Kwanza kabisa ni muhimu kuelewa kwamba mahusiano ya kimapenzi ni safari ya pamoja ambayo inahitaji mawasiliano, uvumilivu na kujitolea.

Kumridhisha mke wako kimapenzi sio tu juu ya tendo la ndoa bali ni kuhusu kuunda uhusiano mzuri na wenye afya. Kuna hatua kadhaa za kuzingatia

1. #MAWASILIANO
Ongea na mke wako kuhusu hisia zake, anachopenda na kile ambacho hakipendi. Mawasiliano ya wazi na ya heshima ni msingi wa mahusiano mazuri.

2. #UELEWA WA MWILI
Jifunze kuhusu mwili wa mke wako na anavyopenda kuguswa. Hii inaweza kusaidia kugundua maeneo yanayompa raha zaidi.

3. #USIHARAKISHE
Chukua muda wako na usiharakishe tendo la ndoa. Fanya maandalizi ya kimapenzi kama vile mabusu, kukumbatiana na mambo mengine ya upendo. Zingatia pia mambo madogo madogo ambayo yanaweza kumfurahisha mke wako nje ya tendo la ndoa kama vile kumletea maua au zawadi yoyote, kumwandikia ujumbe wa mapenzi au hata kumwandalia mtoko wa jioni. Hayo yatamfanya ajione unampenda,unamjali na unamthamini.

4. #UVUMILIVU NA UPENDO
Uvumilivu ni muhimu. Kila mtu ana mapungufu yake,pata muda wa kumjua mke wako vizuri. Hakikisha unamwonyesha upendo na kujali.

5. #ELIMU NA ZIADA.
Usione aibu kutafuta elimu zaidi kuhusu mahusiano na mapenzi. Vitabu, makala na mazungumzo na wataalamu wa mahusiano vinaweza kukusaidia kuongeza uelewa wako.

KUMBUKA
Lengo ni kumfanya mke wako ajisikie salama, kuthaminiwa na kupendwa.

Hii ndiyo njia ya uhakika ya kujenga mahusiano ya kimapenzi yenye afya na furaha.

Ni mimi shangazi mtiifu.
Joyce wa Moro
Mwalimu wa MAHUSIANO, UCHUMBA NA NDOA.

0658474191
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: