Ni wazi Simba kwa sasa inabadilika na kila mchezaji anaonyesha thamani yake.
Kocha anawapa wengi nafasi ili kila mmoja aonyeshe kipaji chake na wanafanya hivyo.

Kikosi kichoanza mechi na Kmc ni wachezaji watatu walioanza mechi na Lipuli ndio walianza.

Hii ina maana pia ni ngumu kwa mpinzani wako kujua unakuja na kikosi gani ili apange mbinu za kukudhibiti.

Kmc walikuja tofauti sana. Walikuja wamekamia na wamedhamiria kupata chochote kwenye mechi ile. Ila mwisho tofauti ya Simba na Kmc ilionekana.

Bado Grayson Fraga alithibitisha waliomlipia nauli kutoka Brazil kuja Tanzania hawakukosea wala hawakutupa hela zao. Ni mchezaji wa kisasa. Hana Mambo mengi na kila analolifanya ni kwa faida ya Timu.

Hutamwona akipiga kanzu au chenga zisizo na sababu. Utamwona anapokonya mpira na haraka mno anaupeleka kinakotakiwa na utafika. Shida anayopata anapenda sana mpira wa kasi Ila wenzie bado hawajafikia kasi yake.

Simba inacheza vizuri mno Ila bado ni taratibu sana. Inatakiwa sasa wakivuka mstari wa katikati kuelekea kwa adui kuwe na kasi zaidi ili kuwachanganya mabeki wa timu pinzani.

Pia inabidi nafasi zinazotengenezwa wazifanyie kazi kuzigeuza magoli kwa pamoja na kufunga magoli mengi nafasi zinazopotea ni nyingi kuliko kuliko zinazokuwa magoli.

Hasan Dilunga ni mchezaji mzuri Ila kwa sasa hayupo kwenye kiwango chake kwa tunaomjua tunajua anaweza kufanya Mara mbili ya anachokifanya sasa. Pamoja na kwamba goli la kwanza lina mchango mkubwa sana kutoka kwake bado tunajua ana kitu cha ziada kuliko anachofanya sasa.

Chama ni Kama anazaliwa upya amejua kwamba yupo timu anapaswa kuendana na ukubwa wa Timu. Taratibu namuona Chama wa msimu uliopita anaanza kurejea. Kahata anathibitisha jicho lililomwona Gor mahia halikukosea.

Kuna watu wanahoji kiwango cha Kager. Kagere ni yule yule na kiwango ni kile kile Ila watu walishakariri kwamba mipira yote mbele lazima apewe Kagere kitu ambacho ilikuwa rahisi tu kwa wapinzani kwamba ukimkaba Kagere basi ni ngumu sana kufungwa goli na Simba na kocha ameliona hilo. Hivyo ametoa majukumu kwa watu wengine nao kutengeneza nafasi na kufunga. Hii inasaidia sana mabeki wote wanapowekeza kwa Kagere wengine wanakuwa huru wanafunga.

Tunakoelekea wapinzani watapata tabu sana kwamba wamkabe nani kwani kila mtu anafunga hii ndio mbinu mpya ya mwalimu na ninaamini kuna baadhi ya mechi ataruhusu Kagere asimame na wanzie wampe mipira afunge na atafunga. Ile Simba ya kuikariri na kujua inakuja kucheza kwa mfumo fulani haipo tena.

Hii ni Simba ya kubadilika kulingana na mechi. Hii ndio tafsiri sahii ya kikosi kipana. Huwezi kujua leo nani anacheza na nani anakaa benchi. Simba sio tena timu ya kugombea ubingwa wa Tanzania bara ni timu inayotakiwa sasa kuanza kutazama mbali. Huu ubingwa wa ligi hata kikosi Cha tatu kinaweza tu kutwaa ubingwa.

Tunaanza sasa kujenga timu ya kushindana Afrika ndani tushamaliza.
( Jicho la tatu la Mgalilaya).
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: