Na Mwandishi Wetu, Nairobi

Kenya leo imeungana kama taifa kushiriki ibada kuu ya kitaifa ya kumbukumbu kwa heshima ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Mhe. Raila Amolo Odinga, aliyeaga dunia akiwa na miaka 80. Ibada hiyo imefanyika kwa majonzi na mshikamano wa kitaifa, ambapo viongozi wa kisiasa, viongozi wa dini, wageni mashuhuri kutoka ndani na nje ya nchi pamoja na maelfu ya wananchi walijitokeza kuenzi maisha ya kiongozi huyo wa kipekee.

Katika hotuba zilizotolewa, Raila Odinga ametajwa kama mwanasiasa shupavu na mzalendo aliyeishi maisha ya ujasiri, amani na imani thabiti kwa taifa lake. Walisema urithi wake hautafutika, kwani maisha yake yaliandikwa kwa mfano wa kujitoa katika haki, demokrasia, mshikamano na maendeleo ya taifa.

"Patriotism, he showed us, is not about what the country gives to us, but about what we are willing to sacrifice and give for the betterment of our nation," ulisomeka ujumbe wa pamoja wa viongozi wa kitaifa.

Zaidi ya hayo, Raila ametajwa kama kiongozi mnyenyekevu, mwenye uvumilivu na imani thabiti katika mustakabali wa Kenya, ambaye hakuchoka kusimamia mabadiliko ya kikatiba na kidemokrasia yaliyoiweka Kenya katika ramani ya dunia kama taifa linaloenzi haki na mshikamano.

Ibada hiyo imetajwa kama tukio la kihistoria, sio tu kwa Kenya bali kwa Afrika nzima, kutokana na nafasi kubwa aliyokuwa nayo Raila katika harakati za ukombozi wa kisiasa na umoja wa bara.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: