ndani ya Tume ya Utumishi wa Mahakama ni muendelezo wa safari mageuzi ya mfumo ya Mahakama ya Tanzania ili kuboresha shughuli za utoaji haki nchini.

”Katika dunia ya sasa teknolojia inakua kwa kasi na shughuli nyingi za Serikali inafanywa kwa mfumo huo, kwa kutambua hili, Tume imeona ni vema kuwa na mfumo wa kielekitroniki utakaoratibu masuala ya Ajira, Maadili na Nidhamu kwa watumishi wa Mahakama”, alisema.

Aidha, Jaji Mansoor alitoa rai kwa wadau kutoa michango ya mawazo itakayozaa matunda yatakayowezesha kujengwa kwa mfumo bora zaidi wa ajira ambao utafungamanishwa na mfumo wa kielekitroniki wa uendeshajiwa Kamati za maadili ambazo Wenyeviti wake ni wakuu wa Mikoa na wakuu wa Wilaya.

Awali akitoia neno la utangulizi, Katibu wa Tume ya Utumishi wa Mahakama ambaye pia ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel alisema kuwa lengo la kikao hicho ni kupata maoni ya wadau kuhusu uanzishwaji wa mfumo ambao utaleta mabadiliko ya Utendaji kazi wa Tume.

“Nia yetu ni kuona kwamba Tume ya Utumishi wa Mahakama ya Tanzania inaenda kuwa kitovu cha mageuzi ndani ya Afrika na duniani kote katika matumizi ya TEHAMA”, alisema.

Alitaja baadhi ya mada zilizowasilishwa katika kikao kazi hicho kuwa ni pamoja na rasimu ya mafunzo kuhusu mfumo huo, rasimu ya masuala ya ajira, kushirikishana uzoefu wa masuala ya TEHAMA na kujadiliana namna ya kuboresha mfumo huo ulioanza kujengwa.

Alisema kuwa ujio wa mfumo huo utasaidia katika kusimamia rasilimali watu, ajira, maadili na nidhamu na utakuwa na manufaa kwa Tume ya Utumishi wa Mahakama na watanzania kwa ujumla.

Naye Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Bw. Jocktan Bikombo alisema kuwa Tume imedhamiria kuanzisha kuanzisha Mfumo ambao utasaidia kupanua wigo wa kiutendaji kazi wake.

Tume ya Utumishi wa Mahakama ni chombo cha kikatiba kilichopewa jukumu la kusimamia uendeshaji wa Mahakama ya Tanzania. Moja ya jukumu lake ni kusimamia Maadili ya Maafisa Mahakama ili kuhakikisha Mhimili wa Mahakama unatekeleza jukumu lake la msingi na la kikatiba la kutoa haki kwa wananchi.

Waziri wa Katiba na Sheria, Mh Dkt.Damas Ndumbaro (Mb) akipokea machqpisho mbalimbali kutoka kwa Afisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Rehema Nyagawa wakati alipotembelea banda la Tume Leo Januari 26,2023 katika maonesho ya wiki ya sheria kitaifa inayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mh Dkt.Damas Ndumbaro (Mb) akipokea machqpisho mbalimbali kutoka kwa Afisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, akipatiwa eklimu ya mpiga kura wakati alipotembelea banda la Tume Leo Januari 26,2023 katika maonesho ya wiki ya sheria kitaifa inayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma
Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Prof. Elisante Ole Gabriel akizungumza jambo leo Januari 23,2023 wakati alipotembelea banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika maonesho ya wiki ya sheria kitaifa inayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma.
Jaji Mfawadhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Baraza la Ushindani Mhe. Salma Mussa Maghimbi tarehe 27 January, 2023 ametembelea Banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwenye Maonesho ya Wiki ya Sheria yanayoendelea kwenye viwanja vya Nyerere Square jijini Dodom.
Jaji Mfawadhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Baraza la Ushindani Mhe. Salma Mussa Maghimbi tarehe 27 January, 2023 ametembelea Banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwenye Maonesho ya Wiki ya Sheria yanayoendelea kwenye viwanja vya Nyerere Square jijini Dodom.
Jaji Mfawadhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Baraza la Ushindani Mhe. Salma Mussa Maghimbi akipatiwa machapisho mbalimbali ya Tume.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mh.Rosemary Staki Senyamule akipokea machapisho mbalimbali ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutoka kwa Afisa Mwandamizi wa Tume, Titus Mwanzalila (kushoto) wakati kiongozi huyo alipotembelea Banda la Tume, Januari 26,2023 katika maonesho ya Wiki ya Sheria yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Sylvester Anthony Mwakitalu ametembelea banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi na kupatiwa Elimu ya Mpiga Kura katika Maonesho ya Wiki ya Sheria Januari 25,2023. Maonesho ya Wiki ya Sheria yanaendelea katika viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Sylvester Anthony Mwakitalu ametembelea banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi na kupatiwa Elimu ya Mpiga Kura katika Maonesho ya Wiki ya Sheria, Januari 25,2023. Maonesho ya Wiki ya Sheria yanaendelea katika viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma.
Askofu Mkuu wa Kanisa la Viziwi Tanzania Makao Makuu Dodoma Mchungaji Frank Sarungi tarehe 27 Januari 2023, ametembelea Banda la Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwenye Maonesho ya Wiki ya Sheria yanayoendelea katika Viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.
Afisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bi. Rehema Nyagawa akizungumza Katibu wa Wanawake Chama cha Viziwi Tanzania Mkoa wa Dodoma Bi Amina Issah wakati alipotembelea banda la Tume kwenye maonesho ya Wiki ya Sheria Tanzania yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.
Watu wenye ulemavu wafurahishwa na kuwepo kwa wakalimani wa lugha ya alama inayotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwenye Banda la maonesho la Tume katika maoneolsho ya Wiki ya Sheria yanayoendelea viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpigakura, Bi. Giviness Aswile alipotembelea banda la Tume
Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Emmanuel Kawishe akizungumza na wadau alipotembelea banda la Tume
Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Leonard Tumua akiwa katika banda la Tume
Mkaguzi Mkuu wa ndani wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Amos Akim aakiwa katika Banda lka Tume.