Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Subira Mgalu, (wapili kulia), akipatiwa maelezo wakati akikagua mitambo katika kituo cha kuzalisha umeme wa gesi asilia cha Somanga, Mkoani Lindi Februari 24, 2019.
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Subira Mgalu akihutubia wananchi wa Kijiji cha Nangambi ambapo alimlaumu mkandarasi anayehusika na kusambaza umeme vijijini Mkoani Lindi State Grid kwa kufanya kazi kwa kusuasua 
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Subira Mgalu akihutubia wananchi wa Kijiji cha Nangambi ambapo alimlaumu mkandarasi anayehusika na kusambaza umeme vijijini Mkoani Lindi State Grid kwa kufanya kazi kwa kusuasua 
Wananchi wa Nangambi na Naipul kata ya Migumbi Wilayani Kilwa wakimsikiliza Naibu wazi Wa Nishati Mhe. Subira Mgalu (hayupo pichani) wakati akiwahutubia.

NA SAMIA CHANDE, KILWA.


NAIBU Waziri wa Nishati Mhe Subira Mgalu amekerwa na kasi ya mkandarasi State Grid katika kutekeleza miradi ya kusambaza umeme vijijini Mkoani Lindi.

Akizungumza mwanzoni mwa ziara yake ya siku nne kukagua maendeleo ya usambazaji umeme vijijini huko Wilayani Kilwa Mkoani Lindi Februari 24, 2019, Mhe. Mgalu alisema kinachofanywa na mkandarasi huyo ni utapeli na ubabaishaji.

“Kiongozi wao anakaa Ulaya, huku kaacha tu watendaji wengine yeye hayupo nchini, hili halikubaliki kwani wanakwamisha juhudi za Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli za kuhakikisha wananchi wote wa Tanzania wanapata umeme wakiwemo wa vijijini.” Alisema.

Alisema, Wakandarasi wanaofanya kazi ya kusambaza umeme vijijini wamekabidhiwa kwa Wakuu wa wilaya na kuwataka wakuu wa wilaya kuchukua hatua kali dhidi ya wakandarasi wote wanaokwenda kinyume na mikataba yao kwa kufanya kazi kwa kusuasua bila sababu zozote za msingi.

Akionyesha kukerwa na kutoridhishwa na ubora wa kazi iliyofanywa na mkandarasi huyo yaani State Grid, Mhe. Naibu Waziri aligoma kuwasha umeme katika vijiji vya Nangambi na Naipul Kata ya Mingumbi Wilayani Kilwa na kuwataka wananchi kuwa na uvumilivu kwani suala la mkandarasi huyo atalifikisha kwenye mamlaka zinazohusika ili hatua za haraka zichukuliwe na ikiwezekana kuleta mkandarasi mwingine akamilishe kazi hiyo. 

Pia Naibu Waziri alipata fursa ya kutembelea kituo cha kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asili cha Somanga, (Somanga gas plant) kilichopo Somanga Fungu nakujione matengenezo ya mashine yanavyoendelea.

Kwa mujibu wa Meneja wa kituo hicho, Mhandisi Oscar Kidia, alimueleza Mhe Naibu Waziri kuwa kwa sasa mashine mbili katika kituo hicho zenye uwezo wa kutoa Megawati 5 zimefanyiwa matengenezo.

Nia ya Serikali ya awamu ya Tano ni kupeleka umeme wa uhakika na wakutosha katika Mikoa ya Kusini hivyo wananchi wawe tayari kuupoke umeme unapofika katika miji na vijiji kwani umeme utawasaidia kuchoche maendeleo na kukuza shughuli za kiuchumi katika maeneo yao.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: