no image
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Amani Abeid Karume amesema kuwa madhumuni makubwa ya jengo jipya la Afisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar ni kuendeleza shughuli za kusimamia umoja na mshikamano wa kidini kwa wananchi wote wa Zanzibar.

Wito huo umetolewa leo na Alhaj Karume mara baada ya kulizindua rasmi jengo jipya la Afisi ya Muftii Mkuu wa Zanzibar lililopo Mazizini mjini Unguja lililojengwa kwa msaada wa Serikali ya Oman kutokana na juhudi binafsi za Sheikh Ahmad Al-khaliyl ambaye ni Mufti Mkuu wa nchi hiyo.

Alhaj Dk. Karume alisema kuwa jengo hilo litasaidia kwa kiasi kikubwa kutoa elimu na taaluma kwa Waumini wa dini ya Kiislamu na kusisitiza kuwa afisi hiyo itumike zaidi kwa kuendeleza mshikamano.

Alhaj Karume alisema kuwa historia ya Zanzibar inaonesha kuwa kutofautiana katika suala la kuandama kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani kulikuwepo tokea siku za nyuma kwani madhehebu ya Mabohora yalikuwa yakitofautiana na madhehebu mengine katika muandamo wakuandamisha mwezi huo lakini walizingatia heshima kwa madhehebu mengine.

“Tulikuwa tunatofautiana lakini katika jambo hilo tumejifunza ni kuwa wenzetu walikuwa wakitangulia mapema na wanasali Iddi katika msikiti wao na matayarisho yote yalikuwa yakifanywa kimya kimya na siku ya pili wote tulisherehekea Iddi kwa mashirikiano na hapakutokea ugomvi wala msukumano....hii ni imani tu lakini dini ni ile ile”,alisisitiza Alhaj Karume.

Kutokana na hali hiyo, Rais Karume alisema kuwa hakuna haja ya kugombana miongoni mwa Waislamu na badala yake Afisi ya Mufti inatakiwa kutoa elimu na taaluma kwa Waislamu na wale wote wenye kufuata njia hiyo.

Katika hotuba yake, Alhaj Karume alipongeza kazi nzuri zinazoendelea kufanywa na Afisi ya Mufti ikiwemo kutoa elimu, mawaidha na taaluma na kuitaka afisi hiyo kuendelea kufanya hivyo kwani kuna baadhi ya watu hufanya mambo kwa vile hawaelewi lakini wakipata elimu huelewa. Pia, Dk. Karume alisisitiza kuwa pongezi hizo zichukuliwe na afisi hiyo kama changamoto za kufanya vizuri zaidi.

Aidha, aliitaka Afisi hiyo kusimamia vizuri masuala ya mirathi kwa kuwapa haki zao mayatima,vizuka na watoto wa kike.

Sambamba na hayo, Rais Karume aliitaka afisi hiyo kuendeleza mahusiano na maelewano na dini nyengine hapa nchini na kuitaka Afisi ya Mufti kusimamia hilo na kutosubiri hadi kutokea tatizo, licha ya kuwa historia inaeleza kuwa halijawahi kutokea tatizo lolote la kidini hapa Zanzibar.

Alieleza kuwa mahusiano mazuri ya kidini yapo hapa Zanzibar katika siku za sikukuu hata wakati wa Mwezi mtukufu wa Ramadhani na hayo ndiyo yaliofanya kuendelea kuwepo mshikamano wa kidini hapa nchini na kusisitiza kuwa afisi hiyo iwe ni macho ya kuona hayo yanatekelezwa kwa kuzidisha mashirikiano zaidi.

Rais Karume alitoa shukurani kwa Mufti Mkuu wa Oman kwa kusimamia kupatikana fedha za ujenzi wa jengo la afisi hiyo hatua ambayo ilitokana na muwaliko alioutoa kwa Mufti Mkuu wa Zanzinar kutembelea nchi hiyo na hatimae kujengwa jengo hilo.

Alisema kuwa watu wa Oman wanahistoria kubwa na wananchi wa Zanzibar na kuwa na utamaduni wa kushirikiana, kutembeleana na hata kuishi pamoja na kusifu maelewano hayo yaliopo.

Alitoa shukurani kwa wananchi wa Omani na Mfalme Qaboos kwa mashirikiano na uhusiano na kuwataka waendelee kupata amani.

Mufti Mkuu wa Oman, Sheikh Ahmed Alkhaliyl alisema kuwa uhusiano wa Oman na Zanzibar ni wa kihistoria na kueleza kuwa Zanzibar ni nchi tukufu na chimbuko la elimu ya dini katika ukanda wa nchi za Afrika Mashariki hali ambayo imemvutia zaidi kusaidia ujenzi wa afisi hiyo.

Mufti Mkuu wa Wazanzibar Sheikh Harith bin Khelef Khamis alitoa shukurani kwa Mufti wa Oman na wananchi wake wote na kutaka uhusiano uliopo uzidi kuendelea kwa manufaa ya nchi mbili hizo.

Mapema Katibu Mkuu wa Wizara ya Nchi Afisi ya Rais Katiba na Utawala Bora, Mahadhi Juma alisema kuwa ujenzi wa jengo hilo ulianza Mei 6, mwaka 2006 chini ya Kampuni ya Mazrui Building Contractors ya Zanzibar chini ya ushauri wa Al-Habibi Consultant kutoka Dar-es-Salaam ambao umegharimu jumla ya Riali 65,000 sawa na dola 170,000 za Kimarekani.

Alisema kuwa Serikali kwa upande wake imechangia shilingi milioni 48 ambazo zimetumika kwa ujenzi wa uzio ili kuiweka afisi katika hali ya usalama na inayovutia zaidi.

Katibu Mkuu huyo, alisema kuwa jengo hilo lina sehemu kubwa ya mapokezi, afisi ya walinzi, vyumba viwili vikubwa vya afisi kwa ajili ya Mufti Mkuu na Katibu wa Mufti, chumba cha kusalia kina mama, jiko, ukumbi wa mikutano unaweza kuchukua watu kati ya 35 hadi 45 na afisi 7 za maafisa wa afisi hiyo pamoja na sehemu nyenginezo.

Alieleza kuwa jengo hilo limejengwa katika hali ambayo inaruhusu kuongezwa ghorofa moja juu iwapo mahitaji yatatokea na hali itaruhusu.

Katika uzinduzi huo viongozi mbali mbali wa dini na serikali walihudhuria.


Habari kwa hisani ya Rajab Mkasaba wa Ikulu Zanzibar.
Uchunguzi wa kina uliofanywa na gazeti hili umebaini kwamba, mademu wengi wamekuwa wakiingia mkenge kwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wasanii hatimaye kupachikwa ujauzito na kuachwa solemba.

Miongoni mwa akinadada waliokumbwa na adha hiyo ni Jamila Mbwana aliyezalishwa kisha kutelekezwa na msanii wa muziki wa kizazi kipya Mheshimiwa Temba.

Jamila alisema kuwa, awali uhusiano wake na msanii huyo ulikuwa bomba, lakini baada ya kuzalishwa penzi lilipungua ambapo ‘mchizi’ aliamua kumwaga na kumuoa msichana mwingine.

“Achilia mbali suala la kuniacha na kuoa mwanamke mwingine, lakini kimsingi amekuwa hamlei mwane ipasavyo, kwa asilimia kubwa nimekuwa nikimlea mtoto mwenyewe,” anaeleza Jamila.

Hata hivyo, Temba ambaye sasa hivi ameoa mwanamke mwingine mara kwa mara amekuwa akikanusha kumtelekeza mtoto wake na kueleza kuwa, bado anaendelea kumhudumia.

Mwingine ni msanii wa zamani wa Kaole aitwaye Lilian ambaye amezalishwa na msanii mwenzake Tuesday Kihangala kabla ya kutelekezwa na kula msoto na mwanae.

Lilian pia analalamikia msaada mdogo anaoupata kutoka kwa Chuzi ambaye sasa hivi anajulikana kama ‘mzee wa totoz’.

Msanii Aboubakar Katwila ‘Q-Chiller’ naye anadaiwa kumtelekeza mtoto wake aliyezaa na binti aitwaye Shaha Juma.

Shaha katika mahojiano na gazeti hili alieleza kuwa, mzazi mwezake huyo amekuwa akisuasua katika kumpatia mahitaji muhimu mtoto wake huku akidaiwa kujiachia na mwanamke mwingine nchini Kenya.

Q-Chiller hakuweza kupatikana mara moja kuzungumzia shutuma hizo kwani kwasasa yuko nhini Kenya kwa shughuli zake za kimuziki.

Wengine wanaodaiwa kutelekeza watoto wao ni pamoja na msanii Mohammed Mwikogi ‘Frank’ aliyezaa na binti aliyetajwa kwa jina moja la Amina, mwanasoka Mrisho Ngassa anayedaiwa kumtelekeza mkewe na mtoto huko Mwanza na kuoa mwanamke mwingine.

Hata hivyo, sababu za baadhi ya mastaa kuwapa ujauzito mabinti kisha kuwaacha zimetajwa kuchangiwa na umaarufu ambapo wahusika hufikia kipindi cha kuwaona ‘malava’ wao wa nyuma kama ‘zilipendwa’.

Akiongea na Gazeti hili mmoja wa wazazi aliyejitambulisha kwa jina la Bi. Aisha Mzee, ambaye binti yake alizalishwa na kutelekezwa na msanii wa filamu (Jina kapuni) alisema kuwa, wengi wa wasanii hao huanzisha uhusiano na mabinti wa watu kwa ahadi ya kuwaoa, lakini umaarufu unapoongezeka, huwaacha solemba na kuoa wanawake wengine.

“Binti yangu kama unavyomuona amekuwa na msanii yule tangu unaanza mambo ya uigizaji, enzi hizo alikuwa hata kuvaa hajui lakini sasa hivi amekuwa maarufu anaona hastahili kuwa na msichana kama mwanangu.

“Kibaya zaidi ni kwamba amemtelekeza baada ya kumzalisha na sasa anapata tabu na mtoto, mimi namuachia Mungu,”alisema mama huyo.

Aidha, mama huyo aliwatahadharisha wasichana kuwa makini na hawa wanaojiita wasanii kwani wengi wao ni waongo, matapeli wa mapenzi na wachafuzi wanaoweza kuyaharibu maisha yao.

Kama umetelekezwa na Supastaa, kigogo yeyote au unamjua staa aliyetelekeza mtoto cheki na sisi kwa no 0716-007373- 0755261367
Kutoka ndani ya sanaa ya muziki wa Injili, msanii Flora Mbasha ameiambia safu hii kwamba, anatarajia kuzindua albamu mpya ya video za nyimbo zake yenye jina la ‘Furaha yako’, siku ya Sikukuu ya Pasaka ikiwa ni zawadi kwa wapenzi wa kazi zake.

Staa huyo wa Injili alisema kuwa, sehemu kubwa ya maandalizi ya uzinduzi huo imeshakamilika na siku chache zijazo atalitaja eneo la tukio itakapofanyika shughuli hiyo.

“Nawaomba wapenzi wa nyimbo zangu na muziki wa Injili kwa ujumla wasikose kununua albamu hiyo ya video pamoja na ‘audio’ yake ili wapate kusikia maneno mazuri ya kumtukuza Mungu niliyoongea ndani ya kazi hizo,” alisema Mbasha ambaye bado anaendelea kutamba na nyimbo zake mbalimbali katika fani hiyo.

Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya a.k.a bongofleva Juma Nature ambaye pia ni kiongozi wa kundi la TMK Wanaume Halisi lenye makazi yake Temeke jijini Dar, anatarajia kuzindua albamu yake machi 20 katika ukumbi wa Diamond jubilee jijini Dar.

Juma Nature ambaye inaelezwa kuwa ni msanii pekee aliyewahi kuvunja rekodi ya kujaza ukumbi wa Diamond jubilee kuliko msanii yeyote wa hapa yumbani, anazindua albamu yake itakayoitwa TUGAWANE UMASKINI yenye jumla ya nyimbo 11.

Albamu hiyo ambayo kwa sasa iko sokoni,imesheheni ladha mbalimbali ili kuifanya iwe bora na yenye kukubalika kwa kiwango kikubwa,aidha baadhi ya nyimbo zilizomo humo ni siku ya wiki,ulevi,tugawane umaskini,Afrika no 1,kukaa nyumbani,Lakavunda,mgeni wa nani na nyinginezo. Albam alizowahi kuzindua ni NIni Chanzo,Ugari,Ubin adam kazi,History,na sasa hii ya Tugawane umaskini.

Kwa yeyote atakae hitaji nakala/albamu ya TUGAWANE UMASKINI aidha CD ama TAPE wala usisite.

Wasiliana nao kwa namba hizo hapo chini.
0787 878108
0713 424943
no image
Pan-African sportscaster SuperSport has confirmed that it is today in a position to announce that it has secured, amongst others, the exclusive pay television rights to broadcast the much-anticipated 2010 FIFA Soccer World Cup, live across sub-Saharan Africa, excluding South Africa.

The news means that DStv audiences in over 40 countries across the continent will see all the goals, drama, action and excitement from the very first FIFA World Cup to ever be played in Africa . The biggest soccer tournament in the world has always drawn widespread attention from African fans but with the tournament making its African debut that attention is soaring.

Given the African interest in the event, SuperSport International CEO Imtiaz Patel was delighted when announcing the deal, saying that it was in keeping with SuperSport’s legacy of continually bringing viewers across the continent major international sports programming.

"To now be able to bring this prestigious event to Africa the first time it's happening on the continent, is indeed a special and proud moment. Viewers can look forward to quality coverage and we already have plans in place to compliment the live action with superb supplementary product."

“FIFA’s approach has always been to ensure that images of our events will be seen by the widest possible audience. We are therefore very pleased to be working with such an experienced partner as SuperSport in extending the frontiers of football coverage across 42 African countries supplementary to the provided free TV coverage in the region”, says FIFA Secretary General Jérome Valcke.

Running for a full month from June 11 to July 11, the 2010 FIFA World Cup will see 32 nations, including for the first time with the automatically qualified hosts South Africa 6 African teams, contesting 64 matches with one country earning the right to call itself world champions.

For MultiChoice Africa President Eben Greyling, the winners have already been crowned. “DStv soccer fans tuning into this incredible sporting festival will ultimately be the big winners. SuperSport creates several premier channels for our DStv service and we’re confident that with their world-class technical expertise they will fully showcase this historic African event. DStv remains at the forefront of screening major global sporting events and following our coverage of the 2008 Beijing Olympic Games, the next major event is the 2010 FIFA World Cup which our audiences can look forward to seeing on our service.”

First televised in 1954, the FIFA World Cup is arguably the most widely viewed and followed sporting event in the world. The cumulative audience of the 2006 FIFA World Cup, including all of the matches, is estimated to be 26.29 billion with 715.1 million individuals watching the final match of this tournament (a ninth of the entire population of the planet). Played every four years since 1930, with just two interruptions due to World War 2, the FIFA World Cup draws some of the brightest talents in the football world and provides a platform for some of the most entertaining and memorable soccer ever played.

Meanwhile SuperSport has also confirmed that it can today announce that it has secured the exclusive pay television rights for sub-Saharan Africa (excluding South Africa) to screen the upcoming 2009 FIFA Confederations Cup 2009.

Furaha Samalu,
Marketing Manager
Multichoice Tanzania .
no image
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Amani Abeid Karume amesema kuwa nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania ina mambo mengi ya kujifunza kutoka China kutokana na nchi hiyo kupiga hatua kiuchumi, kisayansi na kiteknolojia.

Rais Karume aliyasema hayo leo wakati alipokuwa na mahojiano na Waandishi wa habari kutoka vyombo vya Habari vya China wanaofanya kazi zao katika nchi mbali mbali duniani, mahojiano hayo yaliofanyika Ikulu mjini Zanzibar.

Katika maelezo yake Rais Karume alisema kuwa Tanzania ikiwemo Zanzibar ni miongoni mwa nchi zinazoendelea hivyo zina mengi ya kujifunza kutoka China kutokana na nchi hiyo kuwa na maendeleo makubwa.

Alisema kuwa hatua ya maendeleo iliyofikiwa nchini China ni ya kupigiwa mfano na kuigwa na nchi nyenginezo zikiwemo nchi zinazoendelea na kusisitiza kuwa mbali na hatua hiyo nchi hiyo pia imeweza kujenga mahusiano na ushirikiano mwema na nchi mbali mbali za Afrika ikiwemo Tanzania.

Rais Karume alisema kuwa Zanzibar na China zina uhusiano wa kihistoria ambao umezidi kuimarishwa hadi hii leo na kueleza kuwa ujio wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China chini Tanzania Mhe, Hu Jintao mwishoni mwa wiki hii kutasaidia kuimarisha uhusiano na ushirikiano huo uliopo.

Alisema kuwa China imeweza kuisaidia Zanzibar katika sekta mbali mbali za maendeleo ikiwemo afya, elimu, kilimo,viwanda, michezo, habari na msaada wa lami kwa ajili ya ujenzi wa barabara pamoja na misaada mbali mbali ambayo imeweza kusaidia shughuli za kiuchumi,kijamii na kimaendeleo.

Rais Karume alisema kuwa kwa upande wa afya China imesaidia kuleta madaktari pamoja na vifaa vya hospitali na vya mafunzo pamoja na madawa na kueleza kuwa wananchi wa Zanzibar wamekuwa wakisifu huduma zinazotolewa na madaktari kutoka China.

‘China ina uhusiano mzuri tena wa kihistoria na Zanzibar hali ambayo imeweza kuimarishwa hadi hii leo na kwa kweli China imeweza kuisaidia Zanzibar katika kuimarisha sekta mbali mbali za maendeleo hapa nchini”,alisema Rais Karume.

Aidha, Rais Karume alisema kuwa China imeweza kusaidia sekta ya kilimo kwa kiasi kikubwa pamoja na sekta ya michezo kwa kujenga uwanja wa Amani ambao kwa hivi sasa unafanyiwa ukarabati mkubwa kwa msaada wa nchi ya China.

Akieleza kuhusu sekta ya habari alisema kuwa China imeweza ksuaidia ujenzi na Studio na mitambo ya redio ya Sauti na Tanzania Zanzibar (STZ), pamoja na Kituo cha Televisheni cha Zanzibar (TVZ) na kusema kuwa China imekuwa ikitoa msaada mkubwa wa masomo kwa Wazanzibari.

Pamoja na hayo, Rais Karume alisema kuwa Zanzibar hivi sasa imekuwa ikichukua juhudi za makusudi katika kuhakikisha athari za kiuchumi zilizoikumba dunia hazileti madhara hapa nchini kwa kuimarisha huduma za kimaendeleo zilizomo nchini.

Rais Karume pia aliwaeleza waandishi hao wa habari kuwa Zanzibar inawakaribisha wawekezaji kutoka nchini China pamoja na wafanya biashara kuja Zanzibar kuekeza na kushirikiana na wafanyabiashara waliopo nchini ili kuimarisha sekta ya biashara na kuongeza kuwa Serikali imewawekea mazingira mazuri waekezaji na wafanyabiashara.

“Itakuwa ni jambo zuri iwapo patakuwa na mashirikiano katika sekta za biashara na uwekezaji ambapo wafanyabiasahara na waekezaji watakuja kufanya shughuli zao hapa Zanzibar na wa hapa nao watakwenda China kufanya shughuli zao”,alisema Dk. Karume.

Nao waandishi hao wakiwemo kutoka vyombo vya habari vya ‘Guangming Daily Media Group’, ‘Economic Daily’ na ‘People’s Daily’ kutoka China walitoa shukurani kwa Rais Karume kwa makaribisho yake pamoja na kusifu hatua za maendeleo zilizofikiwa chini ya uongozi wake sanjari na mahusiano na mashirikiano yaliopo kati ya China na Tanzania ikiwemo Zanzibar.


Habari kwa hisani ya Rajab Mkasaba wa Ikulu ZANZIBAR.
Baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu mwanadada Miriam Mhembelo sasa ameanza kutamba na video yake iliyoanza kurushwa katika stesheni za tevevion mbali mbali.

Akizungumza na HABARI NA MATUKIO mwanadada huyo alisema kuwa ameamua kuachilia video yake ya "Nafsi yangu" na imekuwa ikifanya vyema katika chat za video za injili.

“Namshukuru Mungu kwa kuweza kunifanikisha kutengeneza video yangu ambayo naona siyo mbaya na imekuwa ikifanya vyema jambo linalonipa nguvu ya kuendelea mbele,” alisema Miriam.

"Kitu kikubwa ninachomshukuru Mungu ni jinsi anavyoweza kunisaidia kupata nafasi ambapo bado namalizia albamu yangu ninayotarajia kuiingiza sokoni hivi karibuni.
Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Barazala Mapinduzi Mhe Dk Amani Abeid Karume, akisalimiana na Alhaj khamis Dadi Mbulu,Mwenyekiti wa CCM Mkoa Mtwara, Kiongozi wa Wenyeviti wa CCM Mikoa mbali mbali ya Tanzania Bara, na Makatibu,walioalikwa katika sherehe za Miaka 45 ya Mapinduzi, (wa pili kulia) Azim S Premji, Mkoa wa Kigoma, na Onesmo Nangohe,Mkoa wa Arusha, Wenyeviti hao walifika kusalimiana na Rais Ikulu Mjini Zanzibar.

Picha na Ramadhan Othman Ikulu
Hii ni taarifa rasmi kuwa nimepanga kutoa wimbo wangu mpya unaitwa "MSIACHE KUONGEA" na nimemshirikisha Lady JD.

Wimbo huu unazungumzia watu wasio na kazi wanaoshinda kuchukia wenzao wahangaikaji, yeyote ambaye anadhani huo ni wimbo wake ameibiwa ama aliuandika yeye na anahisi kudhulumiwa, nachukua fursa hii kumuomba ajitokeze kutoa madai yake mapema kabla nanga haijang'oka.

Asanteni kwa kunisikiliza na kwakunisoma.

Mwana F.A. a.k.a Binamu

Zaidi tembelea www.djchoka.blogspot.com
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akifurahia jambo katika mazungumzo kati yake na balozi wa Uingereza nchini, Philip P. (kushoto) na Padri Patick Shanahan kutoka Uingereza baada ya kufungua Warsha ya Wadau ya Kuandaa Mpango Mkakati wa Kusaidia Watoto Wanaishi Mitaani iliyofanyika kwenye hoteli ya Giraffe Ocean View jijini Dar es salaam, Januari 19, 2009.
Waziri Mkuu, Mizengo akifungua Warsha ya Wadau ya Kuandaa Mpango Mkakati wa Kusaidia Watoto Wanaoishi Mitaani huku akiwa amezungukwa na watoto hao kwenye hoteli ya Giraffe Ocean View ya jijini Dar es salaam Januari 19,2009.

(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Wanafunzi wa chuo kikuu sehemu ya Mlimani(UDSM) leo mchana wamekamatwana na kutiwa mbaroni baada ya kuandamana kinyume cha sheria wakiwa na mabango yakuushutumu uongozi wa chuo hicho.
Habari na matukio wakiwa kwenye eneo la tukio walishuhudia vurugu kubwa baina ya wanafunzi na askari wa kutuliza ghasia FFU kwenye eneo hilo.

Kwa ujumla hali ni tete katika eneo hilo mpaka Habari na matukio inaondoka ilishuhudia jumla ya wanafunzi watano wakikamatwa na kutiwa ndani ya gari la askari hao na kuondoka nao eneo hilo kwa kuwapeleka kituo cha polisi cha Mlimani.

Katika mabango hayo kama yalivyosomeka mengi yalikuwa yakiwalaumu viongozi wa chuo hicho kwa kushinikiza kuwarudisha Chuoni hapo bila masharti wanafunzi hao, ikiwa ni pamoja na kushinikiza Mkuu wa chuo hicho Prof Mukandala kujiuzulu.

Naye Rais wa DARUSO akiongea kwa niaba ya wenzake walisema wataendelea kubeba mabango mpaka wahakikishe watoto wa Maskini nao wanapata haki ya kuendelea na Masomo.Naye Mkuu wa Chuo hicho Prof Mukandala alisema uongozi wa chuo umeongeza siku badala ya mwisho wa masharti ambao ulikuwa leo badala yake umesogezwa mpaka tarehe 29 ya mwezi huu.

Wadau mnasemaje kuhusu sakata hili la wanafunzi hawa....??Nini kifanyike....??

Yule mchekeshaji maarufu Bongo na bingwa wa kuiga sauti za watu maarufu hapa Bongo na sehemu nyinginezo duniani Steve Mengere maarufu kwa jina la Stive Nyerere, anasema mwaka mpya wa 2009 ni mwaka wa mabadiliko kwake na anasema ni vyema kwa wasanii wenzake kuboresha kila kitu katika maisha kuanzia katika kazi za usanii, maisha, tabia na mavazi.Stive aliyasema hayo wakati akiongea na habari na matukio katika kukitambulisha kipindi chake kipya ambacho kitaanza kurushwa hivi karibuni katika Luninga kupitia kituo cha TBC.
"Nataka nifanye mambo kimataifa zaidi ndio maana nimeamua kuanzisha show yangu ambayo nina uhakika itakuwa babkubwa, wapenzi na washabiki wangu watulie tu mambo mazuri kibao yapo kwa ajili yenu." alisema Nyerere.Jina la Stive Nyerere limetokana na sanaa yake kwa kuwa alianza usanii kwa kuingiza sauti ya Baba wa Taifa ,Mwalimu Julius Nyerere.
Meneja wa Steve ambaye ni mmiliki wa kampuni ya kurekodi movie na vipindi bwana Hartman Mbilinyi anasema kila kitu kiko tayari kilichobaki ni kuanza kuonekana kwa kipindi hicho.Zaidi ya Nyerere Steve pia ana uwezo wa kuwaigiza watu maarufu kama Bin Laden, Rais wa Marekani Bwana George Bush, na wengine wengi.

This year is the fifth anniversary of The Greatest Race on Earth (GROE), the unique marathon team relay series created and sponsored by Standard Chartered, which encompasses four of the world’s most gruelling marathons – Nairobi, Singapore, Mumbai and Hong Kong.

Each year GROE transforms the traditionally individual sport of marathon running into a team event. The challenging team relay sees international men’s and women’s teams battling it out for a share of the US$ 1 million prize fund, one of the largest guaranteed prize pools in world athletics.

Competitors will face some of the most challenging environments in the world – including the high altitude of Nairobi, the humidity in Singapore, the heat of Mumbai and the uphill terrain in Hong Kong:
The ‘highest race,’ at over 1,600m, in Nairobi – 26 October 2008
The ‘island race’ around Singapore – 7 December 2008
The ‘historic race’ through Mumbai – 18 January 2009
The ‘harbour race’ across Hong Kong – 8 February 2009

Partnership, teamwork, trust and courage, all of which are Standard Chartered core values, will be key factors in determining the winners.

Nations Challenge:
Some of the world’s quickest marathon athletes compete in teams of four, running one marathon each – with the singular goal of working together to achieve a faster cumulative time than their rivals and gaining a significant slice of the prize pool.

The 2008/09 series sees a total of 36 Nations Challenges taking part (23 men’s and 13 women’s teams). The Nations Challenges will be split into three regions – Africa, South Asia and North East Asia and Rest of The World. The fastest team in each of the three regions will win US$ 80,000, with US$ 50,000 for second place, and US $30,000 for third.

In addition to the above challenges Standard Chartered will be providing a series of financial prizes for the Performance and Most Improved Awards and there will be a special bonus for ‘Beating the Series Record’.

Standard Chartered Staff Challenge:
Staff teams from across Standard Chartered’s network will also compete in the relay series but over half marathon courses. The team with the lowest cumulative time after all four races will be crowned winners. Standard Chartered staff will run to raise awareness and funds for this year’s nominated race beneficiary Seeing is Believing.

Seeing is Believing (SiB):
Seeing is Believing (SiB) is a global initiative to help tackle avoidable blindness, and is a partnership between Standard Chartered Bank and the International Agency for Prevention of Blindness (IAPB). IAPB is the leading umbrella organisation for NGOs working in the field of eye care. Together with the World Health Organisation, it launched the ‘Vision 2020 – The Right to Sight’, a global campaign to eliminate avoidable blindness by 2020.

To date, Seeing is Believing has raised over US$ 17 million for blindness initiatives and plans to invest a further US$ 20 million by 2014. Seeing is Believing is the single largest contributor
to the development of Vision 2020 programmes through IAPB. Full details of SiB can be found at www.thegreatestrace.com

As part of the Seeing is Believing programme, Standard Chartered Bank pledges to match all donations until the target of US$ 20 million is reached.

Standard Chartered – leading the way in Asia, Africa and the Middle East
Standard Chartered PLC, listed on both London and Hong Kong stock exchanges, ranks among the top 25 companies in the FTSE-100 by market capitalisation. The London-headquartered Group has operated for over 150 years in some of the world's most dynamic markets, leading the way in Asia, Africa and the Middle East. Its income and profits have more than doubled over the last five years primarily as a result of organic growth and supplemented by acquisitions.

Standard Chartered aspires to be the best international bank for its customers across its markets. The Bank derives more than 90 per cent of its operating income and profits from Asia, Africa and the Middle East, generated from its Wholesale and Consumer Banking businesses. The Group has around 1,750 branches and outlets located in over 70 countries. The extraordinary growth of its markets and businesses creates exciting and challenging international career opportunities.

Leading by example to be the right partner for its stakeholders, the Group is committed to building a sustainable business over the long term and is trusted worldwide for upholding high standards of corporate governance, social responsibility, environmental protection and employee diversity. It employs 75,000 people, nearly half of whom are women. The Group's employees are of 115 nationalities, of which 60 are represented among senior management.

For more information, please visit: www.standardchartered.com .