Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ametangaza kusitishwa kwa muda huduma za Mabasi yaendayo Haraka (UDART) katika barabara kuu mbili za jiji hilo — Morogoro kutokaHuduma za Mabasi ya Mwendokasi Zasitishwa kwa Muda Jijini Dar es Salaam katikati ya mji kuelekea Kimara na Morocco, pamoja na barabara ya Kilwa kutoka katikati ya jiji kuelekea Mbagala — kufuatia kuharibika kwa miundombinu.

Akizungumza leo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Chalamila alisema uharibifu huo umetokana na matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea wakati wa uchaguzi, ambapo baadhi ya waandamanaji waliharibu mifumo ya ukataji tiketi na maeneo ya kupakia abiria.

“Tumelazimika kusitisha huduma hiyo kutokana na uhalifu uliofanyika wakati wa uchaguzi na kusababisha kuharibika kwa mifumo yote ya ukataji tiketi pamoja na vituo vya abiria,” alisema Chalamila. “Kwa sasa tunatoa maelekezo kwa LATRA kutoa vibali vya muda kwa wamiliki wa daladala ili kuwahudumia wakazi wa maeneo hayo.”

Amesema serikali inaendelea kufanya tathmini ya hasara iliyosababishwa na uharibifu huo, na baada ya ukarabati kukamilika, huduma za mabasi ya mwendokasi zitarejeshwa kama kawaida.

Katika hatua nyingine, RC Chalamila ametangaza kufunguliwa kwa Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli kilichopo Mbezi Luis, na kuwataka wafanyabiashara waliokuwa wakifanya shughuli zao katika eneo hilo kurejea kuendelea na biashara kama awali.

Aidha, amewatoa hofu wakazi wa Dar es Salaam akisema kuwa hali ya usalama katika jiji hilo imeimarishwa, huku akibainisha kuwa ulinzi umeongezwa katika Kituo cha Magufuli ili kulinda abiria, mali na shughuli za kibiashara.

Wakati huohuo, Chalamila ameiagiza Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Mashariki kuitisha kikao cha dharura na wamiliki wa vituo vya mafuta kujadili utekelezaji wa marufuku ya uuzwaji mafuta kiholela katika vidumu.

RC Chalamila ametumia nafasi hiyo kutoa wito kwa wakazi wa Dar es Salaam na Watanzania kwa ujumla kuendelea kuwa walinzi wa amani ya nchi, akisisitiza kwamba maendeleo hayawezi kupatikana bila utulivu na mshikamano wa kitaifa.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: