Leo, Jumamosi ya tarehe 09 Mei 2026, Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Dar es Salaam imefanikiwa kufanya Maadhimisho ya Kilele cha Wiki ya Jumuiya ya Wazazi Mkoa katika Ukumbi wa VETA Kigamboni, yakiongozwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Dar es Salaam, Ndugu Khadija Said.

Maadhimisho hayo yamebeba ujumbe mkubwa wa kuimarisha upendo, mshikamano na malezi bora ndani ya jamii kwa vitendo kupitia shughuli mbalimbali za kijamii na maendeleo ikiwemo:-

Kutembelea watoto wenye mahitaji maalum
Kuchangia damu katika Hospitali ya Kigamboni.
Uzinduzi wa Kigoda cha Wazazi.
Kupanda miti katika Shule ya Dungu.

Wananchi, wazazi na wadau mbalimbali wamejitokeza kushiriki katika shughuli hizo zenye lengo la kujenga jamii bora na yenye maadili mema kwa kizazi cha sasa na kijacho.
Kauli mbiu '“ Malezi Bora na Uzalendo ni Msingi kwa Taifa"













Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: