
Serikali ya Tanzania imeanza mkakati mpya wa kimataifa wa kutangaza madini ya Tanzanite katika soko la Mashariki ya Kati, ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kurejesha hadhi na thamani ya madini hayo adimu duniani.
Akizungumza Februari 25, 2026 jijini Doha, Waziri wa Madini Anthony Mavunde alisema serikali imeamua kuongeza juhudi za kuitangaza Tanzanite kimataifa baada ya kubaini kuwa baadhi ya masoko bado hayafahamu asili ya madini hayo kuwa yanapatikana Tanzania pekee.
Aidha, serikali imepanga kuratibu ushiriki wa wafanyabiashara wa madini ya vito kutoka Tanzania katika maonesho ya kimataifa ya madini yatakayofanyika Doha mwezi Aprili 2026, yakilenga kupanua masoko, kuongeza uwekezaji na kuimarisha utalii unaotokana na rasilimali madini.
Kwa upande wake, Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mheshimiwa Habibu Awesi Mohamed, alisema fursa za ushirikiano katika sekta ya madini ni kubwa na zikiendelezwa zinaweza kuongeza mapato ya taifa na kukuza uchumi






Toa Maoni Yako:
0 comments: