Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.
 Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta akisaini Kitabu cha wageni, baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akimpigia makofi Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni baada ya kusaini Kitabu cha wageni katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.
 Waziri wa Nishati wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza kwenye mkutano wa Waandishi wa Habari baada ya hafla ya utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga kama Kituo cha Nishati cha Kikanda ulioshuhudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, Ikulu, jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.
 Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini Mhe. Dkt. Musenero Masanza wa Uganda akizungumza kwenye mkutano wa Waandishi wa Habari baada ya hafla ya utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga kama Kituo cha Nishati cha Kikanda ulioshuhudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, Ikulu, jijini Dar es Salaam,
tarehe 06 Agosti, 2026.


Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akutana na Kuzungumza na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, Ikulu Jijini Dare es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakishuhudia utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga kama Kituo cha Nishati cha Kikanda katika viwanja vya Ikulu, jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026. Hati hiyo ya Makubaliano imesainiwa kati ya Shirika la Maendeleo la Petroli Tanzania (TPDC) chini ya Mkurugenzi Mtendaji Bw. Mussa Makame, Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Uganda (UNOC) chini ya Mkurugenzi Mtendaji Bi. Proscovia Nabbanja pamoja na Kampuni ya Biashara ya Mafuta na Nishati ya Vitol ya Bahrain, chini ya Mkurugenzi Mtendaji wake Tom Baker.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakishuhudia utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga kama Kituo cha Nishati cha Kikanda katika viwanja vya Ikulu, jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuhitimisha ziara rasmi ambapo walishuhudia utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga kama Kituo cha Nishati cha Kikanda kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.

Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: