Katika maisha jifunza jambo kubwa:
Ukidhalilishwa, usighadhibike.
Ukitengenezewa fitna, usichukie.
Ukiwekewa ukuta, usijaribu kuubomoa kupita kwa nguvu.
Ukitengenezewa majungu, umia lakini jikaze.
Mungu ana njia zake za kukufariji, na pia ana namna zake za kuwaadhibu wale wanaokuumiza. Subira ni silaha kubwa.
Weka moyoni mwako kumbukumbu za watu hawa katika maisha yako:
Aliyekuinua wakati ulikuwa chini.
Aliyekuhifadhi wakati huna pa kujihifadhi.
Aliyekuacha ukiwa kwenye giza la matatizo.
Aliyekupa heshima wakati ukidharauliwa.
Aliyekupa thamani uliponyimwa thamani.
Aliyekusogelea wakati wengine walikukimbia.
Unapopitia maumivu, usijiumize zaidi kwa kumfikiria sana yule aliyekuletea machungu. Dawa ya maumivu ni kukubali hali, kusimama imara, na kusonga mbele. Usijiumize kwa sababu kufanya hivyo ni kutimiza malengo ya yule aliyekutesa.
Kauli ya, “Sikuamini kama fulani anaweza kunifanyia hivi,” imetoka kwa wengi walioumizwa na watu wao wa karibu. Ili ujilinde, nenda kwenye kioo na muamini unayemuona humo – huyo ndiye usalama wako wa kweli. Wengine wape furaha, lakini usiwape imani yako yote.
Kumbuka: Ukiishi kwa kuumiza wengine, Mungu hukuletea watu wa kukuumiza wewe na kizazi chako. Lakini ukiishi kwa kuwafariji na kuwapa furaha wengine, Mungu hukuletea watu wa kukuinua na kukufurahisha. Wema husafiri mbali, lakini uovu husafiri mbali zaidi.
Muda hauwezi kubadilisha mtu, bali hufichua sura yake halisi. Kadiri unavyosubiri, ndivyo muda utakavyokuletea majibu ya kweli kuhusu watu wanaokuzunguka. Kuwa mtulivu, muda ndio shahidi wa haki.
Maisha haya tumeazimwa kila kitu: uhai, afya, uzuri, ubaya, utajiri na hata umasikini. Siku Mungu akiamua, huchukua tu alichotuazima bila kutuomba ruhusa wala kutuandaa. Kwa sababu hiyo, tuishi maisha kwa nidhamu, kwa unyenyekevu na heshima – maana cha kuazimwa si cha kutamba nacho.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza wakati uzinduzi wa Filamu ya Tanzania'The Royal Tour' ambapo hafla ya Uzinduzi wa Filamu hiyo unafanyika Katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam leo Mei 8, 2022.






Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Hussein Ali Mwinyi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa tayari wamewasili katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere tayari kwa ajili ya Uzinduzi wa Tanzania The Royal Tour ambapo mgeni rasmi ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.



.jpeg)


.jpeg)








.jpeg)





