Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2023, Ndugu Abdallah Shaibu Kaim akipanda mti katika Bwawa la kuhifadhi Maji Mabayani lililopo eneo la Pande wakati wa ziara ya Mwenge wa Uhuru kitaifa Mkoani Tanga.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2023, Ndugu Abdallah Shaibu Kaim akiweka udongo kwenye mti katika Bwawa la kuhifadhi Maji Mabayani lililopo eneo la Pande wakati wa ziara ya Mwenge wa Uhuru kitaifa Mkoani Tanga.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2023, Ndugu Abdallah Shaibu Kaim akipanda mti katika Bwawa la kuhifadhi Maji Mabayani lililopo eneo la Pande wakati wa ziara ya Mwenge wa Uhuru kitaifa Mkoani Tanga.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2023, Ndugu Abdallah Shaibu Kaim amepanda mti katika Bwawa la kuhifadhi Maji Mabayani lililopo eneo la Pande wakati wa ziara ya Mwenge wa Uhuru kitaifa Mkoani Tanga.

Ambapo sambamba na ukaguzi na uzinduzi wa Miradi mbalimbali ya kimkakati, ziara hiyo imejikita pia katika ukaguzi wa utekelezaji wa miradi ya utunzaji mazingira, hususani vyanzo vya maji.

Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge Kitaifa wakati wa ziara hiyo ameipongeza TANGA UWASA kwa jitihada za utunzaji wa vyanzo vya maji na uhifadhi wa mazingira wakati akipokea taarifa ya shughuli za uhifadhi wa vyanzo vya maji katika ziara yake eneo la Mabayani.

"Nawapongeza TANGA UWASA kwa kazi nzuri na jitihada za uhifadhi wa vyanzo vya maji na tuendelee kuwahamisha wananchi kulinda na kutunza Mazingira", ameeleza Ndugu Kaim.

Mkoa wa Tanga umeupokea Mwenge wa Uhuru 2023 tarehe 09.06.2023 kutokea Mkoa wa Kusini Pemba, ambapo kauli mbiu kwa Mwaka huu ni: " TUNZA MAZINGIRA, OKOA VYANZO VYA MAJI KWA USTAWI WA VIUMBE HAI NA UCHUMI WA TAIFA".
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: