Hii ni taarifa rasmi kuwa nimepanga kutoa wimbo wangu mpya unaitwa "MSIACHE KUONGEA" na nimemshirikisha Lady JD.

Wimbo huu unazungumzia watu wasio na kazi wanaoshinda kuchukia wenzao wahangaikaji, yeyote ambaye anadhani huo ni wimbo wake ameibiwa ama aliuandika yeye na anahisi kudhulumiwa, nachukua fursa hii kumuomba ajitokeze kutoa madai yake mapema kabla nanga haijang'oka.

Asanteni kwa kunisikiliza na kwakunisoma.

Mwana F.A. a.k.a Binamu

Zaidi tembelea www.djchoka.blogspot.com
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: