

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kimeutaarifu umma wa Watanzania na kuwaalika wadau wa elimu na maendeleo, kwa ujumla kushiriki katika Maadhimisho ya kumi ya Wiki ya Utafiti na Ubunifu ya UDSM yatakayofanyika kuanzia Juni 9- 11, 2025 katika Viwanja ya Maktaba ya Chuo.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa Chuo-Utafiti, Prof. Nelson Boniface (Pichani) amesema kuwa Maonesho hayo yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 11, 2025 na mazungumzo ya mashirikiano ya kimkakati, kongamano, maonesho na mawasilisho ya watafiti na wabunifu likiwa ni jukwaa la washiriki kupata fursa ya kubadilishana maarifa na ushirikiano.
Aidha, Prof. Boniface amesema kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni: "Kutumia teknolojia ya Dijitali ili kukuza utafiti, ubunifu na ubiasharishaji,".
Ameongeza kuwa miradi mingi itakayooneshwa ni ile ya wanafunzi na Wanataaluma huku akitanabaisha kuwa mtoa Mada Mkuu ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Mhandisi Peter Ulanga na Profesa Lilian Kaale Mkurugenzi katika masuala ya Ubunifu UDSM.
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kinatumia fursa hiyo kujipambanua kwa jamii kwa kuonesha shughuli zake za utafiti, ubunifu, huduma kwa umma na ubadilishanaji maarifa kwa kuunga mkono Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Na Mwandishi Wetu, WHMTH, Arusha.
Waratibu wa Anwani za Makazi Taifa kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari pamoja na wa Wilaya walipokutana na Mtendaji wa Kata ya Enguserosambu, Kijiji cha Engurosambu na Mtaa wa Engurosambu Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro, Arusha tarehe 26 Agosti 2024, ili kukagua maendeleo ya zoezi la Uhakiki wa Anwani za Makazi, Usasishaji na usajili wa taarifa za Anwani za Makazi tangu lililopozinduliwa siku ya tarehe 14 Agosti, 2024 katika Mkoa wa Arusha.Kata hiyo ni miongoni mwa Kata mbili za Ngorongoro zilizo mpakani mwa Kenya na Tanzania zenye changamoto ya eneo kubwa na mwingiliano wa wananchi wa nchi jirani ya Kenya pamoja na mawasiliano duni ya mtandao wa simu na intaneti.
Mwanzilishi wa maktaba ya kijamii wilayani Mwanga, Jennifer Dickson akifurahia tuzo ya Malkia wa Nguvu ajaye katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji) Dk. Kitila Mkumbo (kulia) akimpongeza mshindi wa tuzo la Malkia wa Nguvu ajaye,Jennifer Dickson katika hafla ya kutunuku tuzo hizo iliyofanyika jijini Dar es Salaam,katikati ni mwenyekiti wa bodi ya maktaba ya kijamii ya Mwanga iliyoanzishwa Jennifer, Profesa Bonaventure Rutinwa, ambaye pia ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Barrick nchini, Georgia Mutagahywa, akiwa na wanafunzi wa kike waliofanya vizuri katika somo la hisabati muda mfupi baada ya kukabidhiwa zawadi za laptop kutoka Barrick.







































