Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan,ametoa tuzo kwa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) ikiwa ni kutambua mchango mkubwa wa kampuni na wadau wengine katika juhudi zao za uhifadhi wa mazingira na kuliletea taifa maendeleo endelevu.
● Kupanda miti zaidi ya 10,000 katika Kanda ya Kaskazini na Kanda ya Kati
● Kutekeleza miradi ya maji safi na salama zaidi ya 28 kwa jamii zinazozunguka maeneo yake ya uzalishaji
● Kuwekeza katika kilimo endelevu kwa kuunga mkono vijana zaidi ya 300 kupitia mpango wa Kilimo Viwanda
Aidha, SBL imeanzisha mpango wa Shamba ni Mali, unaolenga kuwapatia wakulima mbolea, mbegu bora, teknolojia ya kisasa na elimu ya kilimo, na lengo la kuwafikia wakulima zaidi ya 4,000 ifikapo mwaka 2030.
Utambuzi huu unaakisi mchango wa SBL kama mdau anayejali mazingira na kuthamini jamii anazozihudumia, sambamba na kuunga mkono ajenda ya Taifa ya maendeleo endelevu




Toa Maoni Yako:
0 comments: