Lazaro Nyalandu, aliyewahi kuwa Mbunge wa Singida Kaskazini kupitia Chama cha Mapinduzi, ametangaza kugombea Ubunge katika jimbo hilo kupitia CHADEMA.

Kupitia ukurasa wake Twitter Lazaro Nyalandu ameandika adhima yake hiyo ya kutaka kurudi kuwatumikia Wananchi wa Singida Kaskazini kwa nafasi ya Ubunge.

“Nitashiriki kama Mgombea katika kinyang’anyiro cha kumpata mgombea Ubunge kwa tiketi ya CHADEMA Jimbo la Singida Kaskazini, Uchaguzi huo utafanyika leo, Jumatatu, Agosti 10, kijijini Ilongero. Asanteni sana kwa sala na dua zenu na zaidi, kwa upendo wenu wa daima kwangu” Nyalandu
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: