Mjumbe wa halmashauri kuu (MNEC UWT), Halima Okashi akitoa zawadi kwa Mmoja ya Wanawake waliolazw aktika wodi ya wamama katika Hospitali ya Mwananyamala ambapo UWT Kinondoni walifika katika hospitali hiyo kutoa Msaada katika kuadhimisha  siku ya Wanawake Dunia.
 Katibu wa UWT CCM Wilaya ya Kinondoni, Nuru Mwaibako, akiwa na Diwani Viti maalum CCM  Kinondoni  Frolenece Masunga wakikabidhi zawadi kwa Wanawake waliofka katika Clinic ya Hospitali ya Mwananyamala na watoto wao, UWT Kinondoni wamefanya maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani kwa kuwatembelea wamama waliopo katika Hospitali ya Mwananyamala.
Diwani Viti maalum CCM  Kinondoni  Frolenece Masunga akiwa amemshika mmoja ya Watoto waliofika kutibiwa katika Hospitali ya Mwananyamala leo wakati wa maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani.

Ujumbe wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Kinondoni kwa Pamoja wakimkabidhi zawadi Mganga wa Hospitlai hiyo kwa ajili ya Wanawake wa Hospitali hiyo.

Ujumbe wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Kinondoni, ukiwasili katika Hospitali ya Mwananyamala ukiongozwa na Mjumbe wa halmashauri kuu (MNEC UWT), Halima Okashi.
Kajunason Blog

Kajunason Blog

A Tanzanian blog operating since October 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.

Toa Maoni Yako:

0 comments: