Na Mwandishi Wetu, Mwanza.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele leo Julai 03, 2025 amemtembelea na kukagua mwenendo wa zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika Gereza Kuu la Butimba lililopo mkoani Mwanza na kushuhudia namna zoezi linavyokwenda kwa ufanisi.

Mzunguko wa tatu wa awamu ya pili ya uboreshaji Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa Wafungwa chini ya miezi sita na mahabusu waliopo katika Magereza kwa Tanzania Bara na Vyuo vya Mafunzo Zanzibar ulianza Juni 28 na unataraji kukamilika Julai 04, 2025.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: