Na Mwandishi Wetu, Iringa

MKUU wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Kheri James (Pichani), ameonesha kukerwa na kitendo cha Mkuu wa Shule moja mkoani humo aliyerudisha nyumbani wanafunzi waliochelewa kuleta rimu baada ya shule kufunguliwa, akisema hatua hiyo imekosa hekima, busara na haizingatii ustawi wa watoto.

Akizungumza kuhusu hali ya lishe na upatikanaji wa chakula kwa wanafunzi shuleni, RC Kheri James amesema viongozi na watumishi wa umma wana wajibu wa kutumia busara katika kufanya maamuzi, hasa yale yanayohusu moja kwa moja haki na maisha ya watoto. Amesisitiza kuwa maamuzi yanayowagusa wanafunzi yanapaswa kufanywa kwa kuzingatia mazingira halisi ya jamii.

RC Kheri ameongeza kuwa si wazazi na walezi wote wana uwezo sawa wa kiuchumi, hivyo ni muhimu kwa viongozi wa shule kuelewa changamoto zinazowakabili baadhi ya familia kabla ya kuchukua hatua zinazoweza kuwaumiza watoto. “Hatuwezi kudhani kila mzazi ana uwezo sawa. Maisha ya watu yanatofautiana, na hili lazima litambuliwe,” amesema.

Aidha, amewataka viongozi wa elimu kuacha tabia ya kujisahau na badala yake waweke mbele maslahi ya wanafunzi, akisisitiza kuwa elimu ni haki ya msingi kwa kila mtoto na changamoto ndogo za vifaa vya shule hazipaswi kuwa sababu ya kuwanyima watoto haki hiyo.

Amehitimisha kwa kutoa wito kwa walimu wakuu na wasimamizi wa shule zote mkoani Iringa kuhakikisha wanajenga mazingira rafiki ya ujifunzaji, yanayochochea ushiriki wa wanafunzi wote bila ubaguzi, kwa lengo la kufanikisha maendeleo ya elimu na ustawi wa watoto.
Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: