Kikundi cha ngoma za asili kikitoa burudani kabla ya Mkutano wa Mawaziri wa Bonde la Mto Zambezi (ZAMCO) kuanza mkutano huo unalenga kujadili mpango mkakati wa miaka 20 kwa Bonde la Mto Zambezi, na unashirikisha Mawaziri kutoka nchi nane Wanachama wa ZAMCO, yaani Angola, Botswana, Malawi, Msumbiji,Tanzania, Zambia na Zimbabwe uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha kimataifa Julius Nyerere kuanzia Februari 26 mpaka Februari 28.
Mkurugenzi Msaidizi wa Maji Shirikishi kimataifa Sylivester Matemu akitoa utambulisho kwa Mawaziri wa nchi wanachama wa ZAMACO (hawapo pichani) katika Mkutano wa Mawaziri wa Bonde la Mto Zambezi (ZAMCO) unaolenga kujadili mpango mkakati wa miaka 20 kwa Bonde la Mto Zambezi, na unashirikisha Mawaziri kutoka nchi nane wanachma za ZAMCO uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha kimataifa Julius Nyerere kuanzia Februari 26 mpaka Februari 28.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof. Makame Mbarawa akitoa hotuba ya kufungua mkutano wa Mawaziri wa Bonde la Mto Zambezi (ZAMCO) unaolenga kujadili mpango mkakati wa miaka 20 kwa bonde la mto Zambezi, uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha kimataifa Julius Nyerere kuanzia Februari 26 mpaka Februari 28.
Picha ya pamoja.
Baadhi ya washiriki wa Mkutano wa Nchi Wanachama wa ZAMCO wakifuatilia mkutano wa ZAMCO, unaolenga kujadili mpango mkakati wa miaka 20 kwa bonde la mto Zambezi, uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha kimataifa Julius Nyerere kuanzia Februari 26 mpaka Februari 28.(Picha na Paschal Dotto-MAELEZO).

Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa, amefungua Mkutano wa Saba wa Mawaziri wa Maji wa nchi nane zilinazohusiana na Bonde la Mto Zambezi (Zambezi Watercourse Commission – ZAMCOM) na kuitaka jamii ya mataifa hayo kuona umuhimu wa kamisheni ya chombo hicho kuendelea kuimarika na kusimamia raslimali za ZAMCOM kwa manufaa yaliyokusudiwa.

Waziri Prof. Mbarawa alikuwa anafungua kikao cha Baraza la Mawaziri wa Maji katika Ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, vikao vikiwa ni Mkutano wa Sita wa Baraza la Mawaziri Februari 26 – 27 na Mkutano wa saba wa Kamati ya Wataalaam ya ZAMCOM, nchi husika zikiwa ni Angola, Botswana, Msumbiji, Malawi, Namibia, Zambia, Zimbambwe na Mwenyeji Tanzania.

Mkataba wa Kamisheni ya Bonde la Mto Zambezi ulianza rasmi mwaka 2011 kwa lengo la kusimamia raslimali za maji za Bonde la Mto Zambezi, Tanzania ambayo ni mwanachama maji yake toka Ziwa Nyasa, kwa wastani wa asilimai 16 ya maji yaingiayo Ziwa Zambezi kwa mito, humwagika Ziwa Zambezi na Bonde hilo linahitaji hifadhi na zipo fursa za kuwepo miradi ya manufaa kwa nchi hizo.

Baraza limepokea Mpango kazi (Strategic Plan) na Mfumo wa kubadilishana, kutumia na kuhifadhi takwimu za raslimali za Maji kwa njia ya TEHAMA, ambapo Tanzania imemaliza muda wake wa Uenyekiti na nafasi hiyo kupewa Zambia.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: