Na Saidi Saidi, WMJJWM – Iringa
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya
Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalum, Felister Mdemu, amewataka
wanawake kushirikiana katika kujikwamua kiuchumi huku wakiendelea
kuthamini familia, malezi bora, kuwaheshimu waume zao na kuhakikisha
watoto wanapata malezi yenye maadili mema.
Mdemu amesema hayo
mkoani Iringa, wakati wa mafunzo ya mwongozo wa uanzishwaji na
uwezeshaji wa majukwaa ya wanawake kiuchumi yaliyofanyika katika Kijiji
cha Kipaduka, Kata ya Uhambingeto, wilayani Kilolo. Mafunzo hayo
yalihusisha madiwani pamoja na viongozi wa majukwaa ya uwezeshaji
wanawake kiuchumi kutoka kata mbalimbali za mkoa huo.
Akizungumzia
umuhimu wa majukwaa hayo, Mdemu amesema ni maono ya Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, yenye lengo
la kuwainua wanawake kiuchumi kupitia elimu ya fedha, ujasiriamali,
matumizi ya teknolojia pamoja na upatikanaji wa mikopo na masoko.
Aidha,
amesisitiza umuhimu wa wanawake kupata taarifa sahihi, kuunganishwa
katika vikundi na kushiriki kikamilifu katika majukwaa hayo ili
wasiachwe nyuma kutokana na ukosefu wa taarifa au usimamizi hafifu. Pia
amewataka madiwani kushirikiana na taasisi za fedha, sekta binafsi
pamoja na wataalam ili kuongeza fursa za kiuchumi kwa wanawake katika
maeneo yao.
Naye Diwani wa Viti Maalum kutoka Tarafa ya Kilolo,
Mheshimiwa Julieth Mkolongo, akizungumza kwa niaba ya madiwani na
viongozi wa majukwaa hayo, amesema wako tayari kutekeleza maelekezo
yaliyotolewa ili kuhakikisha wanawake wanapata fursa za kiuchumi kwa
maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla.
Kwa upande wao, baadhi ya
wanawake walioshiriki mafunzo hayo wamesema elimu waliyoipata
itawasaidia kuendesha vikundi vyao kwa ufanisi, kuongeza kipato pamoja
na kuimarisha ustawi wa familia zao.
Home
HABARI
HABARI NA MATUKIO
HABARI ZA KIJAMII
Mdemu awataka Wanawake kujikwamua Kiuchumi na Kudumisha Malezi Bora
Subscribe to:
Post Comments (Atom)






Toa Maoni Yako:
0 comments: