Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Rais wa Zimbabwe, Mhe. Emmerson Mnangagwa baada ya kuapishwa kwake jijini Harare, Zimbabwe leo. Dkt. Kikwete amehudhulia sherehe hiyo akiwa amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, ambapo aliambayana na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Phillip Mangula pamoja na Mwenyekiti wa UDP, John Momose Cheyo.
Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Katibu Mtendaji Mkuu wa SADC, Dkt. Stergomena L. Tax walipokutana kwenye sherehe za kuapishwa Rais mpya wa Zimbabwe, Mhe. Emmerson Mnangagwa zilizofanyika leo mjini Harare, Zimbabwe. Dkt. Kikwete amehudhulia sherehe hiyo akiwa amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, ambapo aliambayana na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Phillip Mangula pamoja na Mwenyekiti wa UDP, John Momose Cheyo.
Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na viongozi mbalimbali baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Robert Gabriel Mugabe, mjini Harare Zimbabwe, alikokwendwa kwa kumuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, kwenye sherehe za kuapishwa Rais mpya wa Zimbabwe, Mhe. Emmerson Mnangagwa zilizofanyika leo mjini Harare, Zimbabwe.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: