Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nassoro , akizungumza na Waislam wa Kata ya Mtinko wakati wa harambee ya ujenzi wa msikiti iliyofanyika Septemba 3, 2023.

Na Dotto Mwaibale, Singida

WADAU mbalimbali wameombwa kuchangia ujenzi wa Msikiti wa Jaamigh uliopo Kata ya Mtinko Wilaya ya Singida, mkoani Singida ambapo jumla ya Sh. Bilioni 1.8 zinahitajika kwa ajili ya ujenzi wa msikiti huo.

Katibu wa kamati ya ujenzi wa msikiti huo, Abdallah Rajab akizungumza wakati akitoa taarifa ya ujenzi wa msikiti huo mbele ya Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nassoro alisema hadi kukamilika kwa ujenzi huo Sh.Bilioni 1.8 zinahitajika.

Rajab alisema msikiti wa awali ambao ulijulikana kama Msikiti wa Ijumaa Mtinko ulijengwa mwaka 1949 ukiwa na uwezo wa kuhudumia waumini 100 kwa wakati mmoja.

Alisema kutokana na ongezeko la waumini msikiti huo ulipanuliwa mwaka 1990 na kuwa na uwezo wa kuwahudumia waumini 300 na unatumika hadi hivi leo.

Rajab alisema kutokana na ongezeko la waumini na kuanza kuswalia nje mwaka 2018 ndipo walipopata wazo la kuanzisha ujenzi wa msikiti wa sasa wa ghorofa ambao ujenzi wake ulianza mwaka 2019.

'' Ujenzi upo hatua ya kusuka bimu kwenye msingi na ukikamilika utakuwa na uwezo wa kuhudumia waumini 1000 kwa wakati mmoja,'' alisema Rajab.

Alisema msikiti huo utakuwa na huduma za ofisi ya utawala, madrasa, vibanda vya biashara na huduma ya vyoo.

Alisema mahitaji makubwa ya hivi sasa ya ujenzi huo ni mchanga, saruji na nondo na kuwa katika hatua hiyo waliyoifikia ya ujenzi zimetumika Sh.Milioni 28,059,300 fedha zilizotokana na sadaka za waumini na wadau wengine mbalimbali na kuwa kwenye akaunti yao wana Sh.Milioni 3.

Baada ya kutolewa kwa taarifa hiyo iliyoandaliwa na uongozi wa msikiti wakishirikiana na kamati ya bodi ya msikiti, Jumuiya ya Wanawake wa Wakiislam } JUWAKITA }, wa kata hiyo na kamati ya ujenzi ilifanyika harambee ambapo zilipatikana zaidi ya Sh.Milioni 3.7.

Katika kuongeza nguvu ya kupatikana kwa fedha za ujenzi wa msikiti huo Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nassoro anatarajia kufanya harambee nyingine hivi karibuni katika tarehe itakayo pangwa ambayo itawashirikisha wadau na viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya Mkoa wa Singida.

Kamati ya ujenzi wa msikiti huo inawaomba wadau mbalimbali kusaidia ujenzi huo na kwa mtu yeyote, wafanyabiashara, taasisi watakaokuwa tayari kuchangia chochote walichonacho iwe saruji, kokoto, mchanga na vifaa vingine vya ujenzi na kama ni fedha wanaweza kuweka katika akaunti namba 0152737109500 Benki ya CRDB Mtinko Masjid au wanaweza kuwasiliana na Mtunza fedha wa msikiti huo Said Salim Mdimi kwa namba ya simu 0788778591 kwani kutoa ni moyo na si utajiri. 

Katibu wa Baraza la Masheikh Mkoa wa Singida, Said Ally Mang'ola akizungumza kwenye harambee hiyo.
Sheikh wa Kata ya Mtingo, Jumanne Ramadhan akichangia jambo wakati wa harambee hiyo.
Mwalimu wa Dini, Sheikh Isihaka Hassan akizungumza kwenye harambee hiyo.
Kikongwe Hadija Mandi akiwahamasisha Waislam kuchangia ujenzi wa msikiti huo.
Wazee wakiwa kwenye harambee hiyo.
Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nassoro|} katikati } akizungumza wakati akikagua ujenzi wa msikiti huo.
Muonekano wa ujenzi wa msikiti huo.
Kiongozi wa Kamati ya Wanawake wa Kiislam wa kata hiyo, Hawa Ayubu, akiongoza uhamasishaji wa kuchangia ujenzi huo.
Wakina mama wakiwa kwenye harambee hiyo.
Harambee hiyo ikiendelea.
Wakina mama wakichangia katika harambee hiyo.

Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: