Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) imeanza uchimbaji wa kisima eneo la Kisasa-Mwangaza Jiji Dodoma baada ya maagizo ya Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb.) kwa DUWASA kutafuta suluhisho la changamoto ya maji katika maeneo ya Kisasa Bwawani, Kisasa East, Nyumba 300 na Mwangaza.

Zoezi la uchimbaji wa kisima hicho umeanza Oktoba 11 na utakamilika Oktoba 12, 2024 huku hatua inayofuata ni upimaji wa wingi wa maji na ubora wa maji kabla ya kuanza uendelezaji wa kisima hicho.

Uchimbaji kisima eneo la Kisasa - Mwangaza ni hatua ya utatuzi wa changamoto ya ukosefu wahuduma ya maji kwa wananchi wa maeneo ya Kisasa Bwawani, Kisasa East, Nyumba 300 na Mwangaza.

Baadhi ya Wananchi na Viongozi wa Serikali ya Mtaa Nyumba 300 na Mwangaza wameishukuru serikali kwa kusikia kilio chao katika kuwapatia huduma ya maji.

Viongozi na wananchi waliotembelea uchimbaji wa kisima hicho leo ni Donatha Zitatu - Mwenyekiti wa Mtaa Nyumba 300, Vicent Malisa Balozi Mwangaza, Pendo Masigati- Mwananchi wa Nyumba 300 na Mathew Laurent- Balozi Nyumba 300.
Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: