NA EMMANUEL MBATILO

KLABU ya Simba imefanikiwa kuinyuka timu ya Primeiro de Agosto Fc kwa mabao 3-1 mchezo ambao ulipigwa kwenye nchini Angola hivyo nakuwa na faida kwa Simba ambaye atasubiri kucheza mchezo wa marudiano ili aweze kufuzu hatua ya makundi.

Simba Sc iimepata mabao kupitia kwa wachezaji wake Clautos Chama, Israel Mwenda pamoja na mshambuliaji wao hatari Moses Phiri.

Simba Sc ilianza kupata bao la kwanza dakika za mwanzo kipindi cha kwanza kupitia kwa kiungo wao Chama na kuwapeleka mapumziko wakiwa mbele kwa bao 1-0.

Bao la timu ya Primeiro de Agosto Fc lilifungwa dakika za lala salama kupitia kwa mkwaju wa penati.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: