Na Mwandishi Wetu.

Nairobi, Kenya

Rais wa Kenya, William Ruto, amesema Serikali yake inaendelea kuwawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika mabadiliko ya taifa kupitia uwekezaji mkubwa katika sekta mbalimbali zinazolenga kuongeza ajira, kukuza vipaji na kuimarisha uchumi.

Ruto amesema Serikali imewekeza katika michezo, uchumi wa ubunifu na kidijitali, ajira za nje ya nchi, uwezeshaji wa biashara, makazi nafuu pamoja na maendeleo ya miundombinu, hatua ambazo zimeanza kuzaa matunda kwa kuunda mamilioni ya nafasi za ajira na fursa nyingine kwa vijana.
Amesema katika sekta ya michezo pekee, Serikali inaendelea kujenga na kuboresha viwanja 34 vya michezo nchini ili kusaidia kukuza vipaji vya vijana na kuongeza fursa za maendeleo kupitia michezo.

Kwa mujibu wa Rais huyo, uwekezaji huo umeanza kuleta mafanikio, huku wanamichezo wa Kenya wakiendelea kufanya vizuri katika mashindano ya kimataifa. Pia aliipongeza timu ya taifa ya wasichana wenye umri chini ya miaka 17, Junior Harambee Starlets, kwa kuweka historia ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la FIFA kwa wanawake chini ya miaka 17.
Ruto aliyasema hayo baada ya kuikaribisha Ikulu ya Nairobi timu ya Migori Youth FC, mabingwa wa National Super League msimu wa 2025/26, ambapo aliikabidhi basi maalumu litakalowasaidia kusafiri kwa urahisi katika mechi za ligi nchini kote.

Aidha, alisema Serikali inaendelea kujenga uwanja wa kisasa katika Kaunti ya Migori utakaotumiwa na Migori Youth FC pamoja na jamii kwa ujumla, kwa lengo la kuimarisha mazingira ya kukuza vipaji vya michezo na maendeleo ya vijana nchini Kenya.

Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: