Aliongeza kuwa Serikali imeendelea kuimarisha huduma na matunzo kwa wazee kupitia Sera ya Taifa ya Wazee ya mwaka 2003, ambayo hivi karibuni imepitishwa katika toleo la mwaka 2024. Sera hiyo inaweka bayana wajibu wa familia na jamii katika kusimamia matunzo ya wazazi na wazee kwa ujumla, huku ikisisitiza kuimarisha mifumo ya kisheria itakayolinda na kuendeleza ustawi wa wazee pamoja na watoto wanaowatunza.
“Kwa sasa Serikali ipo katika hatua ya kuwashirikisha wadau mbalimbali ili kutoa maoni juu ya masuala muhimu ya kuzingatiwa katika sheria hiyo,” amesema Mhe. Mahundi.
Aidha, Naibu Waziri amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuhamasisha maadili ya uwajibikaji wa kifamilia na kuimarisha mifumo ya kijamii inayosaidia ustawi wa wazee nchini.
Hali hii inaashiria dhana ya Serikali kuwa kulea wazee ni jukumu la kijamii na la kifamilia, badala ya kuwalazimisha watoto kupitia sheria, huku ikiendelea kuboresha huduma za kijamii na kisheria zinazohakikisha ustawi wa wazee nchini.




Toa Maoni Yako:
0 comments: