Na Mwandishi Wetu.

Alizaliwa mwaka 1960 katika kijiji kidogo cha Namoto, wilayani Ruangwa, mkoani Lindi. Leo hii, jina la Kassim Majaliwa Majaliwa linaandikwa kwa heshima kubwa katika historia ya Tanzania. Safari yake ni ya kuvutia kutoka maisha ya kawaida kabisa hadi kuwa mmoja wa viongozi wa juu kabisa wa taifa.
‎Kiu yake kubwa ilikuwa ni kufundisha, hivyo hakuchelewa alisomea ualimu katika Chuo cha Ualimu Mtwara na baadaye Chuo cha Ualimu Kitangali kilichopo Mtwara.
‎Alianza kuwa mwalimu, akilea vijana kwa bidii na maadili, Akawa mkufunzi katika Chuo cha Ualimu mtwara huku akijijengea misingi imara kwa huduma ya jamii,
‎Hakika alijitengeneza kama kiongozi mwenye maarifa, nidhamu, na mwelekeo wa maendeleo kwa taifa.
Kiu yake ya kujifunza iliendelea hadi alipopata shahada kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (Open University of Tanzania).
‎Majaliwa aliyeanzia ualimu, ukufunzi wa chuo cha ualimu, ukatibu wa chama cha walimu, Ukuu wa wilaya ya Rufiji, Unaibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu tawala za mikoa na Serikali za motaa TAMISEMI yana hatimaye Waziri Mkuu wa –
‎ leo ameandika historia isiyo futika katika taifa letu.
‎CHAMA CHA WALIMU MKOA WA SINGIDA CWT wanamkumbuka zaidi hasa kipindi ambacho alianzisha, kusimamia na kukamilisha ujenzi wa jengo la ghorofa la ofisi za chama cha walimu mkoani Singida alipokuwa akihudumu kama Katibu wa CWT mkoani Singida.
‎Majaliwa amechagua historia imjadili katika maisha yake yote.
Rais mstaafu Jakaya Kikwete aliiona nyota ya Majaliwa kutokea Singida, akamteua kuwa Mkuu wa Wilaya ya Urambo alipowekwa kiti moto na wabunge wawili wababe wa wilaya hiyo – marehemu Samuel Sitta na Juma Kapuya waliokuwa wabunge wa Jimbo la Urambo na Kaliua.
‎Hamad, Majaliwa akahamishiwa wilaya ya Rufiji alipohudumu hadi mwaka 2010 ndipo alipoamua kujitosa jimboni Ruangwa kugombea ubunge wa jimbo hilo.
‎Hakika nyota njema iliyoanzia ualimu haikazimika baada ya uchaguzi huo ambapo siku anawaaga watumishi wa wilaya ya Rufiji alikohudumu kama mkuu wa wilaya baada ya kushinda ubunge.
‎Katikati ya maandalizi ya kuelekea jimboni, analisikia jina lake akiwa miongoni mwa manaibu mawaziri wa serikali ya Jakaya Mrisho Kikwete.
‎Mwaka 2010, alichaguliwa kuwa Mbunge wa Ruangwa, kutokana ile kasi yake ya utendaji, jicho la hayati John Pombe Joseph Magufuli lilimuona Novemba 2015 na kumteua kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania.
‎Mtu mwema aliyewahi kutokea katika ardhi ya nchi yetu.
Leo hii tunamzungumzia Kasim Majaliwa
‎Kiongozi imara ambaye ameziishi Enzi na kuziheshimu nyakati zake
‎Kwa ridhaa yake mwenyewe Ameamua kuuwaga Waziri Mkuu baada ya kutangaza kutogombea ubunge wa Ruangwa.
‎Vyovyote iwavyo, vyovyote itakavyotafsiriwa, na vyovyote itakavyoonekana – lakini ukweli usemwe, Majaliwa ameandika historia yake. Sio rahisi kwa kiongozi wa ngazi yake kuamua kung’atuka na kuachia madaraka makubwa kama Uwaziri Mkuu.
‎Watangulizi wake kadhaa iliwabidi wastaafu siasa baada ya kushindwa kupata uteuzi wa nafasi ya juu baada ya kuhudumu kama Waziri Mkuu. Naam, tulimuona hayati Msuya akishindwa urais na hayati Mkapa ndipo akastaafu rasmi siasa mwaka 1995. Ilimchukua hadi kushindwa urais na Jakaya Kikwete mwaka 2005 ndipo akaamua kuistaafu rasmi siasa na kuitwa Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye. Sio hao tu, hata Mizengo Pinda ilimbidi ashindwe kwanza kura za maoni za urais mwaka 2015 na kuteuliwa Magufuli ndipo akatangaza kustaafu siasa.
‎Tofauti kabisa na Majaliwa Kassim Majaliwa aliyetangaza kutogombea tena ubunge wa Ruangwa. Ifahamike kuwa kutokugombea ubunge ni sawa na kusema ameamua kustaafu Uwaziri Mkuu, kwa sababu hauwezi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kama hautokani na ubunge wa kuchaguliwa jimboni. Hii ndiyo kusema kuwa Majaliwa amestaafu rasmi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania.

Amestaafu akiwa bado ana nguvu, ana nishati na uwezo wa kuendelea kuwa mtumishi mwandamizi wa serikali. Waziri Mkuu mwenye historia ya utumishi uliojaa uadilifu na kujitolea. Ni kiongozi wa kipekee anayestaafu mapema kuliko waliomtangulia, lakini akiacha alama ya kudumu. Kassim Majaliwa ni kielelezo cha uongozi wa kweli – unaotanguliza maadili, unyenyekevu, na maslahi ya taifa kuliko jina binafsi.
‎Tanzania itamkumbuka daima kama mtumishi mwadilifu, ambaye alitumikia taifa kwa moyo wote – kwa utulivu, busara, na heshima ya juu. Hongera sana Majaliwa, tumeuona na kuuonja utamu wa utumishi wako kama Waziri Mkuu wa nchi hii.
Hakika wewe ni shujaa unayestahili kukumbukwa, ni mwamba unayehitaji kuegemewa.
‎Unaanza maisha mapya ya ustaafu ukiwa na nguvu na maarifa mapana kiasi cha kuwa mshauri bora kwa wa watakaoendelea madarakani.
‎Itoshe kusema umafanya kila ulichotakiwa kufanya katika nchi, Taifa limafaidika katika kila idara ulipokwepo
‎Sasa ni muda wa wajukuu kufurahia wema wa Babu Kasim Majaliwa
‎Kila la heri, Fahari ya Kusini.
‎Kila la heri, Mpiganaji.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: