Mkazi wa Kijiji cha Makangaga, Kata ya Kiranjeranje,Wilaya ya Kilwa,Mkoa wa Lindi,Salehe Lihanzi (47) akijiuguza majeraha baada ya kushambuliwa na watoto wake wa kufikia.

Na Said Hamdani, LINDI.

MKAZI wa Kijiji cha Makangaga, Kata ya Kiranjeranje,Wilaya ya Kilwa,Mkoa wa Lindi,Salehe Lihanzi (47) amelazwa Hosptalini akiuguza majeraha aliyoyapata baada ya kukatwa mapanga maeneo mbalimbali ya mwili wake na watoto wa kufukia wa mke wake.

Tukio hilo linaelezwa kutekelezwa na vijana hao August 31 mwaka huu saa 7;00 mchana,alipokuwa shambani akilinda mazao yake yasishambuliwe na wanyama waharibifu.

Lihanzi amelazwa wodi namba sita katika Hosptali ya Sokoine,nl mkoani Lindi na amewataja watoto hao kuwa ni Ally Halfani na Hassani Mbulula.

Amesema siku hiyo akiwa shambani akilinda mazao yasiliwe na wanyama waharibifu alifuatwa na vijana hao wakiwa na mapanga na fimbo mikononi mwao.

Lihanzi amesema baada ya kufika mahali aliposimama alikatwa panga mguu na mkono wa kulia na mtoto mkubwa Ally Halfani huku mdogo wake Hasani akimpiga na fimbo kichwani.

Ametaja sababu ya yote hayo ni kuwataka watoto wale kurejesha vitu walivyochukuwa kikiwemo kitanda cha mbao chenye ukubwa wa futi 5 kwa 6.

Amesema licha ya kuwaeleza kurejesha vitu hiyo, suala hilo alilifikisha kwa mama wa watoto hao Ashura Mbunda ambae ni mke wake na kwa bibi yao Zaria Omari ambapo walikubali kuvirudisha.

Amesema ndipo August 30, 2023 saa 7;00 mchana akiwa shambani vijana hao walimfuata na kuanza kumshambuli na kumsababishia maumivu makali.

Mkulima huyo amesema baada ya watoto hao kumfanyia ukatili huo waliondoka kuelekea Ofisi ya Mtendaji wa Kijiji na kueleza kule walicho mfanyia.

"Nilipowaona wanakuja sikuwa na hofu nao wala kudhani wanakuja kundhuru,"alisema Lihanzi.

Lihanzi amesema mtu wa kwanza kufika eneo la tukio ni mama mkwe wake Zaria Omari na kumuomba aende kijijini kuwapa taarifa ndugu zake kwa kile kilichomkuta.

Mkulima huyo amesema baada ya ndugu kufika eneo hilo walimchukua na kumpeleka Zahanati ya Kiranjeranje,lakini kutokana na uzito wa tatizo wakalazimika kumpeleka Hosptali ya Mkoa Sokoine,iliyopo mjini Lindi.

Amesema tayari askari polisi wamefika Hosptali kuchukuwa maelezo yake kwa ajili ya ya kuyafanyia kazi.

Mganga Mfawidhi Hosptali ya Sokoine,mkoani Lindi, Alexander Makalla amethibitisha kumpokea mgonjwa huyo August 30, 2023 saa 2;00 usiku.

Makalla amesema mgonjwa huyo ameshambuliwa na kitu chenye ncha kali mguuni na mkono wa kulia na kichwani na hali yake inaendelea vizuri kutokana na huduma za matibabu anayoyapata

"Mteja wetu amejeruhiwa mguu na mkono wa kulia na kichwsni" alisema Makalla.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi,Pili Mande amekiri kuwa na taàrifa hiyo na kueleza wanaendelea kuifanyia kazi.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: