Mwenyekiti wa UWT Taifa, Gaudentia Kabaka akizungumza na wandishi wa habari leo kuelekea maadhimisho ya wiki ya UWT itakayofanyika Oktoba 23 Wilayani Rufiji Pwani.
Mwenyekiti wa UWT Taifa, Gaudentia Kabaka akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakary Kunenge kuelekea kilele cha wiki ya UWT kitaifa itakayofanyika Wilayani Rufiji Mkoani Pwani.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakary Kunenge akizungumza na wandishi wa habari Ofisini kwake leo kuelekea wiki ya UWT kitaifa itakayofanyika Wilayani Rufiji.
Charles James, Michuzi TV

RAIS Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) itakayofanyika katika eneo la Ikwiriri Wilayani Rufiji Mkoa wa Pwani Oktoba 23 Mwaka huu.

Akizungumza na wandishi wa habari leo, Mwenyekiti wa UWT Taifa, Gaudentia Kabaka amesema maadhimisho hayo yamepangwa kufanyika Wilayani Rufiji kwa lengo la kuenzi mchango wa Mwenyekiti wa kwanza wa UWT na mpigania Uhuru wa Tanganyika, Bibi Titi Mohamed.

Kabaka amesema ahadi ya kufanyika kwa maadhimisho hayo wilayani Rufiji waliitoa katika kampeni za Urais mwaka 2020 ambapo akiwa na Rais Samia wakati huo akiwa mgombea mwenza waliahidi kumuenzi Bibi Titi ambaye licha ya kuzaliwa Mkoani Dar es Salaam Lakini ni mwenyeji wa Rufiji kwa kufanya maadhimisho hayo wilayani humo.

" Kilele Cha Wiki ya UWT kimelenga kumuenzi Mwanamke Shujaa na mpigania Uhuru wetu, Bibi Titi Mohamed ambaye Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Nyerere alimuona anafaa kumsaidia Kwenye mapambano ya Uhuru na kumchukua kazi ambayo aliifanya kwa weledi na nguvu kubwa.

Lakini pia tumechagua mgeni rasmi awe Rais Samia kwa sababu hii ni mara ya kwanza kupata Rais na Mwenyekiti wa CCM Mwanamke tena akiwa shupavu na Shujaa kama Bibi Titi,"

Ametoa wito kwa Wanawake wote wa Mkoa wa Pwani mikoa jirani na Tanzania kwa ujumla kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho hayo yenye kauli ya " Tushiriki kumkomboa Mwanamke kiuchumi, kifikra na kisiasa,".

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakary Kunenge amemshukuru Mwenyekiti wa UWT Taifa,Gaudentia Kabaka kwa kuridhia maadhimisho hayo kufanyika Mkoani Pwani na hasa katika Wilaya hiyo ya Rufiji kwa lengo la kumuenzi Bibi Titi Mohamed.

"Kama Mkoa tunashukuru kwa kupata fursa hii ya kuwa mwenyeji wa maadhimisho haya ambayo yatachangia kukuza utalii wetu wa ndani na nje kwani itatoa fursa kwa wadau wa utalii kutembelea Wilaya y Rufiji katika kusoma historia ya Bibi Titi Mohamed na kutembelea mnara wake ambao tayari umeshajengwa.

Bibi Titi Mohamed alizaliwa Mkoani Dar es Salaam mwaka 1926 na alikua Mwenyekiti wa kwanza wa UWT na baadaye nafasi hiyo ilishikwa na Sophia Kawawa, Anna Abdallah, Sofia Simba na sasa Gaudentia Kabaka
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: