BALOZI wa Tanapa nchini Nancy Sumari kushoto akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Kitaifa ya kutangaza utalii wa ndani hapa nchini uliofanyika kwenye hifadhi ya Taifa ya Mkomazi na kuzinduliwa na Mkuu wa wilaya ya Same Rosemary Senyamule kulia kuhusu umuhimu wa watanzania kutembelea vivutio vya utalii

Mkuu wa wilaya ya Same Rosemary Senyamule akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Kitaifa ya kutangaza utalii wa ndani hapa nchini uliofanyika kwenye hifadhi ya Taifa ya Mkomazi

MKUU wa Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi Abel Mtui kushoto akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo katikati ni Balozi wa Tanapa Nancy Sumari na kulia ni Mkuu wa wilaya ya Same Rosemary Senyamule.
Mkuu wa wilaya ya Same Rosemary Senyamule akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kampeni ya Kitaifa ya kutangaza utalii wa ndani hapa nchini uliofanyika kwenye hifadhi ya Taifa ya Mkomazi kushoto ni Balozi wa Tanapa Nancy Sumari na Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi Abel Mtui kushoto.
Mkuu wa wilaya ya Same Rosemary Senyamule akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kampeni ya Kitaifa ya kutangaza utalii wa ndani hapa nchini uliofanyika kwenye hifadhi ya Taifa ya Mkomazi kushoto ni Balozi wa Tanapa Nancy Sumari na Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi Abel Mtui

Balozi wa Tanapa nchini Nancy Sumari katikati akiwa ameshika kikombe akiwa na Mkuu wa wilaya ya Same Rosemary Senyamule kulia na Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi Abel Mtui kushoto wakati wa uzinduzi huo.
Mkuu wa wilaya ya Same Rosemary Senyamule kulia akipongezana na Balozi wa Tanapa nchini Nancy Sumari kushoto mara baada ya kufanya uzinduzi huo kushoto ni Mhifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi Abeli Mtui.
Balozi wa Tanapa nchini Nancy Sumari katikati akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa wilaya ya Same Rosemary Senyamule na Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi Abeli Mtui kushoto wakati wa watalii wa ndani waliotembelea hifadhi hiyo wakati wa uzinduzi huo.
Muongoza watalii kwenye Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi kulia akitoa maelezo mafupi kwa Balozi wa Tanapa nchini Nancy Sumary wakati aliptembelea hifadhi hiyo.
BALOZI wa Hifadhi za Taifa nchini (TANAPA) Nancy Sumari katika akiwa na baadhi ya watalii wengine wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya kutangaza utalii wa ndani.
Sehemu ya msururu wa magari ukiwa kwenye hifadhi ya Taifa ya Mkomazi

BALOZI wa Hifadhi za Taifa nchini (TANAPA) Nancy Sumari ametembelea hifadhi ya Taifa ya Mkomazi iliyopo wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro huku akiwahimiza watanzania kujenga mazoea ya kutembelea hifadhi zilizopo hapa nchini ili kuweza kujionea vivutio vilivyopo na kujifunza mambo mbalimbali ya uhifadhi wa wanyama pori.

Nancy ambaye aliwahi kuwa Miss Tanzania 2005 na mrembo wa Dunia Afrika mwaka huo aliyasema hayo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Kitaifa ya kutangaza utalii wa ndani hapa nchini iliyofanyika kwenye hifadhi ya Taifa ya Mkomazi na kuzinduliwa na Mkuu wa wilaya ya Same Rosemary Senyamule.

Alisema kwamba utalii wa ndani ni jambo muhimu sana kwa watanzania kwani unamuwezesha kutumia muda mchache kuweza kujifunza na kujionea vivutio vilivyopo ndani ya nchi na kuweza kuvifurahia.

“Kwa kweli niwashukuru wananchi, Mkuu wa wilaya ya Same na Mhifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi kwa kutukaribisha mimi na familia yangu kutembelea na kufurahia utalii wa ndani ni jambo nzuri na la kipekee sana hivyo niendelee kuwasihi watanzania tutembelee hifadhi zetu”Alisema

Hata hivyo aliwakaribisha marafiki na watanzania wengine kutembelea hifadhi ya Taifa ya Mkomazi kwani ni eneo ambalo la kipekee kutokana na kusheheni idadi kubwa ya wanyama wakubwa na ndege ambao wageni wanakutana nao wakati tu wanapoingia kwenye eneo la lango la geti hilo.

Awali akizungumza wakati wa uzinduzi huo Mhifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi Abel Mtui alisema kwamba katika kampeni hiyo wageni ambao walijiandikisha kuingia ndani ya hifadhi ni 78 ambao kati yao kutoka wilaya ya Mwanga ni 13, Same ni 55 na Hedaru ni 10 hivyo hiyo ni idadi kubwa ya kutosha na wanategemea waliokuja watakwenda kuwa mabalozi wazuri kwa wenzao.

Alisema anaimani idadi kubwa ya watalii wa ndani itazidi kuongezeka zaidi kwani wageni waliotembelea hifadhi hiyo wataenda kuwaarifu wenzao huku wageni ambao walipata fursa ya kutembelea hifadhi hiyo wakipiga picha na Balozi Nancy.

“Hivyo niendelee kuwahimiza watanzania kuendelea kutembelea vivutio vya utalii ambao vipo hapa nchini ikiwemo hifadhi ya Taifa ya Mkomazi ambayo inavuvutio vya kipekee”Alisema

Awali akizungumza wakati wa kampeni hiyo Mkuu wa wilaya ya Same Rosemary Senyamule alkiwakaribisha Balozi huyo na familia yake na wananchi ambao tayari walianza kujitokeza kwenye kufanya utalii wa ndani kwani wana matarajio makubwa sana na hifadhi ya mkomazi kutokana na kuwa na vuvutio vingi vinavyopatikana na vya kipelee ambavyo havipatikana maeneo mengine.

Mkuu huyo wa wilaya alisema kwamba wanatagemea hifadhi ya Taifa ya mkomozi inayokuwa kwa haraka kwa kuongeza idadi ya watalii wa ndani na nje ikiwemo kuongeza mapato na kukuza uchumi wa serikali na mwananchi mmoja mmoja.

“Tunaweka nguvu nyingi kama serikali kuhakikisha mkomazi inakuwa na kupata miundombinu na vitu vyengine vitakavyofanya watalii kuvutiw lakini pia ujio wa faru ni kuvutio ambacho kitakuwa hakuna eneo jengine Tanzania hadi ya mkomazi kunajengwa ukuta ambao faru watawekwa pale na upo kwenye hatua zxa mwisho za ukamilishaji”Alisema

“Kukamilika kwake utawawezesha watanzania ambao watakuwa wakifika Mkomazi anakuwa na uhakika wa kuona faru na itakuwa hifadhi pekee kwenye nchi ya Tanzania na nchi chache za Afrika na wanategemea jambo hilo litasaidia kupata idadi kubwa ya wageni “Alisema Dc huyo.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: