NaDodoma, Machi 31, 2026 — Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ngwaru Jumanne Maghembe, amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa wawekezaji kutoka kampuni ya Liaoning Fangda wanaotaka kuwekeza nchini Tanzania.
NaDodoma, Machi 31, 2026 — Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ngwaru Jumanne Maghembe, amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa wawekezaji kutoka kampuni ya Liaoning Fangda wanaotaka kuwekeza nchini Tanzania.
Rais wa Kenya, William Ruto, ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Mbunge wa Jimbo la Ol Kalou, David Njuguna Kiaraho, akieleza kusikitishwa kwake na msiba huo alioutaja kuwa pigo kubwa kwa taifa.
Kupitia ujumbe wake, Rais Ruto amesema mawazo na maombi yake yako pamoja na familia ya marehemu, marafiki pamoja na wananchi wa Ol Kalou katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.
Akimzungumzia marehemu Kiaraho, Rais Ruto alimtaja kuwa kiongozi mnyenyekevu, thabiti na mwenye maono, aliyekuwa nguzo muhimu kwa jamii yake kutokana na kujitolea kwake kuwatumikia wananchi wake kwa dhati.
Aliongeza kuwa marehemu atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika sekta ya elimu pamoja na utumishi wake uliotukuka ndani ya Bunge la Taifa, ambako alisimamia maslahi ya wananchi wake kwa uadilifu.
Rais Ruto pia alibainisha kuwa maisha ya marehemu ni funzo kwa viongozi wa kizazi cha sasa, akiwahimiza kuweka mbele huduma kwa wananchi badala ya siasa zisizo na tija, huku akisisitiza umuhimu wa kuendeleza kaulimbiu yake ya “Kazi Kwanza, Siasa Baadaye.”
Amehitimisha kwa kutoa pole na kumuombea marehemu apumzike kwa amani, huku taifa la Kenya likiendelea kuomboleza kiongozi huyo aliyegusa maisha ya wengi.
Na Mwandishi Wetu -Narok, Kenya.
Rais wa Kenya, William Ruto, amempongeza mwanasiasa David Keter maarufu kama Dollarline kwa kushinda katika kura za mchujo za chama cha United Democratic Alliance (UDA) katika Jimbo la Emurua Dikirr Constituency.
Kupitia ujumbe wake, Rais Ruto alimpa pongezi Keter kufuatia ushindi huo muhimu uliompa tiketi ya kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mdogo ujao wa jimbo hilo.
Aidha, Rais Ruto alimpongeza pia mpinzani wake Bernard Ng'eno maarufu kama Buluu kwa kuendesha kampeni imara, akieleza kuwa ushindani huo umeimarisha misingi ya demokrasia ndani ya chama hicho kuanzia ngazi za chini.
“Tunapongeza ushindani wa haki na wa kidemokrasia uliofanyika, ambao unaimarisha chama chetu na kuonesha mshikamano wa wanachama,” ilieleza sehemu ya ujumbe wa Rais Ruto.
Rais huyo alisisitiza kuwa baada ya mchakato wa mchujo kukamilika, ni muhimu kwa wanachama wote wa UDA kuungana na kumuunga mkono mgombea aliyepitishwa ili kuhakikisha ushindi katika uchaguzi mdogo.
“Tunakwenda mbele kama timu moja imara, tukiwa tumeungana nyuma ya mgombea wetu na ajenda ya chama,” aliongeza.
Ushindi wa Keter unatarajiwa kuongeza ushindani mkali katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo, huku chama cha UDA kikilenga kuimarisha nafasi yake kisiasa katika Kaunti ya Narok na maeneo ya jirani.


Aliongeza kuwa Austria itaendelea kutoa ufadhili wa masomo kwa Watanzania pamoja na kuendeleza ushirikiano na Arusha Technical College (ATC), ikiwa ni sehemu ya Mkakati wa Afrika wa Austria (2026–2029).Hatua hiyo inaonesha dhamira ya nchi hizo mbili kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi, sambamba na kukuza maendeleo endelevu kupitia sekta za umma na binafsi.
Klabu ya Simba SC imefanikiwa kumbakisha kiungo wake mahiri, Elie Mpanzu, baada ya kusaini mkataba mpya wa miaka miwili kuendelea kuitumikia timu hiyo.
Hatua hiyo imepokelewa kwa furaha kubwa na mashabiki wa klabu hiyo, wakieleza kuwa kuendelea kubaki kwa nyota huyo wa kimataifa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ni faraja kubwa kuelekea misimu ijayo.
Wadau wa soka nchini pia wamempongeza Rais wa klabu hiyo, Mohammed Dewji, kwa juhudi zake katika kuhakikisha mchezaji huyo muhimu anaendelea kubaki ndani ya kikosi hicho.
Mpanzu amekuwa miongoni mwa wachezaji tegemeo ndani ya Simba SC, akionesha kiwango cha juu katika safu ya kiungo na kuchangia mafanikio ya timu hiyo katika mashindano ya ndani na kimataifa.

Uongozi wa Simba umeeleza kuwa kuendelea kumbakisha mchezaji huyo ni sehemu ya mkakati wa kuijenga timu imara itakayoweza kushindana katika ngazi ya juu zaidi, ikiwemo mashindano ya kimataifa barani Afrika.Kwa upande wao, mashabiki wameonesha matumaini kuwa uwepo wa Mpanzu utaongeza nguvu katika kikosi hicho na kusaidia timu kufikia malengo yake ya kutwaa mataji makubwa msimu ujao.
Kuongezwa kwa mkataba huo ni ishara ya dhamira ya Simba SC kuendelea kuwekeza kwa wachezaji bora na kudumisha ushindani katika soka la Tanzania na Afrika kwa ujumla.
Ujumbe wa Benki ya Stanbic Tanzania uliohudhuria hafla ya utoaji Tuzo za Euromoney Private Banking Awards 2026 zilizofanyika jijini London, Uingereza mwishoni mwa wiki.
Na Mwandishi Wetu.
Benki ya Stanbic Bank Tanzania imeendelea kuthibitisha ubora wake katika sekta ya fedha baada ya kutwaa tuzo tatu za kimataifa kutoka Euromoney, zikiwemo Benki Bora ya Kimataifa kwa Wateja Maalum, Benki Bora kwa Kizazi Kijacho na Benki Bora kwa Huduma kwa Wateja.
Tuzo hizo zilitangazwa katika hafla ya Euromoney Private Banking Awards 2026 iliyofanyika jijini London, kufuatia tathmini ya kina iliyofanywa na jopo huru la wataalamu wa sekta ya fedha duniani.
Mafanikio hayo yanaifanya Stanbic kuwa miongoni mwa taasisi zinazoongoza katika kutoa huduma za kifedha zilizoandaliwa mahsusi kwa wateja, huku ikitambuliwa kwa mara ya pili mfululizo kama benki bora ya kimataifa kwa wateja maalum.
Akizungumzia tuzo hizo, Mtendaji Mkuu wa benki hiyo, Manzi Rwegasira, alisema mafanikio hayo yanaakisi mabadiliko ya namna mali zinavyosimamiwa nchini, hasa katika mazingira ya uchumi unaokua.
“Kadri uchumi wa Tanzania unavyoendelea kukua, wateja wanahitaji mipango madhubuti ya kulinda na kurithisha mali zao kwa vizazi vijavyo. Haya ndiyo maeneo tunayoyawekea nguvu kubwa,” alisema.
Kwa mujibu wa Benki Kuu ya Tanzania, uchumi wa nchi unatarajiwa kukua kwa kati ya asilimia 5 hadi 6, hali inayochochea ongezeko la ukwasi hasa kwa wajasiriamali na biashara za kifamilia.
Tuzo ya Benki Bora kwa Kizazi Kijacho imeangazia juhudi za Stanbic katika kuwaandaa vijana na warithi kusimamia mali kwa uwajibikaji, wakati tuzo ya Huduma kwa Wateja ikitambua ubora wa ushauri wa kifedha unaotolewa kwa wateja kwa kuzingatia mahitaji yao ya muda mrefu.
Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi na Maalum, Omari Mtiga, alisema benki hiyo inalenga kujenga mahusiano ya muda mrefu na wateja wake kwa kuelewa mahitaji yao ya kifamilia na kibiashara.
Naye Kaimu Mkuu wa Idara ya Huduma kwa Wateja Maalum, Beatrice Kisoka, alibainisha kuwa wateja wengi sasa wanazingatia zaidi uendelevu wa mali zao na mchango wake kwa vizazi vijavyo.
“Wateja wanahitaji zaidi ya mafanikio ya sasa; wanataka kuona uthabiti na mwendelezo wa mali zao kwa muda mrefu,” alisema.
Mafanikio hayo yanaongezea hadhi ya benki hiyo ambayo pia ilitambuliwa kama benki bora nchini Tanzania mwaka 2025 na jarida la The Banker, hatua inayodhihirisha uthabiti wake katika kutoa huduma bora za kifedha.

.jpeg)

Na Mwandishi Wetu.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalum), Prof. Palamagamba J. Kabudi amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Botswana, Mhe. Dkt.Phenyo Butale, jijini London, Uingereza, ambapo viongozi hao wamejadili namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya nchi zao.
Mazungumzo hayo yalifanyika pembezoni mwa mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola uliofanyika Machi 8, 2026 jijini London, ukiwaleta pamoja mawaziri kujadili masuala ya kimataifa na maendeleo ya pamoja.

Kwa upande wake, Waziri Kombo aliishukuru United Nations kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuimarisha taasisi za kitaifa na kulinda amani na utulivu wa nchi. Alibainisha kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na jumuiya ya kimataifa katika kuboresha utawala wa kidemokrasia na kuendeleza mshikamano wa kitaifa.
Waziri huyo pia alieleza kuhusu mpango mpana wa kitaifa uliozinduliwa Januari 2026 chini ya kaulimbiu ya “Repair – Rebuild – Renew”, unaolenga kuimarisha utawala wa sheria, demokrasia na mshikamano wa wananchi.
Katika ziara yake nchini, Onanga-Anyanga anatarajiwa pia kukutana na viongozi wa vyama vya siasa ikiwemo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ACT-Wazalendo, Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMA) na Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na kufanya mazungumzo na viongozi wa mihimili mingine ya dola ili kujadili namna bora ya kuendeleza maridhiano ya kitaifa na kuimarisha demokrasia nchini.















.jpeg)

.jpeg)






























