Articles by "HABARI PICHA"
Showing posts with label HABARI PICHA. Show all posts
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Rabia Hussein Mohamed kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Dkt. Yose Joseph Mlyambina kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Immaculata Kajetan Banzi kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Cyprian Phocas Mkeha kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Yohane Bokobora Masara kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Dkt. Juliana Laurent Masabo kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Abdi Shaaban Kagomba kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Ibrahim Mzee Ibrahim kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya Rufani wakiapa Kiapo cha Maadili kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwaapisha Majaji 9 wa Mahakama ya Rufani, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha na Majaji wa Mahakama ya Rufani, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 26 Mei, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) Gilead Teri (kulia), Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 16 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 16 Mei, 2026.

Nairobi, Kenya — Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameshiriki katika ufunguzi wa Mkutano wa Ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa (Africa Forward: Africa–France Partnership for Innovation and Growth Summit) unaofanyika jijini Nairobi, Kenya, ambapo viongozi wa nchi za Afrika na Ufaransa wamekutana kujadili mustakabali wa ushirikiano wa kiuchumi, kijamii na kiteknolojia.

Mkutano huo umehudhuriwa na Wakuu wa Nchi na Serikali, viongozi wa sekta binafsi, taasisi za kimataifa, wadau wa maendeleo na wawekezaji kutoka pande zote mbili, ukiwa na lengo la kuimarisha ushirikiano katika sekta muhimu ikiwemo biashara, teknolojia, nishati, afya, kilimo, Akili Unde (AI), uchumi wa buluu pamoja na viwanda. Majadiliano hayo yanalenga kuharakisha maendeleo endelevu na kuongeza fursa za ajira hususan kwa vijana na wanawake barani Afrika.

Akizungumza baada ya ufunguzi wa mkutano huo, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mkutano huo ni muhimu kwa Afrika na Ufaransa kwa pamoja kutokana na nafasi ya majadiliano yanayolenga kuimarisha manufaa ya pande zote mbili kupitia ushirikiano wa kiuchumi na uwekezaji. Amesema Afrika ina rasilimali nyingi ambazo zikitumika vizuri zinaweza kuchochea maendeleo makubwa ya kiuchumi na kijamii.

Ameongeza kuwa lengo kuu la ushirikiano huo ni kupambana na umasikini na kuongeza ajira kwa makundi mbalimbali, hususan vijana na wanawake ambao ndio nguvukazi kubwa ya bara la Afrika. Aidha, Dkt. Mwigulu amesema maeneo mengi yaliyojadiliwa katika mkutano huo yanalingana moja kwa moja na vipaumbele vya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050, jambo linaloonesha muunganiko wa ajenda za kikanda na kitaifa katika kukuza uchumi.


Kwa upande wake, Rais wa Jamhuri ya Kenya, Dkt. William Samoei Ruto, amesisitiza umuhimu wa nchi za Afrika kuimarisha mifumo ya kiuchumi kwa kutumia rasilimali za ndani, kuongeza uwekezaji na kuimarisha ushirikiano wa kikanda. Amesema ni wakati wa Afrika kubadilika na kujiona kama mdau muhimu katika uchumi wa dunia badala ya kuwa mtazamaji au mnufaika wa misaada pekee.

Rais Ruto amesema Afrika inapaswa kuwa na sauti yenye nguvu katika maamuzi ya kimataifa ya kiuchumi, akisisitiza kuwa baadhi ya mifumo ya sasa ya dunia haijazingatia usawa wa ushiriki wa mataifa ya Afrika. Amesema mshikamano wa Afrika ndio utakaowezesha bara hilo kufikia maendeleo ya muda mrefu na yenye tija.

Kwa upande wake, Rais wa Jamhuri ya Ufaransa, Emmanuel Macron, amesema Afrika ni bara lenye fursa kubwa na linaloendelea kwa kasi katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kiteknolojia. Amesema Afrika si bara linalosubiri majibu ya changamoto bali ni sehemu inayotoa suluhisho la changamoto zake kupitia ubunifu na uwekezaji.



Katika hotuba yake, Rais Macron ametangaza mpango wa uwekezaji wa dola za Marekani bilioni 27 barani Afrika, utakaolenga sekta za nishati, Akili Unde (AI), kilimo na uchumi wa bahari. Amesema uwekezaji huo unatarajiwa kuchochea uanzishwaji wa ajira takribani 250,000 barani Afrika na nchini Ufaransa, hatua inayolenga kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kati ya pande hizo mbili.

Aidha, Rais Macron amewataka wafanyabiashara wa Afrika kutumia fursa zilizopo nchini Ufaransa kuwekeza, akisisitiza kuwa ushirikiano wa kweli unapaswa kuwa wa pande mbili. Amesema “ushirikiano wa kisasa hauwezi kuwa wa upande mmoja bali ni wa kushirikiana na kunufaika kwa pamoja.”

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, amesisitiza umuhimu wa kuhakikisha wananchi wa Afrika ndio wanakuwa wa kwanza kunufaika na rasilimali za bara lao. Amesema Afrika imejaliwa utajiri mkubwa wa rasilimali ambazo zikitumika ipasavyo zinaweza kuleta mabadiliko makubwa ya kiuchumi na kijamii.

Mkutano huo unatarajiwa kuendelea kwa siku kadhaa ukiwa na mijadala mbalimbali ya kimkakati kuhusu uwekezaji, teknolojia, nishati safi, ubunifu na maendeleo ya binadamu, huku ukilenga kuweka msingi mpya wa ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa kwa mustakabali wa maendeleo endelevu. 

Na Mwandishi Wetu.

Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), leo tarehe 7 Mei, 2026 limefanya kikao na wadau wa ujenzi wa meli jijini Mwanza kwa lengo la kuhamasisha uwekezaji katika ujenzi wa meli na vyombo vingine vya majini nchini ili kusaidia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Akizungumza wakati alipokutana na ujumbe huo, uliongozwa na Wakili Leticia Mutaki, Mkurugenzi wa Udhibiti, Ulinzi, Usalama na Utunzaji wa Mazingira ya Usafiri Majini, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Saidi Mtanda, aliipongeza TASAC kwa kuitisha kikao hicho akisema kuwa kimekuja wakati muafaka kutokana na umuhimu wa sekta ya usafiri majini katika maendeleo ya Mkoa wa Mwanza na Taifa kwa ujumla.
Mhe. Mtanda alisema Mkoa wa Mwanza upo tayari kushirikiana na TASAC katika kuhamasisha uwekezaji kwenye sekta ya ujenzi wa meli kwa kuwa Mwanza ni lango kuu la usafiri majini katika Ukanda wa Ziwa Victoria na kuwa na meli bora kutasaidia kuimarisha usalama wa usafiri majini.

Aliongeza kuwa zaidi ya asilimia 53 ya eneo la Mkoa wa Mwanza ni maji, hali inayodhihirisha umuhimu wa sekta hiyo kwa uchumi wa mkoa.

Kwa upande wake, Wakili Mutaki akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TASAC alisema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeendelea kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji na kuhimiza maendeleo ya uchumi wa buluu pamoja na viwanda vya ndani kupitia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Wakili Mutaki aliongeza kuwa TASAC itaendelea kuhamasisha sekta binafsi kuwekeza katika ujenzi wa meli na vyombo vya majini nchini ili kupunguza utegemezi wa kuagiza vyombo hivyo kutoka nje ya nchi, hatua ambayo pia itasaidia kupunguza matumizi ya fedha za kigeni.

Wadau waliohudhuria kikao hicho ikiwemo kampuni za Songoro Marine, Ankola Shipyard Co. Ltd, na Mkombozi Marine waliishukuru TASAC kwa kuandaa kikao hicho na kueleza kuwa kimewapa fursa ya kutambua maeneo mbalimbali ya uwekezaji katika ujenzi wa meli  pamoja na umuhimu wa kushiriki katika maendeleo ya uchumi wa buluu nchini.

Na Mwandishi Wetu, Kibaha-Pwani.

Imeelezwa kuwa Tume ya Taifa ya Mipango imekamilisha nyenzo zote za utekelezaji wa Dira 2050 ambazo ni Mpango Elekezi wa Maendeleo wa Muda Mrefu 2026/2027–2050/2051 (LTPP 2050), Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2026/27 – 2030/31 (FYDP IV) na Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2026/2027 kuelekea Julai 1, 2026 ambapo utekelezaji wa Dira hiyo utaanza rasmi.

Hayo yameelezwa leo Mei 4, 2026 na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt. Tausi Kida alipofungua mafunzo kwa Wakurugenzi wa Sera na Mipango, Wakurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini, na Wakuu wa Idara na Vitengo vya Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali yanayofanyika katika Chuo cha Uongozi Mwalimu Julius Nyerere, Kibaha - Pwani.

Dkt. Kida amewaambia washiriki wa mafunzo hayo kuwa, baada ya kukamilisha Dira 2050 na nyenzo zake, mafunzo hayo ni utekelezaji wa mkakati mahususi wa Serikali wa kujipanga kufanya utekelezaji wa Dira hiyo kwa kuhakikisha kunakuwepo na uelewa wa pamoja na utekelezaji unaolingana katika ngazi zote za Wizara, Taasisi za Serikali, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa katika kuhakikisha mipango ya Kitaifa inatekelezwa kwa tija.

“ Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Mipango inakamilisha Miongozo ya Upangaji (NPGs), Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Programu na mirado ya Maendeleo (NF-MEDeP) na Mfumo wa Kidigitali uitwao E-Delivery. Mfumo huu na miongozo hiyo italetwa kwenu na mafunzo stahiki yanaandaliwa kwa ajili yenu” Amesisitiza Dkt. Kida.

Aidha, Dkt. Kida amesema kupitia mafunzo hayo, washiriki watapata fursa ya kujifunza kwa vitendo (i.e. case studies), kubadilishana uzoefu, na kujenga uwezo katika hatua zote za mzunguko wa miradi ya maendeleo kuanzia uibuaji, upangaji, uchambuzi, uidhinishaji hadi utekelezaji na ufuatiliaji.