Articles by "MSIBA"
Showing posts with label MSIBA. Show all posts

Dar es Salaam, Machi 30, 2026 — Chama cha ACT Wazalendo kimetangaza kwa masikitiko makubwa kifo cha aliyekuwa mwanachama wake, Ndugu Seleman Bungara maarufu kama Bwege, kilichotokea ghafla alipokuwa akipatiwa matibabu hospitalini.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Kiongozi wa Chama hicho, Dorothy Semu, marehemu Bungara alifariki dunia wakati akiwa hospitali alipokwenda kupata huduma ya kusafisha figo (dialysis).

Chama hicho kimetoa pole za dhati kwa familia ya marehemu, hususan kwa mjane wake Bi. Mwanawetu Said Zarafi, pamoja na ndugu, jamaa na marafiki walioguswa na msiba huo mzito.

ACT Wazalendo imemkumbuka marehemu Bungara kama mwanasiasa wa upinzani aliyekuwa jasiri na aliyejitolea kupigania haki, demokrasia na ustawi wa wananchi katika maisha yake yote.

Aidha, chama hicho kimeeleza kushiriki kikamilifu katika msiba huo kwa kuchangia hali na mali, ikiwemo kugharamia mazishi ya marehemu. Pia kimewaomba wanachama wake, hususan kutoka Kanda ya Kilwa Kusini, kujitokeza kwa wingi kushirikiana na familia katika kipindi hiki kigumu.

“Tunaungana na familia ya marehemu katika kipindi hiki cha majonzi, na tunaomba Mwenyezi Mungu aipokee roho ya marehemu mahali pema peponi,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Kifo cha Bungara kimeacha pengo kubwa ndani ya chama hicho na kwa wanasiasa wa upinzani nchini, huku akitarajiwa kukumbukwa kwa mchango wake katika harakati za kisiasa na kijamii.

Na Mwandishi Wetu

Rais wa Kenya, William Ruto, ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Mbunge wa Jimbo la Ol Kalou, David Njuguna Kiaraho, akieleza kusikitishwa kwake na msiba huo alioutaja kuwa pigo kubwa kwa taifa.

Kupitia ujumbe wake, Rais Ruto amesema mawazo na maombi yake yako pamoja na familia ya marehemu, marafiki pamoja na wananchi wa Ol Kalou katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.

Akimzungumzia marehemu Kiaraho, Rais Ruto alimtaja kuwa kiongozi mnyenyekevu, thabiti na mwenye maono, aliyekuwa nguzo muhimu kwa jamii yake kutokana na kujitolea kwake kuwatumikia wananchi wake kwa dhati.

Aliongeza kuwa marehemu atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika sekta ya elimu pamoja na utumishi wake uliotukuka ndani ya Bunge la Taifa, ambako alisimamia maslahi ya wananchi wake kwa uadilifu.

Rais Ruto pia alibainisha kuwa maisha ya marehemu ni funzo kwa viongozi wa kizazi cha sasa, akiwahimiza kuweka mbele huduma kwa wananchi badala ya siasa zisizo na tija, huku akisisitiza umuhimu wa kuendeleza kaulimbiu yake ya “Kazi Kwanza, Siasa Baadaye.”

Amehitimisha kwa kutoa pole na kumuombea marehemu apumzike kwa amani, huku taifa la Kenya likiendelea kuomboleza kiongozi huyo aliyegusa maisha ya wengi.

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.


Mhe. Lukuvi amefariki dunia tarehe 25 Machi, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Mkoani Dodoma
Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Jaji Joseph Sinde Warioba akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mama Anna Mkapa akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Jaji Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa George Masaju akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tano, Hayati John Pombe Magufuli... Mama Janeth Magufuli akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Kiongozi Mheshimiwa Balozi Moses Kusiluka akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Kassim Majaliwa akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob Mkunda akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Hamza Johari akisaini kitabu cha maombolezo katika ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge,Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu Mhe. William Lukuvi katika Viwanja vya Karimjee leo tarehe 28 Machi, 2026 Jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Viongozi mbalimbali wa kitaifa na serikali wamejitokeza kwa wingi katika viwanja vya Karimjee Hall kushiriki ibada ya kumuombea na kuuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), William Lukuvi, huku wakisaini kitabu cha maombolezo kuonesha heshima zao za mwisho.

Miongoni mwa viongozi waliohudhuria ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete, aliyesaini kitabu hicho akiambatana na mkewe Salma Kikwete, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mchinga.

Pia, Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla, alijitokeza na kusaini kitabu hicho, akifuatiwa na Waziri Mkuu Mstaafu Joseph Warioba.

Wengine waliotoa heshima zao ni pamoja na Mama Anna Mkapa, Jaji Mkuu wa Tanzania George Masaju, pamoja na Mama Janeth Magufuli.

Aidha, Katibu Mkuu Kiongozi Moses Kusiluka, Waziri Mkuu Mstaafu Kassim Majaliwa, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jacob Mkunda, na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Hamza Johari, nao walifika na kusaini kitabu cha maombolezo.

Ibada hiyo imefanyika leo Machi 28, 2026, ikiwa ni sehemu ya shughuli za kitaifa za kuaga mwili wa kiongozi huyo aliyefariki dunia Machi 25, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa alipokuwa akipatiwa matibabu.

Katika salamu zao, viongozi hao walimwelezea marehemu Lukuvi kama kiongozi aliyekuwa na mchango mkubwa katika utumishi wa umma, hususan katika kusimamia sera na uratibu wa shughuli za serikali pamoja na kutetea maslahi ya watu wenye ulemavu.

Umati mkubwa wa wananchi nao umejitokeza kushiriki katika maombolezo hayo, wakionesha upendo na heshima kwa kiongozi huyo aliyewahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini.

Ratiba ya mazishi inaendelea kuratibiwa na serikali, huku Watanzania wakiendelea kuomboleza kifo cha mmoja wa viongozi waliotumikia taifa kwa muda mrefu.

Na Mwandishi Wetu.

Dodoma — Serikali imetangaza rasmi kifo cha aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Jimbo la Isimani, William Vangimembe Lukuvi, kilichotokea leo Machi 25, 2026.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa kwa umma, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa kiongozi huyo amefariki dunia majira ya saa moja asubuhi akiwa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu kufuatia ugonjwa wa mshtuko wa moyo.

Katika taarifa hiyo, Rais Samia ameeleza kusikitishwa na msiba huo mzito, akitoa pole kwa Spika wa Bunge, familia ya marehemu, wananchi wa Jimbo la Isimani pamoja na Watanzania wote kwa ujumla.

“Kifo cha Mheshimiwa Lukuvi ni pigo kubwa kwa Taifa, kutokana na mchango wake mkubwa katika uongozi na utumishi wa umma,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Marehemu Lukuvi alihudumu katika nyadhifa mbalimbali za uongozi serikalini kwa muda mrefu, akitambulika kwa uzalendo wake na mchango wake katika maendeleo ya taifa.

Serikali imesema itaendelea kutoa taarifa zaidi kuhusu taratibu za mazishi kadri zitakavyopangwa.

Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Radio EFM na TVE Ndugu Deniss Ssebo, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Ssebo amefariki baada ya kuugua ghafla. Taarifa zaidi zitawajia baadae.

Mwenyezi Mungu Ailaze , Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi . AMEN

Na Mwandishi Wetu.

Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, leo ameweka saini katika kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu la Katoliki la Dar es Salaam, marehemu Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu jijini Dar es Salaam.

Baada ya kuweka saini, Dkt Kikwete alimpa mkono wa pole Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Thaddaeus S. Ruwa’ichi, na kueleza kuwa marehemu Kardinali Pengo atakumbukwa daima kwa mchango wake mkubwa kwa Kanisa na Taifa pamoja na moyo wake wa upendo kwa wananchi na kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Alisema Kardinali Pengo alikuwa rafiki wa wengi na kiongozi aliyegusa maisha ya watu wengi kupitia huduma yake ya kiroho na kijamii.

Aidha, Dkt Kikwete alitoa pole kwa Askofu Mkuu Ruwa’ichi, viongozi na waumini wa Kanisa Katoliki, akiwataka kuwa na subira katika kipindi hiki cha majonzi huku akiungana nao kumuombea marehemu apumzike kwa amani.


Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutoa pole, Rais huyo Mstaafu alisema yeye na marehemu Kardinali Pengo walifahamiana kwa muda mrefu tangu alipokuwa akihudumu wilayani Nachingwea katika kituo chake cha kwanza cha kazi, wakati marehemu akiwa Askofu Mkuu aliyesimamia maeneo ya Tunduru na Lindi.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Thaddaeus S. Ruwa’ichi, alitangaza msiba huo tarehe 19 Februari 2026 saa 04:00 kwa masikitiko makubwa, akieleza kuwa mpendwa baba yetu, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, ameitwa nyumbani kwa Baba wa Milele akiwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa ratiba rasmi ya mazishi, shughuli za kuaga mwili wa marehemu zitaanza siku ya Jumamosi tarehe 28 Februari 2026 kwa kuwasili kwa mwili katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu saa 03:00 asubuhi.

Kuanzia saa 03:15 asubuhi hadi saa 10:00 jioni waombolezaji watapata fursa ya kutoa heshima za mwisho katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu.
Saa 10:00 jioni kutakuwa na Misa Takatifu ya kumuombea marehemu itakayofuatiwa na mkesha wa sala na maombolezo utakaoshirikisha makundi mbalimbali ya kijimbo, wakiwemo watawa, walei pamoja na vyama vya kitume.

Siku inayofuata, yaani Jumapili, mwili wa marehemu utaondoka Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu saa 12:00 asubuhi kuelekea Kituo cha Hija Pugu, na unatarajiwa kuwasili saa 12:45 asubuhi chini ya usimamizi wa Kamati ya Mazishi.

Kuanzia saa 01:00 hadi saa 03:45 asubuhi waombolezaji watapata tena fursa ya kutoa heshima za mwisho katika Kituo cha Hija Pugu.

Misa ya Mazishi itaanza saa 04:00 asubuhi katika Kituo cha Hija Pugu, ikihitimisha rasmi shughuli za mazishi.

Waumini na wananchi wote wanaombwa kushiriki katika ibada na sala hizi kwa utulivu na heshima inayostahili.
Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo alizaliwa tarehe 5 Agosti 1944 na kupadrishwa mwaka 1971.

Alisoma Teolojia ya Maadili katika Chuo Kikuu cha Kipapa cha Lateran mjini Roma, ambako alipata shahada ya uzamivu mwaka 1977. Baadaye alifundisha katika Seminari ya Kipalapala na kuwa Rektor wa kwanza wa Seminari ya Segerea hadi mwaka 1983.

Aliteuliwa kuwa Askofu wa Nachingwea mwaka 1983 na baadaye Askofu wa Jimbo la Tunduru–Masasi mwaka 1985. Mwaka 1990 aliteuliwa kuwa Askofu Mkuu Msaidizi wa Dar es Salaam na mwaka 1992 akawa Askofu Mkuu kamili wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam.

Mwaka 1998 alitangazwa kuwa Kardinali na Papa Yohane Paulo II, na alishiriki katika mikutano ya kumchagua Papa mwaka 2005 na 2013.

Kardinali Pengo alihudumu pia katika idara mbalimbali za Kanisa Katoliki la Roma na kuongoza Baraza la Makanisa Katoliki Afrika (SECAM) tangu mwaka 2007. Alistaafu mwaka 2019, akiacha alama ya uongozi thabiti na imani isiyotetereka.
Na Mwandishi Wetu.

Kanisa Katoliki nchini limeingia katika majonzi kufuatia kifo cha Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu la Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Cardinal Pengo (pichani), kilichotokea leo tarehe 19 Februari 2026 majira ya saa 4:00 usiku. Taarifa rasmi iliyotolewa na uongozi wa jimbo hilo imeeleza kuwa Kardinali Pengo amefariki akiwa nyumbani kwa Baba wa Milele baada ya kuugua kwa muda.

Kwa mujibu wa tangazo hilo, lililotolewa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa'ichi OFMCap, imesema kiongozi huyo wa muda mrefu wa Kanisa Katoliki Tanzania alipata matibabu katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Cardiac Institute kabla ya kifo chake. Uongozi wa Kanisa umeeleza kuwa taarifa zaidi kuhusu taratibu za mazishi na ratiba za ibada zitatolewa baadaye baada ya maandalizi kukamilika.

Kardinali Pengo anakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika uongozi wa kiroho, maadili ya jamii na maendeleo ya Kanisa Katoliki nchini. Alizaliwa mwaka 1944 katika Mkoa wa Tanga na kuanza safari ya wito wa kipadre tangu ujana wake. Alipadrishwa mwaka 1971, kisha akahudumu katika majukumu mbalimbali ya kichungaji na kitaaluma kabla ya kuteuliwa kuwa Askofu wa Nachingwea mwaka 1983. Uongozi wake uliendelea kukua alipochaguliwa kuwa Askofu Mkuu wa Dar es Salaam mwaka 1992, nafasi aliyotumikia kwa muda mrefu akisimamia ukuaji wa Kanisa na taasisi zake.

Mwaka 1998 aliteuliwa kuwa Kardinali na Pope John Paul II, hatua iliyomwingiza katika baraza la juu la Kanisa Katoliki duniani chini ya mamlaka ya Holy See. Kupitia nafasi hiyo, aliwakilisha Tanzania katika majukwaa mbalimbali ya kimataifa ya Kanisa na kushiriki katika mijadala muhimu kuhusu imani, maadili na maendeleo ya jamii.

Katika kipindi chake chote cha uongozi, alijulikana kwa msimamo thabiti katika masuala ya maadili, mshikamano wa kijamii na sauti ya hekima katika mijadala ya kitaifa. Hata baada ya kustaafu uongozi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam mwaka 2019, aliendelea kuwa mlezi wa kiroho na mshauri wa viongozi wa Kanisa pamoja na waumini. Urithi wake unaendelea kubaki katika historia ya Kanisa na taifa kama mfano wa uongozi wa imani, busara na huduma kwa jamii.

Na Mwandishi Wetu.

Serikali imetuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha mwanamuziki mkongwe wa muziki wa bendi, Steven Hiza, kilichotokea jijini Tanga, huku Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akimuelezea marehemu huyo kuwa msanii mahiri aliyeacha alama kubwa katika tasnia ya muziki na jamii kwa ujumla.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Rais Samia alimtuma salamu hizo kupitia Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, akisisitiza kuwa mchango wa marehemu katika kuelimisha, kuburudisha na kuhamasisha jamii kupitia sanaa hautasahaulika. Alibainisha kuwa Hiza alitumia muziki kama chombo cha kuimarisha maadili, umoja na uzalendo miongoni mwa Watanzania.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa marehemu aliwahi kulitumikia kundi la muziki la Atomic Jazz Band, ambapo alijipatia umaarufu mkubwa kupitia nyimbo zake zilizojaa ujumbe wa uzalendo na mshikamano wa kitaifa, ikiwemo wimbo uliogusa hisia za wengi kuhusu mapenzi ya nchi. Serikali imetambua mchango huo kama sehemu ya historia ya maendeleo ya muziki wa Tanzania.

Rais Samia pia aliwataka wanamuziki na wadau wa sanaa nchini kuuenzi mchango wa marehemu kwa kuendeleza misingi ya ubunifu, uzalendo na uwajibikaji katika kazi zao za kisanaa, akisisitiza kuwa sanaa ni nyenzo muhimu ya kujenga jamii yenye maadili na mshikamano.

Aidha, Rais ametoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa, wanamuziki na Watanzania wote, akiwaombea uvumilivu na moyo wa subira katika kipindi hiki cha maombolezo, huku akimuombea marehemu apumzike kwa amani.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

ALIYEKUWA mfanyakazi wa Kampuni ya Mabasi ya NBS, Mzee Nassor Hamdan Seif (NBS), amefariki dunia leo asubuhi, na kuacha huzuni kwa familia, ndugu, jamaa na wadau mbalimbali wa sekta ya usafirishaji.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na familia na uongozi wa NBS, mwili wa marehemu kwa sasa upo Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam, na unatarajiwa kusafirishwa leo jioni kwa ndege kwenda mkoani Tabora kwa ajili ya mazishi.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa mazishi ya Mzee Nassor Hamdan yatafanyika kesho saa 7 mchana mkoani Tabora, nyumbani kwao, ambapo ndugu, jamaa na marafiki wanatarajiwa kuhudhuria kumpa heshima ya mwisho.

Aidha, Kampuni ya Mabasi ya NBS imetangaza kuweka mabasi maalum kwa ajili ya kusafirisha waombolezaji wanaotaka kwenda Tabora kushiriki mazishi hayo. Mabasi hayo yatakuwa Temeke, jijini Dar es Salaam, na yataondoka leo jioni kuelekea Tabora.

Imesisitizwa kuwa usafiri huo ni bure kwa waombolezaji wote na utahusisha safari ya kwenda na kurudi, ikiwa ni sehemu ya mchango wa NBS katika kuungana na familia ya marehemu katika kipindi hiki cha majonzi.

Familia ya marehemu imewashukuru waombolezaji wote kwa michango, dua na faraja wanayoendelea kutoa, na imetoa wito kwa Watanzania kuendelea kushirikiana katika kumpa marehemu heshima ya mwisho.

Marehemu Nassor Hamdan atakumbukwa kwa mchango wake katika sekta ya usafiri na kwa ushirikiano wake mzuri na jamii aliyokuwa akiishi nayo. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Antiphas Lissu, ametuma ujumbe mzito wa rambirambi kufuatia kifo cha Mwenyekiti Mwanzilishi wa chama hicho, Mzee Edwin Isaac Mbiliewi Mtei, akimtaja kama mjenzi wa taifa, kiongozi wa mfano na hazina ya historia ya Tanzania.

Katika ujumbe wake alioutoa akiwa Gereza Kuu la Ukonga, Lissu amesema kifo cha Mzee Mtei ni pigo kubwa si tu kwa familia yake na wanachama wa CHADEMA, bali kwa taifa lote la Tanzania kutokana na mchango wake mkubwa katika ujenzi wa taifa, uchumi na demokrasia.

Lissu ameeleza kuwa marehemu Mtei alikuwa mmoja wa waasisi wakuu wa misingi ya uchumi wa Tanzania baada ya uhuru, akihudumu kama Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania na baadaye Waziri wa Fedha, ambapo jina na saini yake zilionekana kwenye noti za kwanza kabisa za taifa.

Akizungumzia uadilifu wake, Lissu amesema Mzee Mtei alionesha ujasiri wa kipekee wa kisiasa pale alipothubutu kumshauri Mwalimu Julius Nyerere kubadili sera za kiuchumi za Azimio la Arusha baada ya kubaini kuwa zilikuwa zimeshindwa, na baadaye akaamua kujiuzulu wadhifa wa Waziri wa Fedha kwa misingi ya dhamira na uaminifu kwa nchi.

“Huu ndio uzalendo wa kweli. Mzee Mtei hakutafuta madaraka, bali alisimamia ukweli na maslahi ya taifa,” amesema Lissu katika ujumbe wake.

Kuhusu mchango wake ndani ya CHADEMA, Lissu amesema marehemu alikuwa mfano wa uongozi wa kujitolea, kwani hakuwahi kupokea mshahara, posho wala kunufaika binafsi kupitia nafasi yake ya uongozi ndani ya chama.

Ameongeza kuwa Mtei aliimarisha utamaduni wa uongozi wa kupisha damu changa, alipostaafu uenyekiti wa chama mwaka 1998 akiwa na umri wa miaka 66, jambo linaloendelea kuifanya CHADEMA kuwa chama chenye misingi ya kidemokrasia.

Lissu pia amemsifu marehemu kwa kuchapisha kitabu chake cha maisha “From Goatherd to Governor” mwaka 2009, akisema kitabu hicho kimekuwa hazina muhimu ya historia ya kisiasa na kiuchumi ya Tanzania.

Akihitimisha ujumbe wake, Lissu amesema badala ya kuomboleza kifo cha Mtei, Watanzania wanapaswa kusherehekea maisha yake yenye maana, busara na mchango mkubwa kwa taifa, huku akimuombea apumzike kwa amani.

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania na Makamu wa Kwanza wa Rais wa zamani, Mzee Edwin Isaac Mbiliewe Mtei, aliyefariki dunia usiku wa tarehe 19 Januari, 2026 jijini Arusha.

Kupitia taarifa rasmi iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Rais Samia alisema kifo cha Mzee Mtei ni pigo kubwa kwa taifa kutokana na mchango wake mkubwa katika ujenzi wa uchumi na uongozi wa nchi. Rais alitoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania wote walioguswa na msiba huo.

Rais Samia alimtaja Mzee Mtei kuwa miongoni mwa watumishi na viongozi waliotoa mchango mkubwa katika kuimarisha misingi ya uchumi wa taifa, hususan kupitia nafasi yake kama Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania (1966–1974), ambapo alishiriki katika kuweka mifumo imara ya fedha na taasisi za kifedha nchini.

Aidha, Rais alieleza kuwa marehemu ataendelea kukumbukwa katika historia ya siasa za Tanzania kama mmoja wa waasisi wa demokrasia ya ushindani wa vyama vingi na kiongozi aliyetoa mchango mkubwa ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), akitambuliwa kwa misimamo yake na uadilifu katika uongozi.

Rais Samia pia aliwahimiza Watanzania kuendelea kujifunza kutoka katika maisha na falsafa ya Mzee Mtei, ikiwemo kupitia maandiko yake binafsi (autobiografia), ambayo yanaeleza safari yake ya maisha na mchango wake katika kujenga taifa.

Akihitimisha, Rais aliomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi na kuwapa familia, ndugu na taifa kwa ujumla faraja, nguvu na amani katika kipindi hiki cha majonzi.

Taarifa hiyo imesainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari S. Machumu, na kutolewa rasmi Zanzibar tarehe 20 Januari, 2026.

ZANZIBAR: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametuma salamu za rambirambi kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu, kufuatia kifo cha Mbunge wa Viti Maalum wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Halima Idd Nassor.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, marehemu Halima Idd Nassor amefariki dunia leo Januari 18, 2026, alipokuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili – Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).

Taarifa hiyo imeeleza kuwa mazishi ya marehemu yamefanyika leo Januari 18, 2026 katika eneo la Kigamboni, jijini Dar es Salaam.

Katika salamu zake, Rais Samia ameeleza masikitiko makubwa kwa msiba huo na kusema marehemu alikuwa kiongozi mahiri aliyetoa mchango mkubwa katika maendeleo ya Chama Cha Mapinduzi na Taifa kwa ujumla, hususan kupitia majukumu yake ya kibunge na ndani ya chama.

Rais pia ametoa pole kwa familia ya marehemu, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), wanachama wa CCM, Waheshimiwa Wabunge pamoja na wananchi wote walioguswa na msiba huo.

Aidha, Rais Samia amewaomba Watanzania kuendelea kuwa na subira, mshikamano na kumuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.

Taarifa hiyo imesainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari S. Machumu.
Mwanahabari Joachim Ernest Mushi amefiwa na mama yake mzazi, Mecktilda Joseph Lugazu, aliyefariki dunia Januari 6, 2026, wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya General Jijini Dodoma, tukio lililoacha simanzi kwa familia, ndugu, jamaa na wadau wa tasnia ya habari.

Kwa mujibu wa taarifa za familia, taratibu za msiba zinaendelea kufanyika nyumbani kwa marehemu Kifuru–Kinyerezi jijini Dar es Salaam, ambako waombolezaji wanaendelea kujitokeza kutoa pole na faraja kwa familia iliyopatwa na msiba huo.

Imeelezwa kuwa mwili wa marehemu utasafirishwa kutoka Dodoma kuelekea Uru Mawela, mkoani Kilimanjaro, siku ya Januari 9, 2026, kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika siku inayofuata.

Mazishi ya marehemu Mecktilda Joseph Lugazu yanatarajiwa kufanyika Januari 10, 2026, nyumbani kwao Uru Mawela, huku familia ikitoa shukrani kwa wote wanaoendelea kutoa pole na kuomba dua ili Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.

Dodoma, Tanzania – 12 Desemba 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Mhe. Jenista Joakim Mhagama, kilichotokea jijini Dodoma.

Kupitia taarifa yake, Rais Samia amesema amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba huo mzito na kutoa pole kwa Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu, wananchi wa Jimbo la Peramiho, familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki.

Rais Samia amemuelezea Marehemu Mhagama kama kiongozi shupavu na mtumishi wa umma aliyejitoa kwa moyo wake wote kwa kipindi cha zaidi ya miaka 38 ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Katika safari yake ya kisiasa, Mhagama aliwahi kuwa kiongozi wa vijana, kiongozi wa wanawake, waziri katika awamu mbalimbali za serikali, pamoja na kuwa mshauri wa wanasiasa na wananchi wengi.

“Kwa miaka 38, Mheshimiwa Mhagama amekuwa mwanachama mahiri wa CCM, kiongozi wa vijana, kiongozi wa wanawake, waziri katika awamu mbalimbali na mnasihi wa wengi katika siasa na maisha,” amesema Rais Samia katika salamu zake.

Rais Samia amewaombea wafiwa faraja katika kipindi hiki cha majonzi na kumkabidhi marehemu kwa Mungu, akisema: “Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Amina.”

Mipango ya mazishi inaratibiwa kwa ushirikiano kati ya Serikali, Bunge na familia ya marehemu, na taarifa zaidi zinatarajiwa kutolewa.

Dodoma, 11 Desemba 2025

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limetangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho, Mhe. Jenista Joakim Mhagama, kilichotokea leo jijini Dodoma. Taarifa hiyo imetolewa na Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb), kupitia taarifa rasmi ya Ofisi ya Bunge.

Katika taarifa hiyo, Spika Zungu alieleza kusikitishwa na msiba huo mzito, akisema:

“Kwa masikitiko makubwa, naomba kutangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho, Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama kilichotokea leo 11 Desemba 2025 jijini Dodoma. Natoa pole kwa Waheshimiwa Wabunge wote, familia ya marehemu, ndugu, jamaa na wananchi wa Jimbo la Peramiho. Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu.”

Ofisi ya Bunge imesema kuwa mipango ya mazishi itaendelea kutolewa kwa ushirikiano na familia ya marehemu.

Mhe. Jenista Mhagama alizaliwa tarehe 23 Juni 1967 na amehudumu katika nyadhifa mbalimbali za uongozi nchini, ikiwemo kuwa Mbunge na Waziri katika wizara tofauti.

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina.
Na Mwandishi Wetu - Kilimanjaro.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa moyo wake wa upendo kwa kugharamia mazishi ya miili 42 ya watu waliofariki dunia kufuatia ajali iliyotokea Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro.
Mhe. Nderiananga ametoa shukrani hizo tarehe 03 Julai, 2025 wakati aliposhiriki tukio la kuaga miili 35 katika viwanja vya Hospitali ya Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC) akisema miili Saba ilichukuliwa na ndugu zao na miili miwili bado vipimo vya DNA vinafanyiwa kazi ili kutambulika.
Tukio hilo lilioongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Nurdin Babu ambapo Mhe. Nderiananga alimpongeza kwa kujitoa kwa kiasi kikubwa tangu ilipotokea ajali hiyo akishirikiana na watendaji wake wote.
Amesema Serikali kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa iliyopo Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Kilimanjaro kwa juhudi kubwa zilizofanyika kuokoa manusura wa ajali hiyo pamoja na miili ya walioungua kwa moto mara baada ya ajali kutokea.
Vilevile ameipongeza Serikali kupitia Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa kuchukua sampuli za miili hiyo (DNA) kuhakikisha ndugu wanatambua miili ya wapendwa wao.
Hata hivyo Mhe. Nderiananga ameendelea kutoa pole kwa Serikali, ndugu, jamaa na marafiki kufuatia msiba huo mzito kwa Taifa huku akiwaomba kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu hadi watakapokamilisha kuwahifadhi wapendwa wao.
Aidha, ajali hiyo iliyotokea Juni 28 2025 katika Kitongoji Mahuu, Kata ya Same, takribani kilomita nne kutoka Same mjini, ililihusisha basi kubwa la abiria, Mali ya Kampuni ya Chanel One, lenye namba za usajili T 179 CWL na basi dogo la abiria aina ya Toyota Coaster, lenye namba T 199 EFX linalomilikiwa na Kampuni ya Mwami Trans.

Coaster hiyo, ilikuwa ikitokea Same kuelekea Manispaa ya Moshi, wakati basi la Chanel One lilikuwa likitokea Arusha kuelekea Tanga.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akizungumza na Familia ya Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Mzee Cleopa David Msuya (hawapo pichani) alipoitembelea nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akisisitiza jambo kwa Familia ya Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Mzee Cleopa David Msuya (hawapo pichani) alipoitembelea nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi akifafanua jambo kwa Familia ya Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Mzee Cleopa David Msuya (hawapo pichani) wakati Waziri wa Ofisi hiyo, Mhe. George Simbachawene (wa kwanza kulia) alipoitembelea Familia hiyo nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam.
Mtoto wa Hayati Mzee Cleopa David Msuya, Bi. Joyce Msuya Mpanju (aliyenyanyua mikono) akitoa shukrani kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipoitembelea Familia hiyo nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Msaidizi Utawala na Dawati la Viongozi wa Kitaifa Wastaafu, Bi. Nyasinde Mukono akifafanua jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (wa pili kutoka kulia) wakati Waziri huyo alipoitembelea Familia ya Hayati Mzee Cleopa David Msuya nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam. Watatu kutoka kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Xavier Daudi na Wa kwanza kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Bi. Mary Mwakapenda.
Mtoto wa Hayati Mzee Cleopa David Msuya, Bw. Job Msuya (katikati) akizungumza jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipoitembelea Familia hiyo nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiwa katika picha ya pamoja na Familia ya Hayati Mzee Cleopa David Msuya wakati alipoitembelea nyumbani kwao Upanga Jijini Dar es Salaam. Wengine ni Viongozi na Watendaji wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI.

Na. Mwandishi Wetu-Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ametoa wito kwa Watanzania kumuenzi aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Mzee Cleopa David Msuya kwa kuendelea kudumisha umoja, amani na mshikamano na kuyaenzi mazuri yote aliyoyafanya enzi za uhai wake.

Mhe. Simbachawene ameyasema hayo leo tarehe 22 Mei, 2025 alipoitembelea familia ya Hayati Msuya nyumbani Upanga jijini Dar es Salaam.

Mhe. Simbachawene amesema Hayati Mzee Msuya atakumbukwa kwa kuwagusa watu wengi kwa namna alivyokuwa na upendo, kuwasaidia watu wengi pamoja na kuhamasisha maendeleo katika maeneo mbalimbali nchini.

Aidha, Mhe. Simbachawene amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwathamini Viongozi Wakuu wa Kitaifa Wastaafu kwa mujibu wa Sheria.

Akiongea kwa niaba ya familia, mtoto wa Hayati Msuya, Bi. Joyce Msuya-Mpanju ameishukuru Serikali kwa mchango wake mkubwa na ushirikiano uliotolewa kwa familia hiyo tangu enzi za uhai wa Baba yao alipoanza kuugua hadi umauti ulipomkuta na kusimama bega kwa bega wakati wa msiba mpaka kukamlisha salama taratibu za mazishi yake.

Tunaishukuru sana Serikali kwa kuwa pamoja na familia yetu tangu Mama alipofariki mmekuwa na Baba bega kwa bega, hii ilisaidia sana hata kumfanya Baba aishi maisha marefu maana tunaelewa mtu anapofiwa na Mwenza hali inavyokuwa. Mhe. Waziri tunaomba utufikishie salamu zetu kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samila Suluhu Hassan, Viongozi wote wa Serikali na Ofisi unayoiongoza kwa upendo mliotuonesha kwetu, Bi. Joyce ameongeza.

Hayati Cleopa Msuya alifariki dunia tarehe 7 Mei, 2025 na kuzikwa nyumbani kwake Kijiji cha Chomvu, Usangi Wilayani Mwanga Mkoani Kilimanjaro tarehe13 Mei, 2025.
Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan awaongoza Watanzania kwenye maziko ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Mzee Cleopa David Msuya katika Kijiji cha Chomvu, Usangi Wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro.




















Matukio mbalimbali kwenye mazishi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Mzee Cleopa David Msuya katika Kijiji cha Chomvu, Usangi Wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro tarehe13 Mei, 2025.












Viongozi mbalimbali pamoja na waombolezaji wakiwa kwenye Ibada maalum ya mazishi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Mzee Cleopa David Msuya katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mwanga, Usharika wa Usangi kivindu, wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro tarehe13 Mei, 2025.