Wafanyakazi wa Barrick wakifurahi baada ya kumaliza kushiriki mbio hizo
Wafanyakazi wa Barrick wakishiriki kukimbia mbio za CRDB Bank Marathon 2024
Wafanyakazi wa Barrick wakishiriki kukimbia mbio za CRDB Bank Marathon 2024

Na Mwandishi Wetu.

Wafanyakazi wa kampuni ya Barrick nchini kupitia klabu zao za mchezo wa marathon wameshiriki katika mbio za msimu wa tano wa mbio za CRDB Bank Marathon, zilizofanyika jijini Dar es salaam.

Mbio hizo zililenga kuchangisha fedha kwa ajili ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia watoto,huduma za afya kwa akina mama na vijana.

Wakimbiaji kutoka Barrick Runners clubs wamekuwa wakishiriki marathon mbalimbali zinazofanyika nchini na nje ya nchi hususani zinazolenga kuchangia kupambana na changamoto mbalimbali za kijamii.

Kampuni pia imekuwa na program za mazoezi kwa ajili ya wafanyakazi wake kwa ajili ya kuhakikisha wanakuwa na nguvu na afya bora pia imewekeza katika miundombinu ya michezo na mazoezi kwa ajili ya kuwawezesha wafanyakazi wake kushiriki michezo na mazoezi katika mazingira rafiki.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: