Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars ambao walifika Ikulu jijini Dar es Salaam pamoja na Viongozi wa Shirikisho la Miguu la Tanzania TFF, BMT pamoja na Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea zawadi ya Jezi ya Timu ya Taifa kutoka kwa Nahodha wa Timu hiyo Erasto Nyoni Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Nahodha wa Timu hiyo Erasto Nyoni mara baada ya kumkabidhi Jezi ya Timu ya Taifa.
Beki wa Timu ya Taifa Shomari Kapombe akijitambulisha mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu ya Tanzania Taifa Stars mara baada ya kuzungumza nao Ikulu jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha mstari wa Mbele ni Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe watatu kutoka kushoto, Waziri wa Mambo ya Nje Balozi Dkt. Augustine Mahiga watatu kutoka kulia akifatiwa na Leodgar Tenga Mwenyekiti wa BMT, kocha wa timu ya Taifa Emanuel Amunike Pamoja na Katibu Mkuu wa TFF Wilfred Kidao. Wengine ni Rais wa TFF Wallace Karia akiwa pamoja na Nahodha wa Timu ya Taifa Erasto Nyoni.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Nahodha wa Timu ya Taifa Erasto Nyoni mara baada ya kupiga picha ya pamoja na Timu ya Taifa Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Kipa wa Timu ya Taifa Aishi Manula mara baada ya kupiga picha ya pamoja Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Beki kisiki wa Taifa ya Tanzania Kelvin Yondani mara baada ya kupiga picha ya pamoja Ikulu jijini Dar es Salaam. Picha na IKULU.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: