Ndugu zangu,

Wakati huu tunapoungana na ndugu,  jamaa na rafiki zetu waliopoteza wapendwa wao katika ajali ya Moto hapa Morogoro ni vyema tukatambua kuwa :

- Si kila aliyeathirika na ajali hii ya Moto alikuwa anaenda KUIBA mafuta

- Kauli tunazozitoa zinaongeza MAJERAHA kwa waathirika wa ajali walionusurika na wale waliopoteza wapendwa wao

- Waathirika walionusurika wanahitaji FARAJA na MSAADA wetu wa kila namna hivyo shime kila mmoja kwa nafasi yake aone namna anavyoweza kushiriki katika hili jambo la kijamii

Hebu fikiri Mgonjwa mahututi ambaye muda huu yuko ICU na amejikuta akiwa muathirika wa hili kwa kuwa alikuwa akikimbilia KUMNUSURU MTOTO au MTU ambaye aliona ameelemewa na kutokana na kuwa na UHABA wa MAARIFA juu ya UOKOZI katika majanga ya moto akabeba NDOO YA MAJI na kwenda KUSAIDIA kunusuru MOTO usisambae au MTU ANAYEUNGUA apate kunusurika bila ya kujua kuwa MAJI hayafai kuzima Moto kwa kuwa yanaenda kuongeza OXYGEN na kufanya MOTO ukolee zaidi.

Nashauri ndugu zangu wapendwa,  tuweze kuachia kamati zilizoundwa kuchunguza zikafanya kazi zetu huku TUKICHUNGA NDIMI ZETU na kujizuia kutumia MAJANGA kama haya au yanayofanana na haya kujinufaisha ama KISIASA au kwa namna iwayo yoyote ile.

MUNGU aturehemu na kutuongezea maarifa na moyo wa uwajibikaji huku kila mmoja akiona anao wajibu wa KIZALENDO katika KUILINDA na KUIJENGA Nchi yetu pendwa ya TANZANIA.

Amen.

========== ASANTE ===========

Godwin D.  Msigwa
Morogoro
Tanzania
11 Agosti 2019
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: