TRENDING NOW






Her Excellency Dr. Samia Suluhu Hassan, President of the United Republic of Tanzania, today held talks with the Acting United States Ambassador to Tanzania, Andrew Lentz, at Chamwino State House to advance key areas of bilateral cooperation and reaffirm the shared commitment to a modern, mutually beneficial partnership.

Ambassador Lentz—accompanied by the Counselor for Political and Economic Affairs—underscored Washington’s determination to reset the relationship and deepen economic, political, and security collaboration with Tanzania.

“The United States is committed to a partnership based not on aid dependency but on shared prosperity,” Ambassador Lentz said.

The discussions centred on ongoing negotiations involving major U.S.-linked strategic investments. Both sides acknowledged that talks on two flagship projects—the LNG Project and Tembo Nickel Project—are now in their final stages, pending formal signing. A third investment, the Mahenge Graphite Project, remains under active technical review.

President Samia welcomed Washington’s renewed commitment and assured the delegation that Tanzania remains focused on completing the remaining procedural steps.

“As a non-aligned nation, Tanzania is open, ready, and committed to working with all partners who respect our sovereignty and share our vision for prosperity,” the President said.

“These strategic projects are of national importance, and we are determined to finalise them so they can unlock jobs, investment, and sustainable prosperity for our people.”

The President highlighted that more than 400 American companies currently operate in Tanzania—reflecting the country’s stability, openness to investment, and strong historical ties with the United States.

Beyond investments, the meeting touched on broader areas of cooperation, including political stability, regional security, economic reforms, private-sector growth, health-sector partnerships, and people-to-people exchanges.

Ambassador Lentz congratulated President Samia for her vision and long-term national planning through Vision 2050, noting the U.S. Government’s readiness to support its implementation and reinforce the President’s 4R philosophy of reconciliation, resilience, reforms, and rebuilding trust.

Both sides agreed that strengthened communication, consistent engagement, and timely action on pending agreements are key to unlocking the full potential of U.S.–Tanzania relations.

This meeting marks a pivotal moment in redefining and revitalising the U.S.–Tanzania relationship. The reaffirmed commitment from both governments signals the emergence of a modern, transparent, private-sector-driven partnership rooted in shared prosperity, mutual respect, and long-term strategic cooperation.

Flagship Projects

1. LNG Project — Estimated Value: USD 42 Billion

A transformative natural gas development involving leading international energy companies. The project aims to unlock Tanzania’s vast offshore gas reserves, boost national revenue, create thousands of jobs, and position the country as a major global LNG supplier.

2. Tembo Nickel Project — Value: USD 942 Million

A major critical-minerals investment in Ngara focused on nickel—an essential component in electric-vehicle batteries. The project will support global clean-energy supply chains, stimulate industrialisation, and expand Tanzania’s export base.

3. Mahenge Graphite Project — Value: USD 300 Million

One of the world’s largest high-grade graphite deposits, positioned to serve the fast-growing battery and renewable-energy sectors. The project will reinforce Tanzania’s role as a leading supplier of battery-grade minerals.

Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo amefanya mazungumzo na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Andrew Lentz, katika Ikulu ya Chamwino, kujadili maeneo muhimu ya ushirikiano na kuimarisha dhamira ya pamoja ya kujenga ushirikiano wa kisasa na wenye manufaa kwa pande zote mbili.
Balozi Lentz—aliyefuatana na Mshauri wa Masuala ya Kisiasa na Uchumi—amesisitiza dhamira ya Washington kuhuisha mahusiano na kuongeza kina la ushirikiano wa kiuchumi, kisiasa na kiusalama kati ya mataifa haya mawili.

“Marekani imejitolea kujenga ushirikiano usiotegemea misaada, bali unaojengwa juu ya ustawi wa pamoja,” alisema Balozi Lentz.

Mazungumzo yamejikita katika hatua za majadiliano ya miradi mikubwa inayoongozwa na kampuni za Marekani. Pande zote mbili zimekubaliana kuwa majadiliano ya miradi miwili ya kimkakati—Mradi wa LNG na Mradi wa Tembo Nickel—yamefikia hatua za mwisho kabla ya kutiwa saini rasmi. Uwekezaji wa tatu, Mradi wa Mahenge Graphite, unaendelea kufanyiwa uchambuzi wa kiufundi.
Rais Samia ameukaribisha upya msimamo wa Marekani na kuhakikishia ujumbe huo kuwa Tanzania itaendelea kusimamia hatua zote zilizobaki ili kukamilisha taratibu na kufungua njia ya utekelezaji wa miradi hiyo.

“Kama taifa lisilofungamana na upande wowote, Tanzania iko wazi, tayari na imejitoa kufanya kazi na washirika wote wanaoheshimu uhuru wetu na kushiriki katika dira yetu ya maendeleo,” alisema Rais.

“Miradi hii ni ya umuhimu mkubwa kwa taifa, na tumejidhatiti kuikamilisha ili iweze kufungua ajira, uwekezaji, na ustawi endelevu kwa wananchi wetu.”

Rais pia alibainisha kuwa zaidi ya kampuni 400 za Marekani kwa sasa zinafanya shughuli zao nchini Tanzania—kiashiria cha uthabiti wa nchi, mazingira mazuri ya uwekezaji na historia ya muda mrefu ya ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa haya mawili.

Mbali na uwekezaji, mazungumzo yamegusa maeneo mapana ya ushirikiano ikiwemo utulivu wa kisiasa, usalama wa kikanda, mageuzi ya kiuchumi, ukuaji wa sekta binafsi, ushirikiano katika afya na programu za kubadilishana uzoefu kati ya wananchi wa nchi hizi mbili.

Balozi Lentz amempongeza Rais Samia kwa maono na mipango madhubuti ya muda mrefu kupitia Vision 2050, na kusisitiza kuwa Serikali ya Marekani iko tayari kuunga mkono utekelezaji wake pamoja na kuimarisha falsafa ya 4R ya Rais—maridhiano, ustahimilivu, mageuzi na kujenga upya imani katika utawala.

Pande zote zimekubaliana kuwa mawasiliano ya karibu, ushirikiano wa mara kwa mara, na hatua za haraka katika kukamilisha makubaliano yaliyosalia ni muhimu katika kufungua uwezo kamili wa uhusiano kati ya Tanzania na Marekani.

Kikao hiki kinawakilisha hatua muhimu katika kufafanua upya na kuhuisha mahusiano kati ya Tanzania na Marekani. Dhamira ya pamoja iliyothibitishwa na serikali zote mbili inaashiria mwanzo wa ushirikiano wa kisasa, wazi, unaoongozwa na sekta binafsi—ukijengwa juu ya ustawi wa pamoja, kuheshimiana na ushirikiano wa muda mrefu wa kimkakati.

Miradi Mikuu ya Kimkakati

1. Mradi wa LNG — Thamani Inayokadiriwa: Dola Bilioni 42

Mradi mkubwa wa kugundua na kuchakata gesi asilia unaohusisha kampuni kubwa za kimataifa za nishati. Mradi huu unalenga kufungua hazina kubwa ya gesi iliyopo baharini, kuongeza mapato ya taifa, kuunda maelfu ya ajira na kuiweka Tanzania katika ramani ya dunia kama mchezaji muhimu wa LNG.

2. Mradi wa Tembo Nickel — Thamani: Dola Milioni 942

Uwekezaji mkubwa wa madini muhimu eneo la Ngara unaolenga nikeli—kiungo muhimu katika utengenezaji wa betri za magari yanayotumia umeme. Mradi huu utaimarisha minyororo ya kimataifa ya nishati safi, kuchochea viwanda na kuongeza pato la mauzo ya nje.

3. Mradi wa Mahenge Graphite — Thamani: Dola Milioni 300

Chanzo kikubwa duniani cha madini ya graphite yenye ubora wa juu, yenye umuhimu katika uzalishaji wa betri na teknolojia za nishati jadidifu. Mradi huu utaimarisha nafasi ya Tanzania kama mtoa huduma mkuu wa malighafi muhimu za viwanda vya kisasa vya betri.

  
Dar es Salaam – Katika hafla ya Marketers Night Out iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa, aliwasilisha mada iliyoangazia kwa kina mchango wa programu ya Imbeju katika kubadilisha maisha ya wananchi, hasa wanawake na vijana, kupitia uwezeshaji wa kiuchumi na kukuza ujumuishi wa kifedha nchini.

Akizungumza mbele ya wataalamu wa masoko, viongozi wa taasisi, wajasiriamali na wadau wa maendeleo, Mwambapa alisema Imbeju ni zaidi ya mpango wa kutoa mikopo pekee bali ni programu jumuishi inayolenga kujenga msingi imara wa ujasiriamali. Alieleza kuwa programu hiyo imejengwa juu ya nguzo tatu kuu; elimu ya ujasiriamali na uongozi, upatikanaji wa mitaji rafiki, pamoja na uunganishaji wa wajasiriamali na masoko pamoja na huduma rasmi za kifedha.
 
“Kupitia mafunzo ya vitendo, washiriki huwezeshwa kuendesha biashara zao kwa ufanisi zaidi, kutumia fursa za teknolojia, kufuatilia mapato na faida kwa weledi na kufanya maamuzi sahihi ya uwekezaji. mbinu hiyo imewezesha wajasiriamali wengi kuimarisha biashara zao na kuongeza ajira katika jamii”, alisema Mwambapa

Akizungumzia wanawake, Mwambapa alieleza kuwa wamekuwa walengwa muhimu wa programu kwani ndio mhimili wa ustawi wa familia na jamii. Wanawake wengi waliokuwa wakikabiliwa na changamoto za mtaji na elimu ya ujasiriamali sasa wameweza kuanzisha au kupanua biashara zao kupitia Imbeju, jambo lililosababisha kuongezeka kwa uzalishaji, kuboreshwa kwa kipato cha kaya na kuinuka kwa hali ya maisha ya familia zao. Alisisitiza kuwa uwekezaji kwa mwanamke mmoja hupelekea kuleta mafanikio kwa kizazi kizima.

Kwa upande wa vijana, alisema programu hiyo imekuwa chachu ya kubadilisha fikra bunifu kuwa miradi halisi katika maeneo ya teknolojia, kilimo-biashara, sanaa na biashara mtandao. Kupitia ushauri wa kitaalmu, mafunzo na ufadhili wa mawazo bunifu, vijana wengi wamepata uwezo wa kuzifikisha bidhaa zao katika masoko mengi zaidi kupitia majukwaa ya kidijitali, hivyo kuongeza ushindani na kupanua wigo wa biashara zao.
Mwambapa pia aligusia mchango wa Imbeju katika kukuza ujumuishi wa kifedha nchini kwa kuwawezesha wananchi waliokuwa nje ya mfumo rasmi wa benki kufungua akaunti, kujiwekea akiba, kukopa na kufanya miamala kwa urahisi zaidi baada ya kupata elimu ya kifedha. Kupitia ushirikiano wa CRDB Bank Foundation na Benki ya CRDB, huduma hizi sasa zimefika hata maeneo ya vijijini ambako upatikanaji wa huduma za kifedha ulikuwa mdogo awali.

Alisema hatua hiyo imeimarisha uthabiti wa biashara ndogondogo, kuongeza uwezo wa kujitegemea kwa wananchi na kuongeza mchango wa sekta hiyo katika ukuaji wa uchumi wa taifa.

Akihitimisha mada yake, Mwambapa alitoa wito kwa wadau wote kuendelea kuwekeza katika mipango inayowawezesha wanawake na vijana, akisisitiza kuwa mafanikio ya Imbeju ni ushahidi kuwa uwekezaji katika watu ndiyo msingi wa kujenga uchumi jumuishi, thabiti na wenye tija kwa kizazi cha sasa na kijacho.
Morogoro, Jumamosi, 6 Desemba 2025 — Msanii nguli wa muziki wa Bongo Flava, Afande Sele, anatarajiwa kuandika historia mpya leo baada ya kuamua kuingia rasmi katika maisha ya ndoa na mchumba wake, mwandishi wa habari Imani Makongoro.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Kamati ya Harusi, ndoa hiyo imepangwa kufungwa katika eneo la Nguzo Camp jijini Morogoro, kabla ya wageni kuelekea kwenye tafrija itakayofanyika katika ukumbi wa Hotel ya Morena.

Sherehe hiyo inatarajiwa kuhudhuriwa na ndugu, jamaa, marafiki pamoja na wadau mbalimbali wa muziki na vyombo vya habari.

Afande Sele, ambaye anatambulikana na wengi kama “Mfalme wa Rhymes Tanzania”, amekuwa mmoja wa wasanii wenye mchango mkubwa katika muziki wa hip hop nchini, huku mchumba wake Imani Makongoro akiwa miongoni mwa waandishi chipukizi wenye taswira pana katika uandishi wa habari.
Mhe. Grace Ngowi Jungulu akionesha zawadi ya kitabu cha Mungu Biblia aliyozawadiwa na watumishi wake wakati wa hafla fupi ya kuwashukuru wanachama na wananchi waliojitokeza kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa Serikal Oktoba 29 mwaka huu.

Na Mwandishi Wetu, KIBAHA 

Mhe. Grace Ngowi Jungulu amesema sasa ni muda wa kazi na milango ya nyumba yake ipo wazi, pale wanapoona kuna tatizo wasisite kumpigia simu au kufika nyumbani kwake.

Jungulu amesema, yeye amechaguliwa na wananchi wa Kata ya Picha ya Ndege, hana budi kuwatumikia na hilo atalifanyika kwa uwezo wake wote.

Hayo ameyasema Diwani wa Kata ya Picha ya Ndege Mhe. Grace Ngowi Jungulu wakati wa kuuwashukuru wanachama wote wa CCM na wananchi wa Kata ya Picha ya Ndege baada ya kumchagua na kushindwa kwa kishindo katika Uchaguzi Mkuu wa Serikali uliofanyika Oktoba 29, mwaka 2025.

Akizungumza na wananchi wake wakati wa hafla fupi baada ya kuapishwa, Mhe Jungulu amesema anashukuru kwa ushindi aliopata anaamini yale aliyoyaanza kuyafanya akiwa Mwenyekiti wa CCM Kata ataenda kuendelea kuyamalizia kwa sababu tayari ameshapata nafasi ya kuwasilisha changamoto zote kwenye Serikali Kuu.

Mhe. Jungulu amesema, Kata ya Picha ya Ndege imeweza kumuamini na kumpa nafasi hiyo ya kuwatumikia na anawaahidi kuwa atatimiza yale yote aliyowaahidi wakati wa kampeni.

Aidha, katika hafla hiyo fupi, Mhe Jungulu amewaomba Vijana kutokengeuka na kufuata mkumbo ambao utakuja kuchafua amani iliyopo Kata ya Picha ya Ndege.

"Leo hii mimi nikiwa Diwani wa Kata ya Picha ya Ndege, nawaambia kuwa vijana msije mkajaribu kukengeuka na kufuata mkumbo wa kutuondolea amani iliyopo ndani ya Kata yetu, sitaruhusu hilo litokee,"amesema Jungulu 

Amewataka wananchi kulinda amani ya Picha ya Ndege na kusema yeye akiwa kama Diwani yupo tayari kushirikiana nao kwenye nyakati zote , namba zake zipo hewani hata milango ya nyumba yake ipo wazi pale wanapokuwa wanahitaji kuzungumza nae.

Pamoja na yote, Mhe Jungulu amewashukuru wafanyakazi wake ambao waliweza kumzawadia Kitabu cha Biblia pamoja na picha ya Bikira Maria na wamemtaka kutumia muda wake mwingi kumuomba Mungu amuongoze kwenye shughuli zake za kila siku.

Tarehe 04/12/2025 ilikua ni siku ya uapisho wa Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Mjini ambapo madiwani 19 na tayari kuanza kuwatumikia wananchi wa Jimbo la Kibaha Mjini.
Mhe Grace Ngowi Jungulu akisaini baada ya kumaliza kuapa na kuwa Diwani kamili wa Kata ya Picha ya Ndege. 
Wananachi na wafanyakazi wakiwa na furaha.