Baadhi ya wafanyakazi wa Barrick walioshiriki mbio za riadha za NBC DodomaMarathon 2024 wakifurahi baada ya kumaliza na kukabidhiwa medali za ushiriki
Baadhi ya wafanyakazi wa Barrick walioshiriki mbio za riadha za NBC DodomaMarathon 2024 wakifurahi baada ya kumaliza na kukabidhiwa medali za ushiriki.
Wafanyakazi wa kampuni ya Barrick nchini wameshiriki katika mbio za riadha za NBC DodomaMarathon 2024 zilizofanyika mkoani Dodoma ambapo wamemudu kukimbia mbio za masafa mbalimbali.

Kampuni ya Barrick nchini imekuwa na program za mazoezi kwa ajili ya kuhakikisha wafanyakazi wake wanakuwa na nguvu na afya bora.
Kila mwaka kampuni imekuwa ikiwezesha wafanyakazi wake kushiriki riadha mbalimbali na michezo ikiwemo mbio za kilomita 42 ya Bulyanhulu Healthy Lifestyle Marathon zinayofanyika kila mwaka.

Migodi yake ya North Mara na Bulyanhulu pia imewekeza kujenga miundombinu ya michezo na mazoezi ili kuwawezesha wafanyakazi wake kushiriki michezo na mazoezi katika mazingira rafiki kwa ajili ya kujenga afya zao.

Lengo kuu la mbio hizi zilizowashirikisha maelfu ya wakimbiaji kwa mujibu wa waandaaji lilikuwa ni kukusanya fedha ili kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na kutoa ufadhili wa elimu kwa wakunga ili kuboresha afya ya mama wa mtoto.

Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: