Articles by "MAMA SAMIA SULUHU"
Showing posts with label MAMA SAMIA SULUHU. Show all posts

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) Gilead Teri (kulia), Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 16 Mei, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 16 Mei, 2026.





Ujumbe wa Tanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassanakiwa kwenye mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Africa CDC), Dkt. Jean Kaseya pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 13 Mei, 2026. 



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Africa CDC), Dkt. Jean Kaseya pamoja na Ujumbe wake Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 13 Mei, 2026.

Na Mwandishi Wetu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amekutana na kufanya mazungumzo na Jean Kaseya, Mkurugenzi Mkuu wa Africa CDC pamoja na ujumbe wake, Ikulu jijini Dar es Salaam, ambapo viongozi hao walijadili masuala mbalimbali kuhusu afya ya uzazi, mama na mtoto barani Afrika.

Katika mazungumzo hayo, Dkt. Kaseya alisema Africa CDC ina dhamira ya kushirikiana na Rais Samia ambaye ni Kinara wa Umoja wa Afrika katika Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto, pamoja na Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Afya, kwa lengo la kuimarisha huduma za afya katika sekta hiyo muhimu.

Alisema ushirikiano huo unalenga kuongeza juhudi za kupunguza vifo vinavyotokana na uzazi na kuboresha huduma za afya kwa mama na watoto katika nchi mbalimbali za Afrika.

Dkt. Kaseya alieleza kuwa Tanzania imeonyesha mafanikio makubwa katika sekta ya afya, hususan katika upatikanaji wa huduma kwa wananchi, jambo ambalo linaweza kuwa mfano kwa nchi nyingine barani humo.

Alibainisha kuwa asilimia 85 ya wananchi nchini Tanzania wanapata huduma za afya ndani ya umbali wa kilomita tano kutoka maeneo wanayoishi, hatua aliyosema inaimarisha ajenda ya Afrika ya usalama wa afya na kujitegemea katika sekta hiyo.

Kwa upande wake, Rais Samia alisema Serikali ya Tanzania ipo tayari kuendelea kushirikiana na Africa CDC katika kuendeleza ajenda ya afya ya mama na mtoto, akisisitiza kuwa utekelezaji wa malengo yaliyowekwa unahitaji mipango madhubuti na uratibu wa karibu.

Aidha, Rais Samia aliiagiza Wizara ya Afya kushirikiana kwa karibu na Africa CDC katika kuratibu na kusimamia utekelezaji wa programu mbalimbali zinazolenga kuimarisha afya ya uzazi, mama na mtoto nchini na barani Afrika kwa ujumla.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni kwenye hafla ya Uapisho wa Rais huyo iliyofanyika katika Viwanja vya Kololo, Kampala nchini humo tarehe 12 Mei, 2026.









Matukio mbalimbali wakati wa Sherehe za Uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni zilizofanyika katika Viwanja vya Kololo, Kampala nchini humo, tarehe 12 Mei, 2026.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Waziri Mkuu wa Tatu wa Uganda Mhe. Rukia Isaya Nakadama mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe nchini humo tarehe 12 Mei, 2026. Rais Dkt. Samia amewasili nchini Uganda kwa ajili ya kuhudhuria Sherehe za Uapisho wa Rais Mteule nchi hiyo, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, zitakazofanyika katika Viwanja vya Kololo Jijini Kampala nchini humo.







Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Uganda kuhudhuria Sherehe za Uapisho wa Rais wa nchi hiyo Mhe. Yoweri Kaguta Museveni tarehe 12 Mei, 2026.









Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewataka vijana nchini kulinda amani na kutokubali kutumika katika vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama na taswira ya nchi.

Rais Dkt. Samia ametoa kauli hiyo leo jirani na Uwanja wa Ndege wa Dodoma, akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam, aliposimamishwa na maelfu ya wakazi wa Dodoma waliokusanyika barabarani kwa ajili ya kumsalimia Kiongozi huyo.

Wananchi hao, wakiwemo vijana, maafisa usafirishaji, wafanyabiashara wadogo, machinga, Mamalishe na Babalishe, walijitokeza wakiwa wamevaa fulana na mabango yenye ujumbe wa “Never Again” (Yasijirudie) sambamba na bendera za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akiupokea ujumbe huo, Rais Dkt. Samia amesema matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea nchini hayapaswi kujirudia kwa kuwa yaliathiri taswira ya Taifa na maisha ya wananchi kwa ujumla, hususan vijana.

“Niwaombe sana vijana, katika miji yenu, katika kazi zenu, katika shughuli zenu zote, ambizaneni yaliyotokea yasijirudie tena, kwani yamelitia doa Taifa letu,” amesema Rais Dkt. Samia, akisisitiza wajibu wa kila Mtanzania kuhakikisha matukio hayo, ambayo si sehemu ya hulka ya Watanzania, hayapewi tena nafasi katika jamii.

Aidha, amewataka vijana kulindana, kuelimishana na kuwa walinzi wa amani katika maeneo yao ya kazi, biashara na shughuli za kila siku, na kuongeza kuwa Serikali itaendelea kusikiliza hoja za wananchi na kufanyia kazi changamoto zinazogusa maisha yao.

Kuhusu mikopo kwa wafanyabiashara wadogo, Rais Dkt. Samia amesema Serikali imeanza hatua za kusimamia zoezi la utoaji wa mikopo kupitia taasisi zaidi za kifedha tofauti na ilivyokuwa awali, ili kuongeza wigo wa upatikanaji wa mitaji kwa vijana na makundi mbalimbali ya wajasiriamali.

Amesema mahitaji ya mikopo kwa vijana ni makubwa, na Serikali itaendelea kuongeza rasilimali kadiri uchumi utakavyoruhusu.

Katika hatua nyingine, Rais Dkt. Samia amesema Serikali itatathmini uwezekano wa kuanzisha soko lingine la wafanyabiashara wadogo mkoani Dodoma, pembezoni mwa Soko la Machinga Complex lililopo sasa, ili kukuza fursa zaidi kwa wajasiriamali, kupunguza msongamano na kuboresha mazingira ya biashara.

Awali, wawakilishi wa wafanyabiashara wadogo walieleza namna Soko la Machinga Complex lilivyo mfano bora wa utekelezaji wa maelekezo ya Serikali kuhusu upangaji wa biashara ndogondogo katika maeneo rasmi, salama na rafiki kwa shughuli za kiuchumi, pamoja na kuomba kuimarishwa kwa huduma za usafiri wa daladala kuingia eneo la soko, uratibu na usimamizi endelevu wa biashara katika maeneo rasmi, na ongezeko la huduma za mikopo kwa wajasiriamali wadogo.

Kwa upande wao, Mamalishe na Babalishe waliwasilisha ombi la kuendelea kuboreshewa masharti ya mikopo ya makundi maalum inayotolewa na Serikali ili makundi zaidi, hasa ya kipato cha chini, yaweze kunufaika.

Nao, Maafisa Usafirishaji wameahidi kuendelea kushirikiana na mamlaka za Serikali katika kulinda amani na kuzuia matumizi mabaya ya vyombo vya usafiri ikiwemo vitendo vya fujo.

Akihitimisha, Rais Dkt. Samia ameagiza viongozi wa Mkoa wa Dodoma kufanyia kazi hoja zilizotolewa na wananchi, na kutaka ripoti ya utekelezaji pindi atakaporejea Dodoma.





























Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameielekeza Ofisi ya Waziri Mkuu kufanyia kazi kwa kina hoja zote zilizowasilishwa na wafanyakazi nchini, zilizotolewa katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika leo.

Rais Samia ametoa maelekezo hayo akiwa Mgeni Rasmi wa maadhimisho hayo yaliyofanyika leo mkoani Njombe, ambapo amesisitiza umuhimu wa serikali kuzipokea na kuzifanyia kazi hoja hizo kwa umakini ili kuendelea kulinda na kuimarisha hadhi, haki na maslahi ya wafanyakazi nchini.

Amesema kuwa wafanyakazi ni nguzo muhimu katika maendeleo ya taifa, hivyo serikali haina budi kuhakikisha changamoto zao zinapatiwa ufumbuzi wa kudumu kwa njia ya majadiliano na utekelezaji wenye tija.

Katika hotuba yake, Rais Samia pia amewataka wafanyakazi kujiandaa kukabiliana na mabadiliko ya dunia ya sasa, ikiwemo mageuzi ya kiuchumi na kiteknolojia ambayo yanaathiri soko la ajira na namna ya utoaji wa huduma kazini.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kudumisha amani, ushirikiano na kuaminiana miongoni mwa wananchi na wafanyakazi, akibainisha kuwa misingi hiyo ndiyo mhimili mkuu wa maendeleo na ustawi wa taifa.

Hata hivyo Rais Samia amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na vyama vya wafanyakazi pamoja na wadau wa ajira nchini ili kuhakikisha changamoto zinazojitokeza kazini zinapatiwa ufumbuzi wa haraka na wa kudumu. Amesema lengo la serikali ni kujenga mazingira bora ya kazi yanayochochea tija, nidhamu na uzalishaji, huku haki za wafanyakazi zikiendelea kulindwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo nchini.

Amesema endapo mshikamano na utulivu vitaendelea kudumishwa, Tanzania itaendelea kuwa nchi salama, yenye maendeleo endelevu na mazingira bora ya kazi kwa wananchi wake wote.


Mwandishi Wetu, DODOMA, Aprili 26, 2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametumia mamlaka yake ya kikatiba kutoa msamaha wa kupunguza adhabu kwa wafungwa 1,369 nchini, ambapo wafungwa 436 wameachiwa huru mara moja huku wengine 933 wakipunguziwa vifungo vyao.

Uamuzi huo umetangazwa leo jijini Dodoma na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobass Katambi, ambaye amesema hatua hiyo ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Katambi amesema msamaha huo umetolewa kwa mujibu wa Ibara ya 45(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayompa Rais mamlaka ya kutoa msamaha kwa wafungwa wanaostahili.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, walionufaika na msamaha huo ni pamoja na wafungwa waliotumikia sehemu ya vifungo vyao kwa mujibu wa sheria, wagonjwa mahututi waliothibitishwa kitaalamu, wazee wenye umri wa miaka 70 na zaidi, pamoja na wanawake wajawazito au wenye watoto wachanga waliopo magerezani.

Aidha, wafungwa waliokuwa wakitumikia adhabu ndefu, wakiwemo waliokaa gerezani kwa miaka 25 na zaidi pamoja na waliokuwa chini ya kizuizi kwa muda mrefu, nao wamejumuishwa baada ya kufanyiwa tathmini maalum.

Hata hivyo, Serikali imeeleza kuwa msamaha huo haukuwahusu wafungwa waliopatikana na hatia ya makosa mazito ikiwemo ugaidi, uharamia, ubakaji, biashara ya binadamu, rushwa, uhujumu uchumi, pamoja na wanaotumikia kifungo cha maisha.

Pia wafungwa waliowahi kunufaika na msamaha wa Rais hapo awali hawakujumuishwa katika orodha ya walionufaika safari hii.

Serikali imesema hatua hiyo inalenga kutoa nafasi ya pili kwa wafungwa waliorekebika ili warejee katika jamii na kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya taifa.

“Ni matarajio ya Serikali kuwa wale walioachiwa huru watarejea katika jamii wakiwa na nidhamu, wakijihusisha na shughuli halali za kiuchumi na kuepuka kurejea kwenye vitendo vya uhalifu,” ilieleza taarifa hiyo.

Hatua hiyo imepokelewa na wananchi kama ishara ya huruma na dhamira ya Serikali ya kuendelea kuimarisha haki, utu na mageuzi ya mfumo wa marekebisho ya tabia nchini.

Wachambuzi wa masuala ya kijamii wanasema msamaha huo pia utasaidia kupunguza msongamano magerezani na kuongeza ufanisi wa huduma za marekebisho.

Maadhimisho ya miaka 62 ya Muungano yanaendelea kuambatana na hatua mbalimbali za kijamii na kiuchumi zinazolenga kuimarisha mshikamano wa kitaifa na ustawi wa wananchi


Na Janeth Raphael MichuziTv .

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu mkubwa wa kundi la Mama na Baba Lishe nchini, akieleza kuwa ni mhimili muhimu katika kuendeleza ustawi wa jamii na uchumi wa taifa.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam katika Kongamano la Kitaifa la Mama na Baba Lishe Tanzania, Rais Samia amesema kundi hilo lina mchango mkubwa katika kuhakikisha wananchi, wakiwemo wafanyakazi, wanafunzi na wasafiri, wanapata huduma ya chakula kwa wakati, jambo linalosaidia kuimarisha shughuli nyingine za kiuchumi na kijamii.

Ameeleza kuwa chakula ni afya, na hivyo Mama na Baba Lishe wanachangia moja kwa moja katika afya na ustawi wa wananchi, hivyo wanastahili kutambuliwa, kuheshimiwa na kulindwa katika shughuli zao za kila siku.

“Shughuli za Mama na Baba Lishe zinapaswa kutambuliwa na kuheshimiwa kwa hadhi inayolingana na mchango wao katika maisha ya kila siku. Hawapaswi kusumbuliwa wala kunyanyaswa,” amesema Rais Samia.



Aidha, amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha inatoa mazingira bora ya kisera na kisheria yatakayowezesha kutambuliwa rasmi kwa kundi hilo, pamoja na kuimarisha mchango wao katika uchumi wa taifa. Amesema hatua hiyo pia inahusisha kuimarisha sekta ya biashara ndogo ndogo kupitia mipango ya urasimishaji na uwezeshaji.

Rais Samia pia amebainisha kuwa Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuweka mikakati mahususi ya kuwawezesha Mama na Baba Lishe, ili waweze kuwa sehemu muhimu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

Katika hotuba yake, alitaja pia uamuzi wa kuunda Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum kama moja ya juhudi za Serikali katika kuhakikisha makundi mbalimbali yakiwemo Mama na Baba Lishe yanapata usimamizi na heshima stahiki.

“Serikali itahakikisha inasimamia heshima yenu na kuendelea kuweka mazingira wezeshi kwa kazi zenu muhimu kwa taifa,” alisisitiza Rais Samia.

Kongamano hilo limewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya chakula na biashara ndogondogo, likiwa na lengo la kujadili changamoto, fursa na njia bora za kuimarisha sekta ya Mama na Baba Lishe nchini.