Mbunge wa Jimbo la Chumbuni, Mhe. Ussi Salum Pondeza, ameshiriki ziara ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Bandari ya Abiria Maruhubi, mradi wa kimkakati unaolenga kuimarisha sekta ya usafirishaji na kukuza uchumi wa nchi.

Katika ziara hiyo, Mhe. Pondeza alijionea hatua za utekelezaji wa mradi huo muhimu kwa mustakabali wa wananchi wa Chumbuni na Zanzibar kwa ujumla, huku akieleza matumaini yake kuwa bandari hiyo italeta mabadiliko chanya kwa maisha ya watu.

Mhe. Hemed amesema kukamilika kwa bandari hiyo kutasaidia kupunguza msongamano wa abiria na mizigo katika Bandari ya Malindi, pamoja na kuchochea ukuaji wa biashara visiwani.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: