TRENDING NOW






Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Kassim akizindua Wiki ya Vijana kitaifa uliofanyika Jijini Mwanza.


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Kassim   amewataka vijana wa Kitanzania kutumia fursa za maendeleo ya kidigitali kama njia ya kujitengenezea fursa za ajira na kuacha kutumia mitandao ya kijamii kwa mambo yasiyofaa.

Mhe. Majaliwa amewataka vijana kufichua na kuziainisha taasisi zenye nia ovu ya kuharibu na kuvunja mila na desturi za Kitanzania, pamoja na taasisi hizo binafsi kujitambulisha na kutoa malengo ya Taasisi.

Katika kuadhimisha siku ya Vijana Kitaifa, Shirika lisilo la kiserikali la BRAC Maendeleo Tanzania,limeadhimia kuendelea na kuwekeza kwenye kutoa elimu zaidi kuhusiana na maendeleo ya vijana

Akizungumzia maadhimisho hayo, Meneja wa Mkoa Mwanza Novatus Tarimo amesema elimu wanayotoa kwa vijanai ni  kuwawezesha vijana kupaza sauti kwa Serikali na  jamii ili waweze kujiinua kiuchumi kupitia fursa mbalimbali zilizopo.

Amesema, Shirika la BRAC Maendeleo Tanzania limekuwa na miradi ya uwezeshaji kiuchumi kwa vijana na ikiwa ni katika  kuunga mkono Serikali ya awamu ya sita kwa kuwainua kiuchumi na kuwapa fursa za kujiajiri.

Tarimo amesema,  wao ni Wadau namba moja wa maendeleo na wamekuwa wakifanya kazi na Serikali kwa ngazi ya kitaifa na  kuwekeza kwenye kutoa hamasa kutokana na matakwa muhimu kwa wakati huo.

 "Vijana ndio taifa la kesho, kuna kila sababu ya kuwasaidia vijana hawa kwa kupaza sauti zao na kuwapatia elimu ya zaidi ili waweza kujiendeleza na kujiinua kiuchumi na kujiajiri,"amesema Tarimo.

"Mradi wa AIM, unaojihusisha na utoaji wa elimu na uwezeshaji wa kiuchumi na katika kipindi chote umekuwa na mafanikio makubwa sana,"

BRAC Maendeleo ni shirika lililojikita katika kuwezesha kiuchumi vijana kwa elimu ya ujasiriamali, na kwa kutoa mikopo ya vikundi kwa wakina.mama kupitia BRAC Finance Limited.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Kassim aizungumza na Vijana waliojitokeza katika viwanja hivyo  amewataka vijana wa Kitanzania kutumia fursa za maendeleo ya kidigitali kama njia ya kujitengenezea fursa za ajira na kuacha kutumia mitandao ya kijamii kwa mambo yasiyofaa.Maandamano ya wafanyakazi na vijana wa BRAC Maendeleo Tanzania wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Vijana Kitaifa yaliyofanyika Jijini Mwanza.
Wananchi wakipita na kupata maelezo kutoka wafanyakazi wa BRAC Maendeleo Tanzania kuhusiana na uwezeshaji wa Vijana nchini
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) imeanza uchimbaji wa kisima eneo la Kisasa-Mwangaza Jiji Dodoma baada ya maagizo ya Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb.) kwa DUWASA kutafuta suluhisho la changamoto ya maji katika maeneo ya Kisasa Bwawani, Kisasa East, Nyumba 300 na Mwangaza.

Zoezi la uchimbaji wa kisima hicho umeanza Oktoba 11 na utakamilika Oktoba 12, 2024 huku hatua inayofuata ni upimaji wa wingi wa maji na ubora wa maji kabla ya kuanza uendelezaji wa kisima hicho.

Uchimbaji kisima eneo la Kisasa - Mwangaza ni hatua ya utatuzi wa changamoto ya ukosefu wahuduma ya maji kwa wananchi wa maeneo ya Kisasa Bwawani, Kisasa East, Nyumba 300 na Mwangaza.

Baadhi ya Wananchi na Viongozi wa Serikali ya Mtaa Nyumba 300 na Mwangaza wameishukuru serikali kwa kusikia kilio chao katika kuwapatia huduma ya maji.

Viongozi na wananchi waliotembelea uchimbaji wa kisima hicho leo ni Donatha Zitatu - Mwenyekiti wa Mtaa Nyumba 300, Vicent Malisa Balozi Mwangaza, Pendo Masigati- Mwananchi wa Nyumba 300 na Mathew Laurent- Balozi Nyumba 300.

Katika jitihada zake za kuendelea kuimarisha utekelezaji wa majukumu yake, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limekutana na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi kuzungumzia masuala ya usalama wa usafiri wa majini kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Kanali Mtambi ameipongeza TASAC kwa hatua mbalimbali wanazochukua kuimarisha masuala ya usafiri wa majini na ushirikiano wanaoutoa katika Mkoa wa Mara na hususan usalama wa wasafiri katika katika Ziwa Victoria.

Kanali Mtambi ameiomba TASAC kuendelea kutoa elimu kuhusu sheria na kanuni zinazohusiana na usafiri wa majini kwa wananchi na taasisi za Serikali na binafsi ili kupunguza ajali na athari za ajali za vyombo vya usafiri wa majini.
“Sisi kama Serikali tunatakiwa kuendelea kuwahakikishia usalama watumiaji wa Ziwa Victoria ikiwemo wasafiri wanaotumia vyombo vya usafiri vya majini kuhusiana na usalama wao wanapotumia usafiri wa majini,” amesema Mhe. Kanali Mtambi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Udhibiti, Ulinzi, Usalama na Utunzaji wa Mazingira na Usafiri wa Majini, Bi. Leticia Mutaki amesema TASAC inaendelea na jukumu lake la utoaji wa elimu ya usalama wa usafiri majini kwa wadau wa mikoa ya Kanda ya Ziwa ikiwemo taasisi na Halmashauri kuhusiana na usimamizi wa usafiri wa majini.
“Tuna mpango wa kuingia katika makubaliano ya ushirikiano na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Halmashauri zote zinazopakana na ziwa ili Halmashauri zisaidie kusimamia usafiri wa majini kwa niaba ya TASAC,” amesema Bi. Mutaki.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa TASAC, Bi. Judith Kakongwe amesema Sheria na kanuni za sasa zinawabana zaidi wenye vyombo vya usafiri kuweka jaketi okozi lakini haziwabani abiria kuzivaa jambo ambalo linaleta changamoto kwa sababu wamiliki wakiweka bila kuvaliwa hazisaidii kama inatokea ajali.

“Tupo kwenye mchakato wa kubadili vipengele vya sheria na kanuni ili abiria nao wabanwe kuvaa jaketi okozi na sio tu wamiliki wa chombo kama ilivyo sasa ili kusaidia kupunguza madhara ajali zinapotokea” amesema Bi. Kakongwe.
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewahimiza vijana nchini kuchangamkia fursa za kidijitali ikiwemo akili bandia (Artificial Intelligence), kwa kubuni mifumo itakayotatua changamoto za kijamii na hivyo kujipatia kipato.

Meneja TCRA Kanda ya Ziwa, Mhandisi Imelda Banali ametoa rai hiyo Ijumaa Oktoba 11, 2024 wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Vijana 2024 yanayofanyika katika uwanja wa Furahisha jijini Mwanza kuanzia Oktoba 08-14, 2024 yakiwa na kaulimbiu ya "vijana na matumizi ya fursa za kidijitali kwa maendeleo endelevu".

Amesema mamlaka hiyo inawawezesha vijana kunufaika na matumizi ya kidijitali kwa kutoa rasilimali za mawasiliano ili kufanikisha mawazo yao ya kibunifu ikiwemo kupata masafa na namba za kuwafikia wateja bure.

"Vijana wenggi wamekuwa na kasumba ya kupuuzia fursa mbalimbali za kimaendeleo zinazotangazwa mpaka waone watu wengine wamefanikiwa, tunapaswa kuchangamkia soko la kidijiti ili kujikwamua kiuchumia" amesema John Waronga ambaye ni mmoja wa vijana waliotembelea banda la TCRA.

Maonesho ya wiki ya vijana yamefunguliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ambaye amewataka vijana kutumia mitandao kujiajiri na kukuza uchumi ili kuwa na taifa lenye uchumi imara huku akiwataka kutotumia maendeleo hayo ya kidijitali kwa matumizi mabaya ikiwemo kuchochea chuki, kueneza taarifa za uongo na picha ama video zisizo na maadili katika jamii.


Majaliwa amesema ili kufikia dira ya maendeleo ya taifa 2050, teknolojia ya kidijitali ina fursa muhimu na maadhimisho hayo ni jukwaa muhimu kwa vijana kuwa chachu ya maendeleo na kwamba Serikali itaendelea kuwajengea vijana uwezo ili kufanikisha bunifu zao.
Na George Binagi- GB Pazzo, BMG
Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa, Mhandisi Imelda Banali (kulia) akitoa ufafanuzi wa shughuli mbalimbali zinazofanywa na mamlaka hiyo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Ridhiwani Kikwete (kushoto) alipotembelea banda la TCRA.
Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa, Mhandisi Imelda Banali (kulia) akisalimiana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Ridhiwani Kikwete (kushoto) alipotembelea banda la TCRA.
Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa, Mhandisi Imelda Banali (kulia) akitoa elimu kwa mwananchi aliyetembelea maonesho ya wiki ya vijana kuhusu kampeni ya 'Ni Rahisi Sana' inayoendeshwa na TCRA kwa lengo la kuhamasisha jamii kutambua fursa za kidijiti nk.
Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa, Mhandisi Imelda Banali (kulia) akioa elimu kwa mwananchi aliyeembelea banda la TCRA.
Tazama Video hapa chini

Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Christina Mndeme akitoa elimu na uhamasishaji wa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa wananchi wa Wilaya ya Gairo mkoani Morogoro Oktoba 10,2024 ambapo alikuwa mgeni rasmi katika Tamasha la tatu la ‘Samia Kilimo Biashara Expo 2024’.
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Christina Mndeme (kushoto) akipika ugali ikiwa moja ya njia ya kutoa elimu na uhamasishaji wa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa wananchi wa Wilaya ya Gairo mkoani Morogoro Oktoba 10,2024 katika Tamasha la tatu la ‘Samia Kilimo Biashara Expo 2024’ ambapo alikuwa mgeni rasmi.
Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabir Makame (katikati) akifafanua jambo kwa Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Christina Mndeme (kulia) ambaye alikuwa mgeni rasmi katika Tamasha la tatu la ‘Samia Kilimo Biashara Expo 2024’ lililofanyika Oktoba 10,2024 wilayani humo. Wa kwanza kushoto ni Mkurugeni wa Halmashauri ya Gairo, Bi. Sharifa Nabalang’anya.
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Christina Mndeme (kushoto) akigawa Nishati Safi ya kupikia kwa Juliana Ngunei ambaye ni mwanafunzi wa darasa la sita Shule ya Msingi Kisitwi ya Gairo Mkoani Morogoro ikiwa moja ya njia ya kutoa elimu na uhamasishaji wa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa wananchi katika Tamasha la tatu la ‘Samia Kilimo Biashara Expo 2024’ ambapo alikuwa mgeni rasmi, Oktoba 10,2024.
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Christina Mndeme (kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabir Makame (kulia) na Bi. Hilda Chilongola mkazi wa Gairo mkani Morogoro wakipika ugali ikiwa moja ya njia ya kutoa elimu na uhamasishaji wa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa wananchi kwa kutumia aina tofauti ya Nishati Safi katika Tamasha la tatu la ‘Samia Kilimo Biashara Expo 2024’ ambapo alikuwa mgeni rasmi Oktoba 10,2024.

Na Mwandishi Wetu Gairo 

Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Christina Mndeme ameupongeza uongozi wa Wilaya ya Gairo mkoani Morogoro namna jitihada zinavyochukuliwa katika kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Uongozi wa Wilaya ya Gairo umeandaa Tamasha ‘Samia Kilimo Biashara Expo 2024’ ambapo wananchi hupewa elimu mbalimbali ikiwemo faida ya matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia sambamba na athari zitokanazo na matumizi ya Nishati isiyo salama ya kupikia ya kutumia kuni na mkaa.

Bi. Mndeme ambaye alikuwa mgeni rasmi katika tamasha hilo Oktoba 10,2024 ameupongeza uongozi wa wilaya kwa namna ambavyo wamekuwa mstari wa mbele kwa kutoa elimu kwa wananchi wao juu ya matumizi ya nishati safi sambamba na kushirikiana na wadau wake ambapo wananchi wameanza kunufaika kwa kupata majiko ya gesi kwa bei nafuu na majiko banifu yakigawiwa bure kwa baadhi ya wananchi.

“Kila mmoja wetu anafahamu kwamba kinara namba mojoa wa uhamasisha wa matumizi ya nishati safi ni Rais wetu ambaye amekuwa akionesha mfano kwa vitendo na hiyo yote sababu ya upendo wake kwa wananchi ili kuepuka athari zitokanazo na matumizi ya kuni na mkaa.

“Niwaombe elimu hii na ugawaji wa majiko haya ifanyike hadi vijijini ili kila mtu anufaike na punguzo hii ambayo hapa tumeshuhudia wenzetu wakiipata kwani kwa kufanya hivyo tutaokoa watu wengi hasa kina mama ambao asilimia kubwa ndio tunaoshinda jikoni kuandaa chakula cha familia,” amesema Bi. Mndeme.

Kw aupande wake Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabir Makame amesema kwa kutambua umuhimu wa tamasha hilo wanashirikisha wadau mbalimbali ikiwemo wanaohusika na mazingira lengo ikiwa kuwasogezea fursa wananchi wa wilaya hiyo.

“Ajenda moja wapo iliyobebwa katika tamasha hili ni kuhusu nishati safi, ajenda ambayo imesisitizwa na kutolewa maelekezo na viongozi wetu na katika Wilaya ya Gairo tumeweza kuipa kipaumbele na kuifanyia kampeni na katika tamasha hili kila siku tumekuwa tukitoa elimu,” amesema Mhe. Makame.

Kaulimbiu ya tamasha hilo inasema “Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo na Mifugo.”
Mkuu wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa Vodacom Tanzania, Happiness Shuma (kushoto), Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Biashara kutoka Shirika la Reli Tanzania (TRC) Never Daimon, na Mkuu wa Idara ya Mauzo wa Vodacom Business, Rahma Dachi wakiwa wakifurahia mara baada ya kukata utepe ishara ya makubaliano ya ushirikiano na TRC ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja ambapo Vodacom imewasogezea huduma zake abiria wa treni hiyo maarufu kama ‘Treni ya Mwakyembe’ inayofanya safari zake hapa jijini Dar es Salaam.
Wakiķata keki mara baada ya kusaini makubaliano ya shirikiano na TRC ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja ambapo Vodacom imewasogezea huduma zake abiria wa treni hiyo maarufu kama ‘Treni ya Mwakyembe’ inayofanya safari zake hapa jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Vodacom na TRC wakifurahia pamoja ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja ambapo Vodacom imewasogezea huduma zake abiria wa treni hiyo maarufu kama ‘Treni ya Mwakyembe’ inayofanya safari zake hapa jijini Dar es Salaam.