Na Oscar Assenga, TANGA

MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya Tanzania (NHIF) Mkoani umeshirikia maonyesho ya 11 ya Biashara na Utalii yanayoendelea kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara ili kutoa elimu kuhusu huduma wanazotoa ikiwemo vifurushi wanavyovitoa.

Banda la Mfuko huo limekuwa lililopo kwenye maonyesho hayo limekuwa ni kivutio kwa wananchi ambao wamefika kupima afya zao na kupata ushauri namna ya kuepukana na magonjwa yasiyoyakuambikizana.

Pia wananchi hao wamekwenda kwa ajili ya kuona namna ya kujiunga na vifurushi mbalimbali vinavyotolewa na mfuko huo ili kuweza kunufaika na matibabu bure pindi wanapougua.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: