Na Mwandishi Wetu, Nairobi

Mwili wa aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Kenya, Mhe. Raila Amollo Odinga, umelazwa leo katika Jumba la Bunge, ikiwa ni heshima ya kitaifa kwa kiongozi huyo ambaye kwa zaidi ya miongo mitano aliweka alama kubwa katika historia ya siasa na demokrasia nchini. Hatua hiyo inalenga kutoa nafasi kwa mihimili yote mitatu ya dola — Serikali Kuu, Bunge na Mahakama — pamoja na wananchi kwa ujumla, kutoa heshima zao za mwisho kwa mzalendo huyo.

Kwa miaka 20, Raila aliwatumikia wananchi wa Jimbo la Lang’ata kama Mbunge, akijulikana kwa msimamo wake thabiti katika kutetea haki, demokrasia na maendeleo. Aidha, mchango wake mkubwa ulionekana wakati wa uongozi wake kama Waziri Mkuu, ambapo alihusishwa moja kwa moja na mageuzi makubwa ya kisheria na kisiasa, hususan kupitishwa kwa Katiba ya mwaka 2010.

SSerikali imesema kuwa kumlaza Raila bungeni ni ishara ya heshima na shukrani kwa mchango wake mkubwa kwa taifa. “Ni heshima stahiki kwa kiongozi ambaye maisha yake yote yalijikita katika kutafuta demokrasia, usawa na mshikamano wa kitaifa,” ilisomeka sehemu ya taarifa rasmi.

Wananchi wanatarajiwa kupewa fursa ya kuuaga mwili wake baada ya viongozi wa kitaifa, huku maandalizi yakiendelea kuelekea mazishi ya kitaifa yatakayofanyika nyumbani kwake Bondo, Kaunti ya Siaya.

Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: