Kulia Mratibu wa Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Bw. Salim Mwinjaka, akizungumza wakati wa ujumbe huo ulipotembelea Ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita, ujumbe huo upo katika ziara maalum ya ukaguzi wa maeneo yanayotekeleza program hiyo ya AFDP.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita Profesa Godius Kahyarara akizungumza na ujumbe na wataalam kutoka Program ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) haupo katika picha ulipotembelea ofisini kwake jana jioni. ujumbe huo upo katika ziara maalum ya ukaguzi wa maeneo yanayotekeleza program hiyo ya AFDP.
Kushoto Bi Jackline Motcho, Afisa wa Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi nchini (AFDP) akizungumza na baadhi ya wajumbe waliokuwepo katika ziara ya ukaguzi wa maeneo yanayotekeleza mradi huo katika kijiji cha Rubambagwe Wilayani Chato, Mkoani Geita.
Bi. SIFA Bujune, ni mfugaji wa viumbemaji katika kijiji cha Rubambagwe kilichopo Wilayani Chato, Mkoani Geita, akizungumzia baadhi ya changamoto wanazokutana nazo katika majukumu yao.
Picha ikionesha moja ya jengo lililojengwa katika kijiji cha Rubambagwe na Mradi wa kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) litakalo tumika wakati wa kutoa mafunzo kwa wafugaji wa viumbemaji

Na Mwandishi wetu - CHATO

Imeelezwa kuwa Mradi wa kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) unakwenda kutatua changamoto wanazokumbana nazo wafugaji VIUMBEMAJI katika kituo Cha Rubambagwe kilichopo Wilayani Chato,mkoani Geita.

Hayo yameelezwa Leo na Dkt. Nazaeli Madala, Mkurugenzi wa ukuzaji viumbe Maji kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Dkt. amesema kituo Cha Rubambagwe kipo katika UJENZI ambapo, Nia na madhuni ya kituo hiki ni kuhamasisha, kuendeleza na kusimamia ukuzaji viumbe Maji,Kwa maana Ufugaji wa samaki kwa mabwawa na vizimba katika ukanda wa ziwa Victoria.

Alisema kuwa, kituo kitakwenda kutoa mafunzo ya utengenezaji wa chakula cha samaki,Ufugaji na ulishaji sahihi wa samaki, wafugaji watafundishwa pia namna ya kutengeneza chakula Cha samaki Kwa kutumia malighafi za asili, kutakuwa na majengo ambayo yatawezesha wafugaji wanaotoka mbali kukaa hapo wakati wa mafunzo, sambamba na hilo, kutakuwa na kiwanda kidogo Cha kutengeneza chakula cha samaki.

Aliongeza kusema kuwa kituo pia kitazalisha vifaranga vya samaki ili kuweza kutatua changamoto ambazo wafugaji wanakutana nazo "kutakuwa na kitotoleshi ambacho kitakuwa na uwezo mkubwa sana wa kuzalisha vifaranga ambavyo vitakwenda kuwezesha vitotoleshi vya sekta binafsi kupata wazazi "Alifafanua

Akiongea na ujumbe huo, Bi. Sifa Buguni mmoja wa wafugaji wa samaki Rubambagwe Chato alibainisha changamoto kubwa mbili walizokumbana nazo kabla ya mradi huu kukamilika kuwa ni pamoja na uhaba wa upatikanaji wa mbegu na chakula cha kulisha samaki.

Awali, ujumbe huu wa IFAD ulifika ofisini Kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita Prof. Godius Kahyarara ambapo alisema ni wakati sasa kwa wakazi wa Mkoa wa Geita kujikita katika katika shughuli za kilimo na ufugaji wa viumbemaji na kwa uwekezaji wa uhakika kuweza kuwekeza katika sekta hizo kama wanavyowekeza katika sekta ya madini.

Ujumbe kutoka IFAD, wataalam na Mratibu wa Programu hiyo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Bw. Salim Mwinjaka wapo katika ziara ya ukaguzi wa maeneo yanayotekelezwa mradi huo.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: