Articles by "MAISHA NA MAHUSIANO"
Showing posts with label MAISHA NA MAHUSIANO. Show all posts
Kulikuwa na kijiji kimoja kilichoishi watu wema na wabaya kwa pamoja. Kijiji kilibarikiwa na mto ulioleta uhai kwa kila kiumbe. Ng’ombe walikunywa maji yale na kutoa maziwa matamu, lakini vilevile, nyoka walikunywa maji hayo hayo na kutengeneza sumu kali.
(Maji yaleyale anayokunywa ng’ombe kutengeneza maziwa, ndiyo hayo hayo anayokunywa nyoka kutengenezea sumu yake.)

Katika kijiji hicho, aliishi mzee mmoja mwenye mbwa aliyekuwa mwaminifu. Lakini siku moja, mbwa yule akaanza kumbwekea bwana wake kila alipomkaribia. Mzee akagundua kuwa jirani yake alikuwa amemzoesha kumpa mifupa kwa siri.
(Mbwa wako akianza kukubwekea, tambua kuna mtu mwingine anamlisha.)

Siku moja, mzee huyo aliona panya akimcheka paka wake shupavu. Alishangaa, lakini hakujua kuwa panya alikuwa amejificha karibu na shimo lake la kutorokea.
(Ukiona panya anamcheka paka, ujue yupo karibu na shimo.)

Baadaye, mbweha alifika nyumbani kwake kuomba msamaha baada ya kuiba vifaranga wawili. Kwa moyo wa huruma, mzee akamsamehe. Lakini haikupita muda, mbweha huyo akarudi tena — safari hii akaiba mbuzi wake mzima.
(Ukimsamehe mbwea kwa kukuchukulia vifaranga wako, kuna siku atakuibia mbuzi wako.)

Mzee alijaribu kumshawishi nyani wake wa shambani kwamba asali ni tamu kuliko ndizi, lakini nyani akacheka tu na kusema, “Hata tamu ya dunia, siwezi kuiacha ndizi yangu.”
(Huwezi kumshawishi ngedere asali ni tamu kuliko ndizi.)

Siku moja mzee alipokuwa akipita shambani, alikuta mzoga wa mbuzi wake kati ya mimea ya viazi. Wengi walidhani labda alikufa kwa njaa, lakini macho ya mzee yaliona zaidi — alijua kuwa kilichomuua kilikuwa sumu kutoka kwa nyoka aliyekunywa maji yale yale ya mtoni.
(Ukikuta mzoga wa mbuzi kwenye shamba la viazi, unapaswa kujua kilichomuua si njaa.)

Baadaye, tumbili walianza kumpigia makofi kila alipopita, wakimsifia kwa maneno matamu. Lakini ndani ya usiku ule ule, walimuangushia ndizi zake zote ardhini.
(Tumbili akikupigia makofi, ujue anakaribia kukuangushia ndizi zako.)

Mwishowe, mzee akaenda kumshauri kijana wa kijiji aliyekuwa anajulikana kwa ukaidi. Alimwambia, “Usisubiri hadi uharibifu ukufike ndipo usikie.” Lakini kijana hakusikia. Ilibidi apitie mateso ndipo ajifunze.
(Kenge huwa hasikii mpaka atokwe na damu masikioni.)

Ndipo mzee akakaa chini ya mti wa mwembe, akatazama mto ule ule, akatabasamu kwa uchungu na kusema:

“Maisha ni kama maji yale ya mtoni — yanamlisha ng’ombe na nyoka kwa pamoja. Uamuzi ni wako kama utakua wa kutoa maziwa au sumu.”
Baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025, taifa letu limepata majeraha kutokana na matendo ya baadhi ya vijana waliotumika vibaya kufanya fujo na vurugu. Wengi wamepoteza maisha, wengine wamejeruhiwa, na ndoto nyingi zimezimika — yote kwa sababu ya kuchochewa na watu wenye maslahi binafsi.

Kijana, usikubali kuwa chombo cha uharibifu.
Usikubali kutumiwa kuvunja amani kwa ahadi za muda mfupi au hisia za hasira.
Tafakari kabla ya kuchukua hatua — je, unachokifanya kinajenga au kinabomoa mustakabali wako?

Acha nia ovu, jenga nia njema.
Tumia nguvu zako kwa maendeleo, elimu, ubunifu, na kulinda amani ya nchi yako.
Kumbuka, taifa lenye amani linatoa nafasi kwa ndoto zako kukua.

🇹🇿 Tanzania inakuhitaji ukiwa imara, mwenye hekima, na mwenye upendo.
#KijanaWaAmani #UsikubaliKutumika #AmaniKwanza #TanzaniaYetu #FikraSahihi

Kuna maumivu ambayo hayawezi kuelezeka kwa maneno — maumivu ya kumpenda mtu kwa dhati, kumpigania, kumuinua, kumsamehe, kumsomesha, au hata kumuuguza… halafu siku moja unaamka na kugundua amekuacha kama hukuwahi kuwepo.
Huu ni uchungu wa kimya, ule unaolia ndani ya roho, si kwa hasira, bali kwa maswali yasiyo na majibu.

Lakini ukweli ni huu: maumivu haya hayajawekwa ili yakumalize, bali yakukamilishe.

JINSI YA KUPONA BAADA YA KUUMIZWA NA MTU ULIYEMPENDA KWA DHATI

Hapa chini ni hatua 10 za kupona kiakili, kihisia, na kiroho baada ya kuumizwa na mtu uliyetolewa roho yako kumpenda.

1. KUBALI KUUMIA — USIJIFICHE NYUMA YA NGUVU BANDIA

Usijifanye “nipo sawa” wakati moyo wako unavuja damu. Kubali kuwa umeumizwa, ukubali kwamba ulipenda kupita kiasi. Kukubali ndiyo hatua ya kwanza ya uponyaji.

Usione aibu kulia — machozi si udhaifu, ni njia ya roho kutoa sumu ya huzuni. Wacha moyo wako upate nafasi ya kuvujisha maumivu badala ya kuyabeba ndani na kuwa mzigo wa maisha.

2. USIJILAUMU KWA WEMA WAKO

Wema wako haukuwa kosa. Ulichofanya kilikuwa sahihi, ila kwa mtu asiye sahihi.

Kujitolea kwako, huruma yako, na moyo wako wa kutoa havipaswi kuwa sababu ya kujichukia. Dunia inahitaji watu kama wewe, ila safari ijayo lazima ujifunze kuweka mipaka.

Tambua: mtu aliyekuacha hakukataa wema wako, alishindwa kuuhimili.

3. TOA WAZI KWA HISIA ZAKO KWA NJIA ZENYE AFYA

Badala ya kujifungia chumbani na kulia kila siku, andika hisia zako.

Andika barua ambayo hautamtumia.

Enda baharini, mlimani, au sehemu tulivu—piga kelele, lia, toa yote.

Hiyo ni njia ya roho kujisafisha. Ukijinyima nafasi ya kutoa hisia, utajikuta unalipiza kisasi kimya, au unakuwa mtu mkavu kihisia kwa wote.

4. USIRUDISHE HESHIMA KWA MTU ALIYEITUPA

Baada ya kuumizwa, kuna jaribu la kutaka kuonyesha bado unamjali, bado uko pale. Hapana.

Ukirudisha heshima kwa mtu ambaye hakujali hisia zako, unazidisha kidonda.

Sio chuki — ni heshima binafsi. Acha roho yake iende. Usijaribu kumshawishi akuone tena. Wacha akumbuke mwenyewe alivyoondoka kwa mtu ambaye hakuwa na kosa ila moyo safi.

5. TENGA MUDA WA UKIMYA NA UPWEKE

Upweke ni tiba ya nafsi. Wengi wanakimbilia uhusiano mwingine au marafiki wapya haraka ili kusahau, lakini wanajikuta wanaumizwa tena.

Tulia. Tembea peke yako. Tafakari.

Sauti ya ndani yako haiwezi kuzungumza kwenye kelele.

Ukimya utakufundisha kitu ambacho mapenzi hayakuweza—kuwa rafiki wa nafsi yako.

6. JIFUNZE SOMO BADALA YA KUJENGA UKUTA

Kila maumivu yana fundisho. Usiyatumie kujenga chuki au ukuta wa kutomwamini mtu tena.

Jiulize: “Nilijifunza nini kuhusu moyo wa binadamu? Nilijifunza nini kuhusu mipaka? Nilijifunza nini kuhusu mimi?”

Maumivu yasipoleta hekima, yanakuwa mateso bure. Wacha yakukue.

7. JENGA UPYA UTAMANI WA MAISHA BILA YEYE

Wakati mtu anaondoka, si dunia yote imeondoka.

Rudisha furaha ndogo ulizokuwa nazo: soma kitabu, fanya mazoezi, soma neno la Mungu, tembelea watu wanaokujali kwa dhati.

Polepole utaona, maisha yana rangi nyingine hata bila mtu huyo.

Usiishi kwa kumbukumbu ya jana. Kila siku mpya ni nafasi ya kuandika ukurasa mpya wa furaha yako.

8. WACHA MUNGU AWE DAKTARI WA MOYO WAKO

Kuna maumivu ambayo hakuna maneno, hakuna marafiki, hata pesa haiwezi kutuliza—lakini Mungu anaweza.

Mpe nafasi aingie katika nafasi iliyoachwa wazi.

Omba si kwa hasira, bali kwa upole: “Bwana, nisaidie nione maana ya hili.”

Mara nyingi, Mungu anaondoa mtu fulani sio kwa sababu hakupendi, bali kwa sababu hawezi kuwa sehemu ya hatima yako.

9. JIFUNZE KUPENDA KWA HEKIMA, SIO HURUMA

Wakati mwingine, tuliumizwa si kwa sababu tulipenda vibaya, bali tulichanganya huruma na upendo.

Safari ijayo, usipende kwa sababu unahisi huruma au unataka kuokoa mtu. Penda kwa uwiano—kwa moyo na akili.

Weka mipaka ya hisia zako; upendo usio na mipaka huvuta watu wasio na mipaka.

10. TENGENEZA MAONO MPYA YA MAISHA YAKO

Ukipoteza mtu, usione ni mwisho. Ni nafasi ya kujenga toleo jipya la wewe.

Andika malengo mapya. Fufua ndoto ulizoacha kwa sababu yake.

Usiruhusu maumivu yakufanye ushindwe kuamini tena katika upendo.

Mtu sahihi hatatisha uhuru wako, hatakufanya ujisikie mdogo, wala hatakupenda kwa sababu ya msaada wako—atakupenda kwa sababu ya utu wako.

MANENO YA KUHITIMISHA

Usijilaumu kwa kuwa mtu mzuri.

Wema wako si upumbavu, ni zawadi ambayo dunia inahitaji.

Lakini sasa umejifunza kitu muhimu — kwamba upendo haumaanishi kujitolea hadi kujiua ndani.

Upendo wa kweli ni ule unaoweza kutoa na bado ukaendelea kujiheshimu.

Na siku moja, utamuangalia nyuma huyo aliyekuacha, moyo wako ukiwa umetulia, halafu utasema kwa utulivu:

“Asante kwa kuniumiza, maana maumivu yako yamenifundisha kujipenda.”

Katika maisha jifunza jambo kubwa:

Ukidhalilishwa, usighadhibike.

Ukitengenezewa fitna, usichukie.

Ukiwekewa ukuta, usijaribu kuubomoa kupita kwa nguvu.

Ukitengenezewa majungu, umia lakini jikaze.

Mungu ana njia zake za kukufariji, na pia ana namna zake za kuwaadhibu wale wanaokuumiza. Subira ni silaha kubwa.

Weka moyoni mwako kumbukumbu za watu hawa katika maisha yako:

Aliyekuinua wakati ulikuwa chini.

Aliyekuhifadhi wakati huna pa kujihifadhi.

Aliyekuacha ukiwa kwenye giza la matatizo.

Aliyekupa heshima wakati ukidharauliwa.

Aliyekupa thamani uliponyimwa thamani.

Aliyekusogelea wakati wengine walikukimbia.

Unapopitia maumivu, usijiumize zaidi kwa kumfikiria sana yule aliyekuletea machungu. Dawa ya maumivu ni kukubali hali, kusimama imara, na kusonga mbele. Usijiumize kwa sababu kufanya hivyo ni kutimiza malengo ya yule aliyekutesa.

Kauli ya, “Sikuamini kama fulani anaweza kunifanyia hivi,” imetoka kwa wengi walioumizwa na watu wao wa karibu. Ili ujilinde, nenda kwenye kioo na muamini unayemuona humo – huyo ndiye usalama wako wa kweli. Wengine wape furaha, lakini usiwape imani yako yote.

Kumbuka: Ukiishi kwa kuumiza wengine, Mungu hukuletea watu wa kukuumiza wewe na kizazi chako. Lakini ukiishi kwa kuwafariji na kuwapa furaha wengine, Mungu hukuletea watu wa kukuinua na kukufurahisha. Wema husafiri mbali, lakini uovu husafiri mbali zaidi.

Muda hauwezi kubadilisha mtu, bali hufichua sura yake halisi. Kadiri unavyosubiri, ndivyo muda utakavyokuletea majibu ya kweli kuhusu watu wanaokuzunguka. Kuwa mtulivu, muda ndio shahidi wa haki.

Maisha haya tumeazimwa kila kitu: uhai, afya, uzuri, ubaya, utajiri na hata umasikini. Siku Mungu akiamua, huchukua tu alichotuazima bila kutuomba ruhusa wala kutuandaa. Kwa sababu hiyo, tuishi maisha kwa nidhamu, kwa unyenyekevu na heshima – maana cha kuazimwa si cha kutamba nacho.

Dondoo 15 za matumizi sahihi ya muda ambazo zinaweza kukusaidia kazini na hata kwenye maisha ya kila siku:

1. Panga ratiba ya kila siku – andika majukumu yako kabla ya kuanza siku.

2. Weka vipaumbele – fanya mambo ya muhimu kwanza.

3. Tumia kalenda au daftari la kumbukumbu – kusaidia kukumbuka tarehe na mikutano.

4. Epuka kazi nyingi kwa wakati mmoja (multitasking) – maliza moja kabla ya kuanza nyingine.

5. Weka muda maalum wa mapumziko – kupunguza uchovu na kuongeza ufanisi.

6. Tumia teknolojia kwa busara – alarms, reminders, na apps za kupanga muda.

7. Punguza usumbufu – kama simu na mitandao ya kijamii unapofanya kazi.

8. Gawa majukumu (delegation) – usijaribu kufanya kila kitu mwenyewe.

9. Weka muda wa dharura (buffer time) – kati ya majukumu ili kuepuka msongo.

10. Anza mapema – kufanya kazi kubwa kabla ya muda haujaenda sana.

11. Jifunze kusema ‘hapana’ – kwa kazi au shughuli zisizo na umuhimu mkubwa.

12. Weka malengo ya muda mfupi na mrefu – ili kujua unakoelekea.

13. Kagua maendeleo yako – angalia kama unatumia muda vizuri.

14. Tambua saa zako za ufanisi zaidi – fanya kazi ngumu wakati akili ikiwa timamu.

15. Hifadhi muda kwa ajili ya familia na afya yako – usitumie muda wote kazini pekee.
●Wivu wa mapenzi wadaiwa kuwa chanzo cha tukio la kusikitisha

Na Regina Ndumbaro, Songea-Ruvuma.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Ruvuma linamshikilia mwanamke mmoja, Wende Luchagula, kwa tuhuma za mauaji ya kikatili ya watoto watatu, akiwemo Lugola Lutelemula mwenye umri wa miaka 6 pamoja na mapacha wa miezi minane, Kulwa na Doto Lutelemula – wote wakazi wa kijiji cha Milonji, kata ya Lusewa, Wilaya ya Namtumbo.

Tukio hilo la kusikitisha lilitokea mnamo tarehe 12 Julai 2025, na linasemekana kuchochewa na wivu wa mapenzi kati ya wake wawili wa mume mmoja.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 25, 2025 katika Manispaa ya Songea, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Mkoa wa Ruvuma (SACP), Marco G. Chilya (Pichani) amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa tukio hilo lilitekelezwa majira ya saa nane mchana na tayari mtuhumiwa anashikiliwa na Polisi kwa hatua zaidi za kisheria.

“Tukio hili limehuzunisha na kushtua taifa zima, hasa ikizingatiwa kuwa waliouawa ni watoto wadogo wasio na hatia. Jeshi la Polisi limechukua hatua stahiki kuhakikisha mtuhumiwa anafikishwa kwenye vyombo vya sheria haraka iwezekanavyo,” alisema Kamanda Chilya.

Aidha, Jeshi la Polisi Mkoa wa Ruvuma limetoa rai kwa wanandoa wanaoishi katika ndoa za wake wengi kuwa wavumilivu, kujiepusha na chuki au wivu wa kupindukia, na kutafuta suluhu kwa njia ya amani kupitia viongozi wa dini, wazee wa familia au viongozi wa kijamii.

Pia, jamii imetakiwa kuendelea kushirikiana na vyombo vya dola kwa kutoa taarifa mapema pale panapojitokeza viashiria vya migogoro au uvunjifu wa amani, ili kuzuia madhara makubwa kama haya kutokea tena.

Jeshi hilo limeahidi kuendelea kushirikiana na wananchi katika kuhakikisha mazingira salama na yenye ustawi kwa wote, hasa watoto ambao ni kundi lenye uhitaji mkubwa wa ulinzi na upendo kutoka kwa jamii nzima.
Wanawake (kama ilivyo kwa wanaume pia) wanaweza kutumia mbinu mbalimbali kuficha usaliti wa kimapenzi. Hapa chini ni baadhi ya njia ambazo wanawake hutumia kuficha usaliti, kulingana na uzoefu wa wataalam wa mahusiano, saikolojia ya tabia na simulizi halisi za maisha:

●1. Kubadilisha Ratiba Ghafla lakini kwa “Sababu Zenye Mantiki”

Wanawake wengi huongeza muda kazini au huanza “mashughuli mapya” kama:

Kujitolea kusaidia kwenye taasisi zisizo za kiserikali

Kujiunga na vikundi vya mazoezi au ibada

Kufanya “shughuli za kikazi” weekend Sababu hizi zinaonekana halali, lakini huweza kutumika kuficha miadi ya faragha.

●2. Kuongeza Umakini Kwa Mpenzi Wake Halali (Ili Kuficha Hatia)

Baadhi ya wanawake wanaosaliti huanza kuonyesha:

Mapenzi ya ghafla yasiyo na sababu

Zawadi zisizotarajiwa

Kuwa wapole kuliko kawaida Hili hufanyika ili kumshawishi mwanaume kwamba hakuna tatizo lolote, huku wakificha hatia ya usaliti.

●3. Kulinda Simu Kupita Kiasi

Kuweka password ngumu

Kuondoka na simu hata chooni

Kupokea simu wakiwa na wasiwasi au kwenda mbali kupokea

Kubadilisha majina ya wapenzi wa pembeni kuwa majina ya jinsia moja au "Boss", "Client", "Auntie"

●4. Kuanzisha Migogoro Isiyo na Sababu

Anakuchokonoa bila sababu, au anakulaumu kwa kila kitu

Anaanzisha ugomvi ili awe na “sababu” ya kutokulala nyumbani au kutopatikana

Anaacha kuonyesha upendo na mguso wa kimapenzi kama njia ya “kukwepa lawama”

●5. Kujifanya Ameokoka au Amebadilika Dini Sana

Anaanza kujitenga kimapenzi akitumia kisingizio cha “safari ya kiroho”

Anatumia dini kuficha ukweli kwamba hayuko sawa kihisia, wakati sababu halisi ni usaliti

●6. Kulalamika Sana Kwamba “Anafuatiliwa”

Anakushambulia kuwa unamchunguza sana ilhali wewe hujauliza chochote

Anaanza kutumia maneno kama “huna imani na mimi”, “mbona unanipima?”, “mapenzi si kifungo” Hili ni janja ya kujikinga asije akaulizwa maswali kuhusu mienendo yake isiyoeleweka.

●7. Kudai Hana Hamu ya Tendo la Ndoa Kwa Muda Mrefu

Anaweza kudai yuko “stressed”, ana uchovu wa kazini, au ana matatizo ya kiafya

Lakini ukweli ni kwamba mahitaji yake ya kimapenzi yanatimizwa kwingine

●8. Kuweka Siri Za Safari au Mikutano

Hataki uende naye kazini au kwenye sherehe fulani

Anasema amesafiri kikazi lakini hawezi kupiga simu au kutuma picha

Safari nyingi za ghafla zisizopangwa

●9. Kudai Rafiki wa Kike (ambaye si halisi)

Hucheza karata ya rafiki wa kike aliyempenda sana: “Niko na Asha”, kumbe ni mwanaume

Anaweka picha feki au hutaja majina ya ndugu wa jinsia moja kama kisingizio

 ●10. Kuvuruga Mawasiliano na Familia Yako

Anaanza kutopenda marafiki na ndugu zako

Anakata mawasiliano na watu waliokuwa wa karibu Sababu: watu hao wanaweza kuona au kuhisi tabia yake isiyo ya kawaida

Hitimisho:

Sio wanawake wote hufanya haya. Hizi ni tabia za mtu binafsi, sio jinsia nzima. Pia, wanaume pia hutumia mbinu nyingi sana kuficha usaliti. Njia bora ya kushughulikia mashaka ya usaliti ni mawasiliano ya wazi, uchunguzi wa tabia (si tuhisia), na msaada wa kitaalamu wa mahusiano pale panapohitajika.
Kwanza kabisa ni muhimu kuelewa kwamba mahusiano ya kimapenzi ni safari ya pamoja ambayo inahitaji mawasiliano, uvumilivu na kujitolea.

Kumridhisha mke wako kimapenzi sio tu juu ya tendo la ndoa bali ni kuhusu kuunda uhusiano mzuri na wenye afya. Kuna hatua kadhaa za kuzingatia

1. #MAWASILIANO
Ongea na mke wako kuhusu hisia zake, anachopenda na kile ambacho hakipendi. Mawasiliano ya wazi na ya heshima ni msingi wa mahusiano mazuri.

2. #UELEWA WA MWILI
Jifunze kuhusu mwili wa mke wako na anavyopenda kuguswa. Hii inaweza kusaidia kugundua maeneo yanayompa raha zaidi.

3. #USIHARAKISHE
Chukua muda wako na usiharakishe tendo la ndoa. Fanya maandalizi ya kimapenzi kama vile mabusu, kukumbatiana na mambo mengine ya upendo. Zingatia pia mambo madogo madogo ambayo yanaweza kumfurahisha mke wako nje ya tendo la ndoa kama vile kumletea maua au zawadi yoyote, kumwandikia ujumbe wa mapenzi au hata kumwandalia mtoko wa jioni. Hayo yatamfanya ajione unampenda,unamjali na unamthamini.

4. #UVUMILIVU NA UPENDO
Uvumilivu ni muhimu. Kila mtu ana mapungufu yake,pata muda wa kumjua mke wako vizuri. Hakikisha unamwonyesha upendo na kujali.

5. #ELIMU NA ZIADA.
Usione aibu kutafuta elimu zaidi kuhusu mahusiano na mapenzi. Vitabu, makala na mazungumzo na wataalamu wa mahusiano vinaweza kukusaidia kuongeza uelewa wako.

KUMBUKA
Lengo ni kumfanya mke wako ajisikie salama, kuthaminiwa na kupendwa.

Hii ndiyo njia ya uhakika ya kujenga mahusiano ya kimapenzi yenye afya na furaha.

Ni mimi shangazi mtiifu.
Joyce wa Moro
Mwalimu wa MAHUSIANO, UCHUMBA NA NDOA.

0658474191
*Awashauri CHADEMA kuacha maandamano

*Asisitiza umoja, mshikamano na maridhiano

Na Mwandishi Wetu

MAKAMU Makamu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Abdulurhman Kinana, ameshauri vyama vya siasa vya upinzani hususan CHADEMA kuacha kufanya maandamano yasiyo na msingi badala yake wathamini nia njema aliyonayo Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika kuleta maridhiano na kuwatumikia Watanzania.

Aidha, ametumia nafasi hiyo kufafanua kwa kina ubora wa sheria ya uchaguzi ambayo imepitihswa na Bunge hivi karibuni, baada ya wadau mbalimbali nchini kutoa maoni yao ambapo amesisitiza sheria hiyo ni bora kuliko iliyopo sasa.

Kinana aliyasema hayo jana Dar es Salaam alipozungumza na wana CCM na wazee wa mkoa wa Dar es Salaam, ambapo mbali ya kutumia muda mwingi kuzungumzia, maridhiano yaliyoingiwa kati ya CCM na CHADEMA pamoja vyama vingine vya upinzani, alisema kuna mambo mengi mazuri yamefanyika.

Alisema mambo mazuzi yamefanikisha kupata mwafaka ingawa CHADEMA haitaki kueleza ukweli ikiwemo serikali kukipatia chama hicho ruzuku ya Sh.bilioni 2.7 ambayo waliikataa kwa miaka mitatu nyuma.

Akielezea kuhusu sheria mpya, Kinana alisema pamoja na uzuri wake ikiwemo kuzingatia maoni ya wadau wakiwemo CHADEMA wenyewe, lakini bado kinasema haifai.

“Nilifikiri sheria hii mpya wangesema itatufikisha mbali zaidi, lakini wao wanasema hii haifai, basi turudi kule. Sheria ya sasa ni bora kwa muundo, kwa maudhui, kwa malengo, kwa dhamira sijui mnanielewa?. Nitumie nafasi hii kuwasihi ndugu zangu wa CHADEMA waungane na Watanzania waachane na mandamano, waangalie dhamira ya Rais.

“Hivi Rais na baraza lake la mawaziri kama wasingepeleka hii sheria mpya ya uchaguzi nani angemlazimisha? Lakini Rais busara imemuongoza akasema hapana hebu twende pamoja na mimi ndio mtetezi mkubwa wa maridhiano na ustahimilivu. Hebu tupeleke sheria mpya bungeni na kila hoja aliyopelekewa, aliyoambiwa kwamba haya ndio maoni ya wadau Rais akasema sawa, nakubali.
“Sasa niwasihi ndugu zangu Watanzania, tujipange kwa uchaguzi wa serikali za mitaa, tujipange kwa uchaguzi mkuu mwaka 2025. Sheria hii ni nzuri, bora kuliko sheria yoyote iliyopo katika historia ya nchi yetu, inakidhi mahitaji na matakwa ya nchi na jumuiya ya madola, inakidhi mahitaji ya nchi za Umoja wa Afrika (AU), inakidhi vile vile mahitaji ya nchi za Kusini mwa Afrika ambao na sisi ni wanachama,” alisema.

Aliongeza kwamba hakuna tume ya miujiza zaidi itakayokuwepo, huku akifafanua kila jambo ambalo litafanyika lazima litakuwa na kasoro moja au mbili, na kuhoji kwani CHADEMA wao hawana kasoro?.

“Wanazo, sasa nawaambia ninyi chama kikuu cha upinzani kuweni basi na ustahimilivu kidogo, uungwana na kusikiliza wenzenu na kuona nia njema iliyopo katika Chama Cha Mapinduzi, kwa na serikali yake,” alisema.

Akifafanua zaidi Kinana alisema kuwa kushinda uchaguzi kunatokana na sera, mipango ya uchaguzi na kusikiliza watu, kwani unaweza kuwa na tume nzuri ya uchaguzi na matokeo yakawa ni ya hovyo, usiyoyataka.

Alitoa mfano wa moja ya nchi jirani ambayo walipigania sana kuwa na tume huru kwa miaka 20, wakaipata, lakini wamegombea mara nne hawakupata.

“Hawakuingia madarakani, wale waliotengeneza hiyo tume hawakupata, sasa wanasema Katiba hii haina maana waifute, wale walioingizwa na katiba baadae nao wakashindwa wanasema katiba hii haina maana. Kwa hiyo aliyeshinda anasema Katiba haina maana na aliyeshindwa naye anasema Katiba haina maana.

“Sasa kushinda uchaguzi sio Katiba tu, Nigeria baada ya wanajeshi kutoka baradakani walitengeneza Katiba mpya mwaka 1969 na kwa sehemu kubwa walienda kuchukua Katiba ya Marekani, tume ya uchaguzi ya Rais inateuliwa na Rais kwa kushauriana na baraza la ushauri.

“Baraza la ushauri ni nani? Rais ndio Mwenyekiti, makamu mwenyekiti ni makamu wa rais, wajumbe wengine marais wastaafu, hapo vipi? Kuna mtu anatoka nje ya mfumo?

“Hao ndio wanateua, mwenyekiti na makamu mwenyekiti wa tume, uchaguzi unafanyika na watu wanakubali. Hapa tunatafuta malaika wa kuja kuongoza tume, kila utakachofanya unaambiwa kinakasoro, hivi mnavyoona yote tuliyokubali wanasema hamna kitu.

“Nimesikia wanaandaa maandamano Mwanza, Mbeya na Arusha na mimi nataka niwasaidie kutangaza kama watu wengine hamjasikia. Wanakwenda kueleza haya yaliyopitishwa na CCM na Bungeni hamna kitu.

“Tume si kila kitu, Namibia kamati inatengenezwa baada ya pale anayetua Rais, kuna nchi inaitwa Mauritius na hizi nchi zote ambazo nimezitaja ni za Jumuiya ya Madola, Rais anashauriana na watu wawili tu, anashauriana na waziri mkuu na kiongozi wa upinzani bungeni hakuna mtu mwingine,” alisisitiza.

“India wana mkurugenzi na wana makamishina. Nani anateua? Waziri Mkuu na Baraza lake la Mawaziri kwisha, yaani Rais Samia akae na baraza lake la mawaziri atengeneze orodha ateue, si moto utawaka hapa? Watasema tu maigizo.

“Sasa kuna shida hapa nchini kila unalofanya halina heri ndani yake, lakini vizuri haya mambo tukayaeleza maoni mengine yakatolewa unajua siku hizi kuna watu wanapita bila kupingwa lakini ni vizuri wanaopita bila kupingwa wakapigiwa kura ya ndio au hapana Bunge likasema sawa tumekubali.

“Wanauliza kwa nini? Wanasema kuna watu wengine wanafanya ujanjaujanja wa kupita bila kupingwa, hivyo wapigiwe kura tujue kama wanakubalika Bunge limesema sawa itapigwa kura ya ndio au hapana,” alisema.

KUHUSU MARIDHIANO

Akizungumzia maridhiano ambayo yamefanyika kwa nyakati tofauti, Kinana alisema kuwa wakati Rais Samia Suluhu Hassan anaingia madarakani kulikuwa na wanachama wa CHADEMA wasiopungua 400 wako mahabusu wakikabiliwa na kesi zilizotokana na sababu mbalimbali za kiuchaguzi, lakini ulitengenezwa utaratibu wa kisheria waakachiwa huru.

Kinana alisema hakuna maridhiano bila ustahimilivu, Rais alialika taasisi za kidini na kiraia ili waelewane kujiuliza nini wanahitaji kwa lengo la kuhakikisha tunakuwa na taifa liwe la watu wenye mshikamano na kupendana.

Alisema Dk. Samia aliunda tume ya kusikiliza makundi ya Watanzania kusikiliza hoja zao ikiwemo Katiba, lakini mwishowe CHADEMA waligomea kwa sababu zao.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba (katikati), akizungumza wakati alipokuwa akiukagua mradi wa maji katika Kijiji cha Matare uliotekelezwa na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Wilaya ya Ikungi wakati wa ziara yake aliyoifanya leo Juni 6, 2023.

Na Dotto Mwaibale, Ikungi

MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba amefurahishwa na kuridhishwa na usimamizi mzuri na ukamilishaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi na kuwapongeza viongozi wote kwa utekelezaji wa miradi hiyo kwa thamani halisi ya fedha zilizotolewa na Serikali.

Serukamba ametoa pongezi hizo wakati wa ziara yake wilayani humo aliyoifanya leo Juni 6, 2023 ambapo alipata fursa ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kuhimiza ikamilike kabla ya Julai 1, 2023.

Aidha, Serukamba amewapongeza wataalam na wananchi kwa kuunga mkono juhudi za serikali kwa kuchangia utalaam na nguvu kazi katika kutekeleza miradi hiyo ambayo imegharimu fedha nyingi.

"Serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imefanya kazi kubwa kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi hii naomba tumuheshimishe Rais wetu kwa kuikamilisha haraka kabla ya Julai 1, 2023 ili ianze kutumika," alisema Serukamba.

Alisema Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi imekuwa ikimpa raha kutokana na kufanya vizuri katika kutekeleza miradi ya maendeleo na kuwa imekuwa ikipata mafanikio hayo kutokana na ushirikiano uliopo baina ya viongozi, wataalam na wananchi.

Miradi aliyoitembelea na kuikagua ni mradi wa maji katika Kijiji cha Matare uliopo Kata ya Unyahati uliogharimu Sh. Milioni 386.8 ambao utawahudumia wananchi 5036, ujenzi wa madarasa katika Shule ya Msingi Matare na ujenzi wa mabweni mawili na bwalo katika Shule ya Msingi Ikungi.

Miradi mingine aliyoitembelea na kuikagua ni ujenzi wa madarasa katika Shule ya Msingi ya Ikungi B, ujenzi wa madarasa katika Shule ya Sekondari ya Ikungi ambayo sasa imekuwa na kidato cha tano na sita, ukaguzi wa mradi wa Kikundi cha vijana kijulikanacho kama Ikungi Chapakazi ambao unajishughulisha na ufyatuaji wa matofali ambapo aliwataka wana kikundi hicho kurejesha mkopo waliokopeshwa na Halmashauri ya Ikungi ili waweze kukopeshwa vijana wengine.

Aidha, miradi mingine iliyokaguliwa na kuhimiza ikamilike haraka ni ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Ikungi, ukaguzi wa ujenzi wa madarasa katika Shule ya Msingi ya Dung'unyi na ujenzi wa barabara ya Ikungi- Matongo yenye urefu wa kilometa moja.


Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, akipokea taarifa ya ujenzi wa madarasa katika Shule ya Msingi Matare.
Muonekano wa madarasa yanayo jengwa Shule ya Msingi Matare.
Muonekano wa kazi nzuri ya utunzaji wa mazingira katika Shule ya Msingi Matare inayofanywa na walimu wa shule hiyo kwa kuwashirikisha wanafunzi.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba (katikati) akiwa na viongozi wengine wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Ikungi.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba (mbele) akiongoza msafara wa viongozi mbalimbali na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hiyo kuelekea kutembelea jengo la Ustawi wa Jamii linalo ratibu na kusimamia shughuli za upingaji wa vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa watoto wa kike na kiume na wanawake katika Wilaya ya Ikungi
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba (mbele) akiongoza msafara wa viongozi mbalimbali na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hiyo kuelekea kutembelea jengo hilo.Muonekano wa jengo hilo.
Muonekano wa mabweni mawili yalio jengwa Shule ya Msingi, Ikungi.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mabweni mawili na Bwalo katika Shule ya Msingi Ikungi. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Thomas Apson.
Muonekano wa ujenzi wa madarasa katika Shule ya Msingi Ikungi B
Taswira ya ujenzi wa madarasa katika Shule ya Sekondari ya Ikungi.
Mhandisi wa Wilaya ya Ikungi, Edward Millinga (katikati), akitoa maelezo ya ujenzi wa madarasa katika Shule ya Sekondari ya Ikungi. Wa kwanza kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Justice Kijazi
na wa pili ni Mkuu wa Shule hiyo, Madamu Neema Stephano.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba (katikati) akiongoza msafara wa viongozi mbalimbali na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hiyo wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa Barabara ya Ikungi-Matongo.
Taswira ya mradi wa vijana Chapa kazi Ikungi, unaojishughulisha na ufyatuaji wa matofali.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Ikungi, Zilfat Muja (katikati) akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida (wa wanne kutoka kushoto) kuhusu mradi huo. Kutoka kushoto ni Afisa Maendeleo wa Wilaya ya Ikungi, Haika Masawe, Mwenyekiti wa kikundi hicho, Mwanahamisi Omari, Mkuu wa wilaya hiyo, Thomas Apson na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Ally Mwanga.


Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba akitoka kukagua ujenzi wa madarasa katika Shule ya Msingi Dung'unyi wakati wa ziara hiyo. Katikati ni Diwani wa Kata hiyo, na kushoto kwa diwani ni Afisa Mtendaji wa kata hiyo, Yahaya Njiku.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza wakati uzinduzi wa Filamu ya Tanzania'The Royal Tour' ambapo hafla ya Uzinduzi wa Filamu hiyo unafanyika Katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam leo Mei 8, 2022.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Hussein Ali Mwinyi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa tayari wamewasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere tayari kwa ajili ya Uzinduzi wa Tanzania The Royal Tour ambapo mgeni rasmi ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Na Said Mwishehe, Michuzi TV

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania samia Suluhu Hassan ametoa rai kwa Watanzania wa sekta mbalimbali ikiwemo ya utalii kujitayarisha kupokea watalii watakaokuja kutalii nchini.

Ametoa rai hiyo leo Mei 8, 2022 wakati akizindua filamu ya Royol Tour katika Jiji la Dar es Salaam ikiwa ni siku chache tu baada ya kuzinduliwa rasmi nchini Marekani, kisha jijini Arusha na baadae Zanzibar.

“Mategemeo yangu baada ya filamu hii kuzinduliwa Tanzania inatakiwa kujitayarisha kupokea wageni wengi, wageni watakuwa wa tofauti tofauti hizo hata watakapokuja watakaa katika hoteli za tofauti.

“Hivyo nitoe rai kwa sekta za utalii kujitayarisha ili watalii wakija wakute hoteli zipo, wakute watu wa kupokea wageni wapo, wapokea wageni viwanja vya ndege nao wajiandea.

“Zile sifa ambazo zimeoneshwa kwenye filamu lazima uonekane, tunapaswa kujitayarisha, watu wa sekta ya utalii na sekta nyingine tujitayarishe, narudia tena lazima Watanzania wote tujitayarishe,amesema Rais Samia.

Aidha amesema kuzinduliwa kwa Filamu ya Royol Tour ni mwanzo tu wa kuzindua filamu nyingine za Royal Tour awamu ya pili na ya tatu kwani kuna picha nyingi ambazo zilichukuliwa ambazo zitatumika kutengeza filamu nyingine kwa lengo la kendelea kutangaza utalii wa Tanzania.

“Filamu hii ya Royal Tour ni mwanzo tu kwani nyingine zitakuja.Nimpongeze Rais wa Zanzibar Dk.Hussein Mwinyi kwa ushiriki wake mzuri kwenye filamu hii na amekuwa na msemo wake kuwa yajayo yanafurahisha, hivyo tuseme yajayo yanafurahisha”amesema Rais Samia.