Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Jerry William Silaa akiagana na Mwenyekiti
Mgeni rasmi Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Jerry William Silaa akiwasili katika Ukumbi wa Hazina, kufungua Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Shirika la Utangazaji la Taifa - TBC na kupokelewa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Stephen Kagaigai na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo Dkt. Ayub Rioba Chacha leo tarehe 20 Septemba, 2024 Jijini Dodoma.

Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Jerry William Silaa akiwa katika picha ya pamoja na makundi mbalimbali ya Wajumbe wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Shirika la Utangazaji la Taifa - TBC kilichofanyika leo tarehe 20 Septemba, 2024 katika Ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma.

Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Jerry William Silaa akiwa katika picha ya pamoja na makundi mbalimbali ya Wajumbe wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Shirika la Utangazaji la Taifa - TBC kilichofanyika leo tarehe 20 Septemba, 2024 katika Ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma.

Picha mbalimbali za wajumbe wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Shirika la Utangazaji la Taifa - TBC kilichofanyika leo tarehe 20 Septemba, 2024 katika Ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma ambapo pamoja na mambo mengine kimemchagua Katibu wa Baraza Bi. Anna Malimbo na Kamati ya maazimio ya baraza hilo.

Picha mbalimbali za wajumbe wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Shirika la Utangazaji la Taifa - TBC kilichofanyika leo tarehe 20 Septemba, 2024 katika Ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma ambapo pamoja na mambo mengine kimemchagua Katibu wa Baraza Bi. Anna Malimbo na Kamati ya maazimio ya baraza hilo.

Na Mwandishi Wetu, WHMTH, Dodoma.

Serikali imelihakikishia Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kwamba inafanya kila linalowezekana kuhakikisha shirika hilo linatekeleza majukumu yake muda wote, na itaendelea kutatua na hatimaye kumaliza changamoto zote zinazolikabili, zikiwemo za kifedha, vifaa na raslimali watu.

Ahadi hiyo ya Serikali imetolewa tarehe 19 Septemba, 2024 na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Jerry Silaa (Mb), wakati akifungua Kikao cha Pili cha Baraza la Wafanyakazi wa TBC kilichofanyika katika Ukumbi wa Kambarage (Hazina) Jijini Dodoma.

"Naomba niwahakikishie kuwa Serikali inafanya kila linalowezekana ili TBC itekeleze majukumu yake muda wote, na Wizara itahakikisha changamoto zote zinazowakabili zinatatuliwa kwa wakati kwani Mkakati wa Serikali ni kuhakikisha mnawezeshwa kifedha, vifaa na raslimali watu ili kutekeleza dhima yake kwa umma wa Watanzania," amesema Mhe. Silaa.

Mhe. Silaa amesema, Serikali inatambua juhudi mbalimbali zinazofanywa na TBC kuhakikisha kunakuwa na fedha za kutosha na kwamba kwa kutambua changamoto za kifedha kwa Shirika, Wizara inasimamia kwa karibu mchakato wa kutungwa kwa Sheria ya TBC, aliyosema, pamoja na mambo mengine, itaiwezesha kupata vyanzo vya mapato vya uhakika, endelevu na toshelevu.

"Waraka wa Sheria hii umeshasomwa kwa mara ya kwanza Bungeni na hatua inayofuata ni kupitishwa na Bunge baada ya kupata maoni ya wadau kama taratibu zinavyoelekeza," amesema Mhe. Silaa.

Aidha, ameipongeza TBC kwa maendeleo makubwa yaliyofikiwa ya kufunga mifumo ya TEHAMA katika miundombinu ya studio za redio na televisheni, upanuzi wa usikivu uliofikia asilimia 92 mwaka huu, na maendeleo ya ujenzi wa Makao Makuu ya TBC eneo la Vikonje Dodoma uliofikia asilimia 26 hadi sasa.

Awali akimkaribisha Waziri, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Stephen Kagaigai amewashauri watanzania kufuatilia maudhui yanayotolewa na Shirika hilo kwani ndicho chombo cha Umma wa Watanzania.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo Dkt. Ayub Rioba Chacha ameishukuru Serikali kwa uwekezaji mkubwa uliofanywa unaowezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi mkubwa licha ya changamoto ndogo ndogo ikiwemo ya upungufu wa watumishi wenye ujuzi kwani waliokuwepo wengi sasa wamefikia umri wa kustaafu.
Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: