Mwenyekiti wa Chama cha Riadha Mkoa wa Tanga Sophia Wakati akizungumza.
Na Oscar Assenga, Tanga.

CHAMA cha Riadhaa Mkoa wa Tanga (RT) kimesema kwamba kitampa ushirikiano wa kutosha muandaaji wa Mashindano ya Riadhaa ya Tanga City Marathon ili kuweza kuondoa changamoto zilizojitokeza msimu uliopita na yaweza kuwa na tija na mafanikio makubwa.

Hayo yalisemwa leo na Mwenyekiti wa Chama cha Riadha (RT) Mkoa wa Tanga Sophia Wakati alipokuwa akizungumza na vyombo bya habari kuhusu namna walivyojipanga kuhakikisha wanampa ushirikiano wa kutosha muadaaji huyo ili mashindano hayo yaweze kufanyika kwa ufanisi.

Alisema pia kuweza kufanyika vizuri kwa kufuata taratibu zote za Mashindano hayo kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga kupitia Afisa Michezo Mkoa

“Mbio hizi za Tanga City Marathon ni mashindano muhimu kwa mchezo wa Riadha mkoani hapa na kwa sasa tumeyaingiza kwenye kalenda ya Mkoa na sasa yatakuwa yakifanyika kila mwaka na sisi RT kwa kushirikiana na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga tutatoa ushirikiano wa kutosha kwa waandaaji”Alisema Sophia Wakati.

Mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika Septemba 22 mwaka huu ambapo yataanzia kwenye Hotel ya Tanga Beach Resort na kuzunguka maeneo mbalimbali Jijini Tanga na kuishia hapo huku yakishirikisha wakimbiaji katika makundi matatu ya Kilomita 21,10 na 5 za kujifurahisha.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: