Theodosia Mhulo kutoka WLAC Akifungua maadhimisho hayo katika ofisi za
REDESO zilizopo Kinondoni jijini Dar es Salaam, ambapo alitoa wito kwa
wana harakati na Wadau kwa ujumla kuanza kuwatumia Wanaume kama chachu
ya mabadiliko katika vita ya ukatili wa Kijinsia nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya REDESO, Abeid Kasazi akizungumza
kabla ya kumakaribisha mgeni rasmi kufungua maadhimisho ya siku 16 za
kupinga ukatili wa kijinsia Duniani kote, yaliyofanyika katika ofisi za
Taasisi hiyo zilizopo Kinondoni Jijini Dar es Salaam.
Mshauri kutoka REDESO, Brigitha Sedekia akitoa somo juu ya ukatili wa
kijinsia kwa watu waliofika katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga
ukatili wa kijinsia.
Sehemu ya wageni waalikwa waliokuwa wamekaa Meza kuu wakati wa Maadhimisho ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia Duniani wakishiriki kuimba kwa
pamoja.
Kundi
la Muziki la Wakimbizi linalojulikana kwa jina la Bana ba Zambe wakitoa
Burudani wakati wa Maadhimisho ya Siku 16 za kupinga ukatili wa
kijinsia Duniani
Sehemu ya wageni waalikwa walioshiriki katika Maadhimisho ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia Duniani.
Toa Maoni Yako:
0 comments: