Articles by "UCHUMI"
Showing posts with label UCHUMI. Show all posts
MKUU wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungumza wakati wa halfa ya kugawa zawadi ya Sofa seti kwa mshindi katika kampeni yao ya Tisha na Tembo Kadi iliyokwenda sambamba na ugawaji wa Riflect kwa Waendesha Bodaboda iliyofanyika kwenye viwanja vya Tangamano Jijini Tanga

MKUU wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungumza wakati wa halfa ya kugawa zawadi ya Sofa seti kwa mshindi katika kampeni yao ya Tisha na Tembo Kadi iliyokwenda sambamba na ugawaji wa Riflect kwa Waendesha Bodaboda iliyofanyika kwenye viwanja vya Tangamano Jijini Tanga

MKUU wa wilaya ya Tanga James Kaji akizungumza wakati wa halfa hiyo



MKUU wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba kulia akigawa riflect kwa Mwenyekiti wa Waendesha Bodaboda Mkoa wa Tanga katikati ni Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji na kulia ni Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Kaskazini Cosmas Sadat

MKUU wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba kushoto akimkabidhi seti ya sofa msindi a Sofa seti kwa mshindi katika kampeni yao ya Tisha na Tembo Kadi inayoendeshwa na Benki hiyo kulia ni Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Kaskazini Cosmas Sadat
Na Oscar Assenga, TANGA.

BENKI ya CRDB imetangaza neema kwa wafanyabiashara wa bodaboda pamoja na bajaji kwamba hivi sasa hauitajiki kuwa na nyumba,gesti wala shamba kama dhamana ili kuweza kupata mkopo wa bodaboda.

Neema hiyo imetangazwa na Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Kaskazini Cosmas Sadat wakati wa halfa ya kugawa zawadi ya Sofa seti kwa mshindi katika kampeni yao ya Tisha na Tembo Kadi iliyokwenda sambamba na ugawaji wa Riflect kwa Waendesha Bodaboda”,

Alisema kwamba wanachotakiwa ni kufika kwenye tawi lolote la benki hiyo na kumueleza Meneja wamefika kuchukukua bodaboda na dhamana yao na Bajaji ni ile kadi ya hicho kifaa.

Aidha alisema kwamba wameweza kutoa mikopo hiyo ili kuwaepusha wananchi na mikopo kausha damu na wamewapelekea riba nafuu sana kutokana na ombi la mkuu wa mkoa wa Tanga Waziri Kindamba.

“Bodaboda na waendesha bajaji wanasahauliwa sana lakini sisi kama benki ya CRDB tumeamua kuwawezesha wafanyabaishara wa bodaboda na bajaji hauitajiki kuwa na nyumba,sham,ba wale gesti “Alisema

Meneja huyo alisema kwamba benki hiyo wamejiwekea malengo ya kushirikiana katika kuinua uchumi wa nchi kwa kushirikiana na makundi yote ya wajasiriamali wakubwa,wa kati na wachini kabisa.

Alisema kwa sababu wanaamini kanzuri ya ijumaa inaandaliwa Alhamisi na wafanyabsiahara wakubwa wanaandaliwa tokea chini hivyo leo wanakwenda ramsi na mambo matatu ikiwa ni kutimiza agizo la RC Kindamba kushirikisha jamii ya wafanyabiashara wadogo wadogo katika suala la mitaji na biashara kwa ujumla.

Awali akizungumza katika halfa hiyo Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba aliishukuru Benki hiyo kwa kuamua kuwezesha makundi hayo huku akitoa wito kwa watakao kupata mikopo wakaitumie kwa madhumuni yaliyokusudiwa ili waweze kufanya marejeshe kwa wakati.

Kindamba alisema kwamba pamoja na hayo lazima waendelee kutunza uaminifu ambao Benki ya CRDB wamewapa kwa kuhakikisha wanarejesha mkopo huo kwa wakati ili kutoa fursa kwa wengine kunufaika nao.

“Hasa wakina baba usije kupewa fedha ukaenda kuongea jiko watu wa Pwani tunajua wenyewe…fedha hiii ikatumike kwenye madhumuni yaliyokusudiwa”Alisema

Naye kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji aliomba wafanyabiashara ndogo ndogo na maafisa usafirishaji waweze kutumia mikopo hiyo ili kuweza kujikwamua

●Ikiwa ni mojawapo ya eneo lililopendekezwa zaidi kuwa thabiti na muhimu kwa shughuli za uwekezaji barani, Tanzania inajiandaa kuwa mwenyeji wa mkutano wa tano wa mwaka wa kimataifa wa Tanzania Energy Cooperation Summit (TECS) utaofanyika kuanzia Januari 31 mpaka Februari mosi, 2024 jijini Arusha, nyumbani kwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC). 

---

Dar es Salaam - Desemba 22, 2023. Wawekezaji kutoka sekta mbalimbali, fedha na serikali zitakutana kuonyesha uwezo ilionao Tanzania.

Uwezo ambao unaonyeshwa na nchi ambayo kwa sasa imeorodheshwa kuwa ya tatu kusini mwa Jangwa la Sahara kwa uwekezaji siku za mbeleni, ambapo inatarajiwa kuona ukuaji wa Pato la Taifa kwa 6% ifikapo 2025, huku ikishuhudia mamia ya mamilioni, kama sio mabilioni, ya uwekezaji wa dola, unaolenga kuelekezwa kwenye miundombinu, umeme wa maji, gesi asilia (LNG) na miradi ya nishati ya jua katika miaka ya hivi karibuni. 

Ikiwa imeorodheshwa na KPMG ikiwa nyuma ya nchi za Afrika ya Kusini na Nigeria, Tanzania imejithibitishia hadhi yake yanapokuja masuala ya biashara na uwekezaji. 

Taifa lilitajwa kwa eneo lake la kimkakati mashariki mwa bara la Afrika, wingi wa maliasili, na ongezeko la uwekezaji hivi karibuni, haswa katika sekta ya nishati. Kiwanda cha kwanza cha umeme wa jua cha 50MW kwenye gridi ya taifa, uwekezaji wa dola za Marekani milioni 300 katika nishati ya maji, mradi wa gesi asilia wa dola bilioni 42 ulioanzishwa na Shell, Equinor na Exxon Mobil, na takribani dola za Marekani bilioni 7 zilizoingizwa kwenye miundombinu, inathibitisha mvuto wake barani Afrika na kimataifa.

Ukiwa umeratibiwa na EnergyNet, mkutano wa kimataifa wa TECS24 hautoainisha mafanikio haya ya kujivunia pekee bali itaangazia fursa zijazo za biashara na miradi ya uzalishaji inayotarajiwa kubadilisha nchi na ukanda huu zaidi. Changamoto zinazohusiana na fedha na dhamana pia zitajadiliwa, ili kuchochea ari zaidi ya majadiliano na kuhakikisha sekta ya umeme nchini inaendelea kuimarika zaidi.

Pamoja na wawekezaji wakubwa, wadau watakaohudhuria ni pamoja na mawaziri wa kitaifa kutoka Tanzania, Malawi, na Ethiopia, pamoja na viongozi wa makampuni ya utoaji huduma ya kitaifa, ikiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO wa Tanzania, Gissima Nyamo-Hanga. Wasemaji kutoka Electricidade de Moçambique (EDM) na ZESCO ya Zambia pia watakuwepo. Wao, pamoja na wawakilishi kutoka sekta za umma na binafsi, wakurugenzi kutoka taasisi za kifedha - ikiwa ni pamoja na AfDB, BII, World Bank Group na ATIDI - na mashirika ya kikanda, wote watakuwepo Arusha, kwa ajili ya mkutano wa biashara wa hadhi ya juu wa aina yake.

Kwa kuzingatia nafasi ya Tanzania kama mhimili wa nishati kikanda, mada zitakazojadiliwa ni pamoja na mtazamo wa kiuchumi wa Tanzania na uwezo wa maendeleo ya nishati, pamoja na kupanga njia bora ya kujenga soko la umeme la kikanda. Ushirikiano wa sekta za umma na binafsi katika miradi ya usafirishaji pia utakuwa kwenye ajenda, pamoja na wakurugenzi kutoka taasisi za kifedha, utawala na kanuni, na nafasi muhimu ya nishati mbadala. Washiriki watapewa fursa ya kutoa mawazo kuhusu kutengeneza uunganisho bora wa kikanda, mifumo imara zaidi kwa biashara na uwekezaji, na hatimaye kuunda ramani ya ufikiaji wa nishati kikanda kwa siku za usoni. 

"Tanzania imejitengenezea nafasi muhimu kwa biashara barani. Kwa kuwa na uhusiano baina ya kusini na mashariki na pia ulimwenguni kote, nchi hii siku zote imekuwa na uwezo wa kuwa mwanzilishi wa ukuaji wa viwanda - na sasa tunashuhudia jinsi adhma hii itakavyotimizwa. Hivyo nina shauku kubwa kuonyesha ukuaji wa Tanzania kuhakikisha fursa na kasi hii inaendelea," alisema Simon Gosling, Mkurugenzi Mtendaji, EnergyNet. 

Aliongeza, "Pia tunafurahi kuandaa mkutano huu Arusha, ukitoa muda na nafasi kwa kila mtu kujadili kwa kina masuala muhimu zaidi kuhus sekta mbalimbali."

"Tanzania akiwa mmojawapo wa nchi waanzilishi wa Jumuiya yetu, tuna nia ya dhati kuiunga mkono zaidi kusaidia malengo yake kwenye sekta ya nishati. Tukiendeleza mafanikio yaliyopatikana katika mkutano wa mwaka jana uliofanyika Dar es Salaam, tunatumaini kuwa TECS24 itatoa ufafanuzi zaidi kuhusu nafasi ya sekta binafsi katika sekta ya nishati na jinsi wakurugenzi kutoka taasisi za kifedha - hasusani watoaji wa bima na dhamana wa kikanda kama vile ATIDI - wanaweza kusaidia juhudi hizo na mabadiliko makubwa ya nishati kwa ujumla," alisema Obbie Banda, Mchambuzi na Kaimu Mratibu wa Regional Liquidity Support Facility (RLSF) katika taasisi ya African Trade and Investment Development Insurance (ATIDI).

Aleem Tharani, Mkuu mwenza wa Infrastructure Sector Group (Afrika), Bowmans na Mkuu wa Miradi, Nishati na Miundombinu (Afrika), alihitimisha: "Mkutano wa 5 wa kimataifa wa Tanzania Energy Cooperation Summit unaweka alama muhimu kwa sekta ya nishati barani Afrika. Kwa kuwaunganisha wawekezaji, taasisi za serikali na wataalamu wa sekta, tunachochea majadiliano muhimu kwa ajili ya kukuza ramani ya nishati ya Tanzania, kutoa kipaumbele kwa gesi na nishati mbadala, na kuboresha usafirishaji wa kikanda. Bowmans inajivunia kudhamini mkutano huu, ikiona umuhimu wake katika kuunda mustakabali wa nishati wa Afrika na kuzidisha ushirikiano wa umma na binafsi."  

Angalia ajenda na orodha ya wasemaji hapa https://www.tanzania-ecs.com/

Dar es Salaam 11 Desemba 2023 – Benki ya CRDB leo imekabidhiwa cheti cha viwango vya Usimamizi wa Huduma za TEHAMA cha ISO 20000-1:2018 kilichotolewa na Shirika la Viwango la Uingereza (BSI). Cheti hicho kimekabidhiwa katika hafla fupi iliyofanyika Makao Makuu ya Benki yaliyopo barabara ya Ali Hassan Mwinyi.

Akipokea cheti hicho kutoka kwa Mkurugenzi Mkaazi, na Mkuu wa Sera za Biashara na Uwekezaji Ubalozi wa Uingereza, Afisa Uendeshaji Mkuu wa Benki ya CRDB amesema cheti hicho ni ishara ya dhamira ya dhati ya Benki ya CRDB katika kuhakikisha mifumo, taratibu, na huduma za TEHAMA za benki hiyo zinakidhi ubora wa kimataifa.
Mwile alisema Benki ya CRDB imekuwa ikiwekeza katika mifumo ya kisasa na hivyo kupelekea mabadiliko makubwa katika huduma zake za TEHAMA kufikia viwango vya kimataifa. Hata hivyo mazingira ya biashara yamekuwa yakibalika kwa kasi kutokana na ukuaji wa teknolijia jambo ambalo limepelekea benki hiyo kufanya mchakato wa kuboresha viwango vyake.

“Tukitambua umuhimu wa kuwa na mifumo ya utoaji huduma iliyo na viwango bora, Benki ilifanya mchakato wa kupata cheti cha ubora wa ISO 20000 cha usimamizi wa huduma. Tulipitia mchakato mrefu uliohusisha uboreshaji wa michakato yetu ya usimamizi wa huduma za TEHAMA,” alisema Mwile.
Mwile aliongezea kuwa benki hiyo pia iliwekeza mipango ya kina ya mafunzo na uhamasishaji ili kuhakikisha wafanyakazi wanaelewa mahitaji ya viwango vya ISO 20000 na kutambua majukumu yao muhimu katika michakato ya usimamizi wa huduma za TEHAMA. Hii ilienda sambamba na kuanzishwa kwa utamaduni wa kuboreha mifumo ya TEHAMA mara kwa mara.

Akielezea faida za kupata uthibitisho wa kiwango hicho cha kimataifa cha ISO 2000, Mwile alisema kunasaidia kuchochea michakato na taratibu zinazohakikisha huduma za TEHAMA zinatolewa kwa ufanisi na kukidhi viwango vya kimataifa, hivyo kutoa uzoefu uliobora kwa wateja.

“ISO 20000 pia inakuza utamaduni wa kuboresha mara kwa mara. Cheti hiki kinatuhimiza kutathmini na kurekebisha mara kwa mara michakato yetu ya usimamizi wa huduma za TEHAMA, kuhakikisha tunaendana na mabadiliko ya mahitaji ya wateja na maendeleo ya teknolojia,” aliongezea.

Akikabidhi cheti hicho Mkurugenzi Mkaazi, na Mkuu wa Sera za Biashara na Uwekezaji Ubalozi wa Uingereza, Anna-Maria Mbwette ameipongeza Benki ya CRDB kwa cheti hicho cha ubora wa kimataifa na kusema kunaonyesha dhamira yake katika ubora, usalama na usimamizi madhubuti.

Anna-Maria alisema kupata ISO 20000 katika huduma za TEHAMA kutasaidia benki hiyo kujenga imani sit u kwa wateja wake, bali pia wawekezaji na washirika wa kimataifa kwani viwango hivyo vinatambulika na kutumika kote duniani.

Kiwango cha ubora wa ISO 2000O katika usimamizi wa huduma za TEHAMA ni mwendelezo wa jitihada za Benki ya CRDB katika kufikia viwango vya kimataifa kwani benki hiyo tayari imepata vyeti vya ubora vya ISO/IEC 27001:2013 cha usimamizi wa usalama wa taarifa, na ISO 22301:2019 cha mipango, mifumo, na michakato ya uendeshaji biashara yenye ufanisi.
Afisa Uendeshaji Mkuu Benki ya CRDB, Bruce Mwile, akipokea Cheti cha Ubora cha Usimamizi wa Huduma za TEHAMA cha ISO 20000-1:2018 kutoka kwa Mkurugenzi Mkaazi, na Mkuu wa Sera za Biashara na Uwekezaji, British High Commission, Anna-Maria Mbwette ambaye amekabidhi kwa niaba ya Shirika la Viwango la Uingereza (BSI) katika hafla fupi iliyofanyika leo 11 Desemba 2023 Makao Makuu ya Benki ya CRDB jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB, Tully Esther Mwambapa akizungumza wakati hafla fupi ya kupokea Cheti cha Ubora cha Usimamizi wa Huduma za TEHAMA cha ISO 20000-1:2018 kilichotolewa na Shirika la Viwango la Uingereza (BSI) kwa Benki ya CRDBBenki ya CRDB. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa TEHAMA Benki ya CRDB, Mwanaisha Kejo.




Mawakala wa usajili wa kampuni ya Vodacom Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa kampuni, makao makuu ya ofisi jijini Dar es Salaam. Mawakala hao waliagwa kuanza ziara ya kutembelea Afrika ya Kusini ikiwa ni jitihada iliyotambulishwa mapema mwaka huu na kampuni hiyo kuwazawadia mawakala wa usajili kutokana na utendaji bora wa kazi.

Mawakala wa usajili wa kampuni ya Vodacom Tanzania wakiwa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere tayari kwa ziara ya kutembelea Afrika ya Kusini ikiwa ni jitihada iliyotambulishwa mapema mwaka huu na kampuni hiyo kuwazawadia kutokana na utendaji bora wa kazi.

Mawakala wa usajili wa kampuni ya Vodacom Tanzania wakiwa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo tayari kwa ziara yao ya kutembelea Afrika ya Kusini ikiwa ni jitihada iliyotambulishwa mapema mwaka huu na kampuni hiyo kuwazawadia kutokana na utendaji bora wa kazi.

Mawakala wa usajili wa kampuni ya Vodacom Tanzania wakiwa katika makao makuu ya ofisi mama ya Vodacom nchini Afrika ya Kusini walipotembelea kujifunza masuala mbalimbali. Ziara hiyo ni jitihada iliyotambulishwa mapema mwaka huu na kampuni hiyo kuwazawadia kutokana na utendaji bora wa kazi.

Mawakala wa usajili wa kampuni ya Vodacom Tanzania wakimsikiliza mmojawapo wa wafanyakazi wa kampuni mama ya Vodacom nchini Afrika ya Kusini walipozuru kujifunza masuala mbalimbali. Ziara hiyo ni matokeo ya jitihada iliyotambulishwa mapema mwaka huu na kampuni hiyo kuwazawadia mawakala wa usajili kutokana na utendaji bora wa kazi.
Mawakala wa usajili wa kampuni ya Vodacom Tanzania wakiwa katika mitaa tofauti nchini Afrika ya Kusini walipozuru kujifunza masuala mbalimbali. Ziara hiyo ni matokeo ya jitihada iliyotambulishwa mapema mwaka huu na kampuni hiyo kuwazawadia mawakala wa usajili kutokana na utendaji bora wa kazi.

 Watumishi Housing Investments(WHI) inashiriki maonesho ya WIKI YA HUDUMA ZA FEDHA yanayofanyika kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha kuanza tarehe 20/11/2023 – 26/11/2023 ambapo watu mbalimbali wanajitokeza kupata elimu kuhusu uwekezaji na mambo mbalimbali yanayohusu fedha.Akizungamza katika banda la WHI Mkuu wa Kitengo cha Mauzo na Masoko WHI Bw. Raphael Mwabuponde amesema WHI inatumia nafasi hii kutoa elimu kuhusu huduma zitolewazo na Watumishi Housing Investments hasa elimu ya uwekezaji katika mfuko wa uwekezaji wa pamoja (FAIDA FUND) pamoja na mradi wao mpya unaotegemea kuanza hivi karibuni wa Mikocheni Apartments.

Bw. Raphael Mwabuponde amewaelezea watu mbalimbali kuhusu faida za mfuko wa Faida pamoja na jinsi ya kujiunga na huu mfuko kwa kupiga *152*00# then 1. Malipo na 6. WhI. Na kwa wale wanaotumia simu janja wanaweza jiunga kwa kutumia app ya “wekezawhi”

Vile vile Bw. Raphael Mwabuponde amesema kuwa tayari maombi ya kununua Apartment za mradi wa Mikocheni yameanza kupokelewa. Hivyo amesema kwa taarifa nyingi zaidi kuhusu huduma zitolewazo na WHI zinapatikana kwenye website “whi.go.tz” na kwenye account zao za social media .






Meneja Masoko na Uhamasishaji wa Mfuko wa Self Microfinance Fund uliopo chini ya Wizara ya fedha, Bi. Linda Mshana akiongea na waandishi wa habari katika Maonyesho ya tatu ya wiki ya Huduma za Kifedha Kitaifa yanafanyika mkoani Arusha, kwenye viwanja vya Sheikh Amri Abed Jijini, Arusha.
Afisa mikopo kutoka Self, Bw. Mbwana Msangule akiendelea kuwapa elimu wateja walioudhuria katika banda lao lililopo katika Maonyesho.

Na Mwandishi Wetu, ARUSHA.

Watanzania wametakiwa kujitokeza kwa wingi kupata elimu kuhusiana na masuala ya fedha ili iwasaidie kutimiza malengo yao na kukuza uchumi kwa ujumla.

Ili kuepuka matatizo ya kuuziwa mali, kutokana na kushidwa kurejesha mikopo wanayochukuwa katika taasisi mbalimbali.

Hayo yamebainishwa na Meneja Masoko na Uhamasishaji wa Mfuko wa Self Microfinance Fund uliopo chini ya Wizara ya fedha, Bi. Linda Mshana wakati akiongea na waandishi wa habari katika Maonyesho ya tatu ya wiki ya Huduma za Kifedha Kitaifa yanafanyika mkoani Arusha, kwenye viwanja vya Sheikh Amri Abed Jijini, Arusha.

Bi. Linda Mshana amesema kuwa chanzo ni kutokuwa na uelewa wa kutosha pamoja na elimu ya duni ndicho kinachopelekea baadhi ya Watanzania kushindwa kurejesha mikopo mbalimbali kwani wengi wao wamekuwa wakifanya maamuzi pasipo kuwa na uelewa wa kutosha katika eneo hilo.

Amebainisha kuwa kulingana na mahitaji ya mikopo na kuongezeka kwa utitiri wa taasisi za mikopo, vijana wa Kitanzania wanashauriwa kuungana na kukopa kwenye taasisi za fedha za kuaminika na zenye usimamizi wa serikali ili kuepuka fedhea katika mikopo hiyo huku akiwasihi kupata elimu ya kutosha kabla ya kuichukuwa mikopo hiyo.

Aidha ametaja aina za mikopo ambayo inatolewa na mfuko wa SELF Microfinance ni mkopo wa Kilimo, Biashara, Makazi, mkopo wa pamoja, mkopo wa Imarika, Mkopo wa Mahitaji na mikopo wa Mkulima ambapo pia alifafanua kuwa nia yao ni kuendela kuwapatia watanzania elimu na kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo hapa nchini.

Amesema kuwa kila Mtanzania ana fursa kubwa ya kupata mkopo na kujikuza kiuchumi, kwa wajasiriamali wote wachini, wa kati, wakubwa, wafanyakazi,na watuwanaotaka kuboresha makazi.

“Wale waliopo kwenye vikundi wanaotaka mikopo ya kujiinua kiuchumi, wasiache fursa zikawapita, tunawafanyakazi waliokidhi na wana weledi wakuhudumia wajasirimali wote wanaotaka kujinua kichumi wafike tu katika matawi yetu yalipo katika mikoa mbalimbali ikiwemo hapa Arusha katika jengo la hazina ,Mwanza ,Dodoma,Dar es Salaam, Mbeya, Kahama, Geita, Morogoro, Tanga, Mtwara, Iringa pamoja na Zanzibar kupata elimu ya kutosha kuhusiana na mikopo namna ya kurejesha pamoja na riba" amebainisha Linda.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Mkumbo (Mb,)wakati alipozindua kitabu cha mwongozo wa uwekezaji Mkoani Tanga wenye kauli mbiu Wekeza Tanga kwa Uwekezaji Endelevu.
NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii na Mbunge wa Jimbo la Mkinga (CCM) Dastan Kitandula akizungumza wakati wa kongamano hilo.
MKUU wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kongamano hilo.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhamani akizungumza wakati wa Kongamano hilo.
Na Oscar Assenga,TANGA
NI Ukweli usiopingika kwamba kumekuwa na urasimu usio wa lazima katika mchakato wa uwekezaji ambao wakati mwengine unatajwa kwamba ndio chanzo cha kuwakatisha tamaa wenye nia ya kufanya hivyo.

Jambo hilo limekuwa likipelekea kukwamisha watu wenye nia ya dhati ya kuwekeza na hilo kubwa linatokana na urasimu ambao unadaiwa kufanywa na mamlaka zinazohusika kwenye mchakato huo.

Kwa kuliona hilo kwamba jambo hilo ni changamoto kubwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Mkumbo (Mb,) analitoa kauli wakati alipozindua kitabu cha mwongozo wa uwekezaji Mkoani Tanga wenye kauli mbiu Wekeza Tanga kwa Uwekezaji Endelevu.

Prof.Mkumbo anakemea vikali urasimu unaofanywa na Mamlaka zinazohusika na Uwekezaji kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi na kusababisha Serikali kukosa mapato yake ya msingi

Katika Taarifa hiyo Prof.Mkumbo anawaagiza viongozi wa Serikali ngazi za mikoa kuhakikisha wanaondoa changamoto zinazowakabili wafanyabiashara wa kutoka ndani na nje yaa nchi ambao wakiwekeza wanalipa kodi na kukuza uchumi.

Katika hatua nyengine anazitaka mamlaka zote zinazohusika kwenye mchakato wa uwekezaji ziondoe urasimu usio wa lazima kiasi cha kuwakatisha tamaa wawekezaji.

Anaeleza kuwa kongamano hilo linaashiria dhamira ya dhati ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kukuza uchumi nchini hivyo uzinduzi huu ni hatua muhimu katika safari ya kujenga taifa linalovutia wawekezaji kutoka pande zote duniani kuja kushirikiana na Mikoa yote nchini.

Prof. Mkumbo anasema kuwa mfumo imara wa mazingira wezeshi ya uwekezaji ndio uti wa mgongo wa Taifa lolote linalojinasibu katika kufufua na kuimarisha uwekezaji wenye ustawi.

“Katika kutengeneza fursa za ajira, kuimarisha miundombinu na kuinua ubora wa maisha kwa wananchi wake lakini pia Mamlaka za Serikali za Mitaa zitenge maeneo mahususi na kuyahodhi kwa ajili ya uwekezaji “Anasema

Anasema pia wahakikisha wanayaweka miundombinu yote muhimu na kuandaa mkakati wa mawasiliano ili kuongeza kasi ya kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo na mipango yote ya uwekezaji izingatie dhamira ya Serikali ya uhifadhi na utunzaji wa mazingira.

Awali akizungumza katika Kongamano hilo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Waziri Kindamba anasema kuwa lengo la uzinduzi wa muongozo wa uwekezaji ni kufungua fursa za kilimo, uchumi wa bahari, viwanda, utalii, usafiri, afya, elimu, huduma za fedha, uendelezwaji wa miji na uboreshaji wa maeneo ya michezo.

Kindamba ameongeza kuwa Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (East African Crude Oil Pipeline) wenye thamani ya dola za kimarekani 3.5 bilioni ni ishara tosha ya dhamira ya Serikali yetu katika kuhakikisha nchi yetu inafanya uwekezaji mkubwa na wenye tija kwa Taifa na wananchi wa kizazi cha sasa na cha baadae.

Anasema kuwa uwekezaji uliofanywa katika kuboresha Bandari ya Tanga uligharimu kiasi cha shilingi za kitanzania bilioni 429.1 ambapo kazi zilizofanyika zilikuwa ni kupanua gati na kuongeza kina na hivyo kuongeza uwezo na ufanisi wa Bandari hiyo.

Aliongeza ili kuhakikisha kwamba inaweza kukidhi ongezeko la shughuli inayoendelea ya ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki na shughuli nyingine za kibiashara, kiusafirishaji na kiuwekezaji. Bomba la mafuta linaloanzia Hoima nchini Uganda hadi chongoleani Tanga

Kongamano hilo limehudhuriwa na Waheshimiwa Mabalozi kutoka Rwanda, Burundi, Uganda na wengine kushiriki kwa njia ya mtandao, Naibu waziri Wizara ya Maliasiri na Utalii Mhe. Danstan Kitandula (Mb), Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge, Mheshimiwa Nurdin Babu, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro pamoja na wakuu wa Wilaya, wabunge, makatibu tawala na wakurugenzi wa halmashauri.

Ndio maana tunasema kwamba kauli ya Prof.Mkumbo ifanyiwe kazi ipasavyo na mam laka husika ili iweze kuleta tija kwa wawekezaji ambao wanakuja kuwekeza hapa nchini na wale wazawa na isipuuzwe.